Kujitetea hakutakusaidia kutokuonekana watu ambao hamjaelimika mkuu. Ni ukweli usiopingika kwamba "WAKURYA" hamjaelimika na mna mambo ya ajabu sana kulingana na sababu zifuatazo;
1. Kupigana wenyewe kwa wenyewe. Sababu kubwa ni kuibiana ng'ombe mfano warechoka. Hii ni ishara tosha kuwa elimu kwenu n muhimu sana. Mnaweka vita mbele badala ya kufanya mambo yanayoleta maendeleo. Ndiyo maana asilimia kubwa ya wakurya mnaishi kwenye vijumba vya nyasi na hata hamjui kama kuna kitu kinaitwa choo.
2. Pia wengi wenu elimu mnaikimbia na kubaki kufuga ng'ombe wengi ambao hawawasaidii chochote kwa sababu wanakuwa kama mapambo tu. Maana unakuta mna shida zinazowaandama mpaka kwenye damu ila hamuuzi hao ng'ombe wawasaidie. pia bado mnaishi maisha ya kizamani kwa kulala kwenye ngozi, vitanda vya kufunga kwa kamba etc.
3. Suala la kuoa wanawake wengi na kuwatelekeza. Wakurya hasa wanaume wana ubwege sana wa kuoa wanawake wengi na kuwatelekeza hao wanawake. Unakuta mwanamke ndiyo hupambana ili watoto wake wasome na wapate hata cha kuweka kinywani. Kazi ya mwanaume ni kwenda kunywa pombe za kienyeji akirudi anaomba chakula ambacho hajui kimepatikanaje.
4. Kuhusu suala la ukeketaji nyie mmekuwa watu ambao siyo waelewa kwa sababu mmekuwa mkiwakeketa watoto wengi kwa kiwembe kimoja. Pia yule ngariba huwa havai hata grovuzi ili kulinda afya za watoto wenu. Hakika tukiweza kumaliza hili suala la ukeketaji kwa kurya itakuwa rahisi sana kulimaliza kwa makabila mengine kwa sababu wakurya ni watu wenye uwezo mdogo wa kuelewa mambo na ni wagumu sana kuelewa kuwa kitu fulani hakifai.
Acheni mambo ya ajabu ambayo hayana tija katika jamii ili muweze kuwapa watoto wenu elimu iliyo bora. Kama muda wote mnawaza vita na kunoa mapanga utakumbuka suala la mwanao kupata elimu iliyo nzuri katika shule iliyo bora?
ungekuwa si mshamba ungejua kuwa siyo kila anayepingana na hoja zako kwenye hii post ni mkurya!!
Ninakujibu uharo wako kama ifuatavyo:
1. suala la wakurya kupigana wenyewe kwa wenyewe halihusiani na elimu kwa namna yoyote ile maana mapigano yao yana sababu, koo zote za kikurya zinaishi kwa kutumia kanuni ya
SURVIVAL FOR THE FITTEST, kwa mfano koo moja imeibiwa ng'ombe halafu iseme imestarabika na kuacha zichukuliwe kijinga jinga tu ili wewe useme wameelimika, unajielewa kweli?
UKURYANI koo zinaishi kwa kujijenga zaidi ili kuwa na nguvu kuliko koo nyingine, koo fulani ikijifanya iliyostarabika itaibiwa mali zote na koo nyingine. kwahiyo jitahidi ujisomee na kujua historia yao usikurupuke.
halafu pia kaa ukijua elimu kwa watanzania wengi bado sana ukiwemo na wewe mwenyewe.
usingekuwa mshamba ungejua kuwa siyo wakurya tu wanaoishi kwenye nyumba za nyasi hapa TZ maana jamii nyingi za watanzania hasa vijijini wanaishi kwenye nyumba za nyasi. kuhusu kuwa na choo, usichokijua ni kuwa kuna watanzania wengi vijijini na shule nyingi tu kwenye mikoa mingi hapa TZ hazina hata choo kwahiyo kama ulidanganywa kuwa ni wakurya tu hawana choo pole sana. hata hivyo utafiti huo wa wakurya kutokuwa na choo uliufanya lini?
2. kufuga ng'ombe wengi si kwa wakurya tu hapa TZ, ungekuwa si mshamba ungelijua hili, jamii ya wakurya wa sasa wana ng'ombe wa kawaida kabisa tena wengi wao wanauza maziwa yao kwenye viwanda kama MARA MILK na kwingineko tena kuna wafugaji wengi wameanza kuuza ng'ombe na kuwekeza kwenye real estates huko musoma, tarime , mwanza, mugumu na kwingineko.
3. suala la kuoa wanawake wengi na kuwatelekeza ni la mtu mmoja mmoja, hata jamii zingine hapa tz zinaoa wanawake wengi tu na kuwatelekeza, juzi juzi huko Dar walijitokeza wanawake kibao waliotelekezwa na waume zao, kwani hao walikuwa wakurya? ungekuwa si mshamba ungelijua hili.
4. suala la ukeketaji linafanywa na jamii nyingi tu hapa TZ si kwa wakurya tu, tena kwa wakurya kila mkeketwaji huenda na viwembe vyake mwenyewe na si kweli kwamba wanachangia kiwembe kimoja. usichojua ni kuwa suala la ukeketaji linapungua kwa kasi kubwa huko kwa wakurya kulingana na wao wenyewe wanavyobadilika siyo kama wewe unavyotaka.
umesema wakurya wanauelewa mdogo, umeupima vipi uelewa wao? je una
study yoyote uliyofanya kuhusu uelewa wao uweke link hapa tuisome hiyo study au research, au unajifanya kujua usicho na uhakika nacho?
jisomee brother kabla hujaja humu kudanganya watu.