Zainab j
JF-Expert Member
- Sep 24, 2018
- 1,816
- 2,368
Wakuu habari,
Mke wangu mdogo (nyumba ndogo) anafanya biashara sehemu maeneo ya wilaya ya Kinondoni, sasa huyo mwanamke nishamkataza mara kibao kwenda huko kwa Mwamposa. Maana yupo tayari afunge biashara aende huko kwa huyo nabii wao. Majukumu ya watoto hayupo makini nayo, yeye Mwamposa, Mwamposa na yeye huna lakumwambia kwakweli.
Cha kuchekesha juzi usiku nimekuta mchanga ndani umewekwa kwenye mfuko, mimi nikishangaa sana nakujiuliza nini hiki sasa?
Basi alivyorudi nikamuuliza vipi mbona nimekuta mchanga kwenye mfuko ndani kama umechotwa sehemu (maana una vimajani majani). Basi akanijibu eti ameuchota kwenye eneo lake la biashara na aliupeleka kwa Mwamposa hili uombewe, then akaumwage pale sehemu yake ya biashara.
Kwahiyo umeshaombewa tayari, anasubiria usiku akaumwage pale sehemu anayofanyia biashara.
Aisee, niliumia nafsi yangu sana, jamani huu sasa si sawa na ushirikina kabisa kabisa.
Mnavyowaponda waganga wa kienyeji, mbona haya pia kama mambo ya kichawi na ya kijini, ukiona mtu anaagiza uchote mchanga sehemu ukaombewe, au nguo ya mtu aliepotea ikaombewe, hayo mambo ya kijini na mashetani ndio wana masharti hayo.
Nahisi hawa wanaojiita manabii wanatumia majini kwenye mambo yao kwa 90%.
Mke wangu mdogo (nyumba ndogo) anafanya biashara sehemu maeneo ya wilaya ya Kinondoni, sasa huyo mwanamke nishamkataza mara kibao kwenda huko kwa Mwamposa. Maana yupo tayari afunge biashara aende huko kwa huyo nabii wao. Majukumu ya watoto hayupo makini nayo, yeye Mwamposa, Mwamposa na yeye huna lakumwambia kwakweli.
Cha kuchekesha juzi usiku nimekuta mchanga ndani umewekwa kwenye mfuko, mimi nikishangaa sana nakujiuliza nini hiki sasa?
Basi alivyorudi nikamuuliza vipi mbona nimekuta mchanga kwenye mfuko ndani kama umechotwa sehemu (maana una vimajani majani). Basi akanijibu eti ameuchota kwenye eneo lake la biashara na aliupeleka kwa Mwamposa hili uombewe, then akaumwage pale sehemu yake ya biashara.
Kwahiyo umeshaombewa tayari, anasubiria usiku akaumwage pale sehemu anayofanyia biashara.
Aisee, niliumia nafsi yangu sana, jamani huu sasa si sawa na ushirikina kabisa kabisa.
Mnavyowaponda waganga wa kienyeji, mbona haya pia kama mambo ya kichawi na ya kijini, ukiona mtu anaagiza uchote mchanga sehemu ukaombewe, au nguo ya mtu aliepotea ikaombewe, hayo mambo ya kijini na mashetani ndio wana masharti hayo.
Nahisi hawa wanaojiita manabii wanatumia majini kwenye mambo yao kwa 90%.
