Wakurya acheni ushamba na tabia za kizamani

Wakurya acheni ushamba na tabia za kizamani

Kwani wamekula nini chako? Ulaya wanapromoti ushoga tena kwa sheria kali lakini wanawazuga nyie kuachana na mambo yenu kwa ghiriba kali. Dunia ni kubwa sana na mtambue haiwezi na hatuwezi kuwa sawa, ni vizuri sahivi tuna haki za makundi na walio wachache ...tuwaache kwasababu nao ni kundi lao na ni haki yao. Wakataeni wanaowatuma ili waachane na ushoga huko makwao kwasababu Tz hatuukubali kisha ndo mje kuwa wafuasi wazuri wa mahubiri yao juu ya mila zetu nzuri
 
kwahiyo wewe unashauri asipige yowe afanyeje au unataka alete matarumbeta na kigodoro!!?
huko unakosema kuna matarumbeta na vigodoro hawana uhalifu? umesha wahi ona wanaume wanakusanyana na pinde na mishale? miaka hii ya utandawazi tena mjini kabisa? mbadilike mtu kaibiwa kuku mishipa yashingo inataka kupasuka kisa yowe anagonga lipsi kwa viganja vya mikono karibia azichane kisa kaibiwa kuku

badilikeniiiiiii
 
Historia ya ukeketaji kwa wakurya-

Wakurya ni kabila lenye asili ya mkoa wa Mara ,na Mkoà wa Nyanza huko nchini Kenya

Wakurya wa nchini Kenya asilimia kubwa ni wakulima na Wakurya wa Tanzania asilimia kubwa ni wafugaji na wakulima

Wakurya wamepakana na makabila yafuatayo kwa upande wa Tanzania,Upande wa Mashariki wamepakana na wamasai,na upande magharibi wamepakana na Wajeluo,kusini wamepakana na wasukuma,ingawa kuna vimakabila vidogo vyenye asili ya kikurya vimejitenga na kujiita makabila yao kama waikizu,wangoreme,Wakabwe nk
Upande wa kusini Magharibi kuna Wajita na Wazanaki

Ukeketaji

Inaanminika kuwa Wakurya ni moja ya makabila ambayo kipindi wanaingia kwenye ardhi ya Afrika Mashariki wakitokea kaskazini mwa Bara la Afrika,misri na Mashariki ya kati walikuwa hawana mila hii ya ukeketaji na kutoboa masikio

Walipofika hapa Afrika Mashariki waliishi pembezoni mwa mto Mara kwa ajili ya shughuli za kiuchumi ufugaji na kilimo

Wakati huo wanaingia hayo maeneo waliwakuta wamasai ambao walikuwa wanakaa maeneo hayo kwa ajili ya ufugaji na makazi

Wakurya na Wamasai walianza vita, wamasai wakipinga wakurya kuvamia maeneo yao
Hiyo vita ilipigana kati ya 100 AD
Wamasai walishindwa ile vita na kukimbilia Arusha na Masai Mara

Hata hivyo wamasai hawakukubali kushindwa ile vita na Wakurya,baadae Wamasai walijipanga kuvamia Wakurya ili wawanyang'anye ardhi na mifugo yao

Mwaka 1500 BC Wamasai walipigana vita kubwa dhidi ya wakurya kando kando na mto mara vita ambayo wakurya walipata hasara sana,na wakakubali kushindwa

Wamasai wakaanza kuwatawala Wakurya katika nyanja zote,
Wakurya wakaanza kulazimishwa kutahiri wavulana na kukeketa wasichana na kutoboa masikio kama ishara ya kuwatambua kama ni sehemu ya wamasai

Hadi mwaka 1700 BC Wakurya wanawaondoa Wamasai kwenye ardhi ya wakurya,wakurya waliendelea na mila ya ukeketaji na kutahiri na kutoboa masikio

Hivyo ndivyo wakurya walianza hiyo mila

Chanzo: Oral sources
 
Kumbe unaweza ukawa mshamba halafu usijijue badala yake ukaanza kuita wengine ndiyo washamba,


uchambuzi wako umejaa makosa ya kifikra (logic and reasoning) kwa sababu zifuatazo;

1. siyo wakurya tu wanaokeketa watoto wa kike hapa Tanzania (ungekua siyo mshamba ungelijua hili). Hivyo ulitakiwa kukemea makabila yote yanayofanya ukeketaji. Kwa kushindwa kwako umedhihirisha chuki binafsi tena za kizamani.


2. Suala la ukatili kwa wanawake limekuwa janga la dunia ya sasa, tena matukio ya juzi juzi yanathibitisha hili, yule mganga mfawidhi aliyeuawa na mmewe, yule mhadhiri wa chuo kikuu cha UDOM aliyeuawa na mmewe n.k hao wanaume wote walioua siyo wakurya. Hivyo basi ungekua siyo mshamba ungelitambua hili.


3. Kuhusu ubabe wa wanaume wa kikurya umeuchambua kitoto sana kana kwamba hata historia ya makabila mbalimbali hujawahi kusoma (huu ni ushamba mkubwa). Umeshindwa kufahamu kuwa wakurya ni kabila la vita tangu zamani (warrior tribe). Unapotaka wanaume wa kikurya wawe mdebwedo utasubiri sana ewe mshamba. Nakushauri utafute historia ya warrior tribes hapa Afrika Mashariki ili uelimike (tafuta historia ya wakikuyu, wamasai, wakurya, wakamba, watutsi, wanyankole n.k ndipo utajua wakurya hawawi majasiri usiku mmoja bali wana vinasaba vya kuwa hivyo walivyo.


4. Umesema wakurya wafute hela, kumbe hata hujui kuwa wanaume wa kikurya kwa miaka hii wanatafuta hela sana na wanazipata haswaa. Nenda Mwanza ulizia wakurya wanavyotafuta hela, kwa miaka hii biashara kubwa Mwanza zinaanza kumilikiwa na wakurya, wahindi, wachaga na wanyantuzu.


Angalizo: Acha kusubiria embe chini ya mkuyu! Huwezi kutegemea eti siku moja wakurya/watutsi/wakikuyu/wanyantuzu watakuwa wapole na wajinga wajinga kama wasukuma wa Mwanza.


Mwisho, Nakuhakikishia hadi kesho, ubabe/ujasiri kwa wakurya hautaisha ila tu utabadilika kulingana na mahitaji ya wakati husika.
 
mkuu wamebadilika, mie nimeopoa kurya,, juz kati nlikuwa huko,, nlikula sana nyama,,

kwa kifupi nlichinjiwa ngo'mbe, hahahahah

jaman wanawake wa kurya watam sanaaa

wanajua kulea

hahahaha siku nakula hadi kichuri, na ule uji wao wa kusindika hahaha
Wee utakuwa mkurya Acha kujificha nyuma ya pazia Mkuu
 
Ndiyo yanaongoza kwa kuwa ' Washamba / Mambwigira ' si tu Tanzania bali hata Ulimwenguni kwa ujumla.
Ni kweli maana juzi nmekutana nammja kasababisha ajali alikuwa na tray la mayai, yamevunjika yote afu anatakaa alipwe kibaya Zaid kayakanyaga mwenyew Kwa miguu dhumuni ili alipwe yote, hopeless kabisa hawa jamaa
 
Ni kweli maana juzi nmekutana nammja kasababisha ajali alikuwa na tray la mayai, yamevunjika yote afu anatakaa alipwe kibaya Zaid kayakanyaga mwenyew Kwa miguu dhumuni ili alipwe yote, hopeless kabisa hawa jamaa

Ndiyo wanaokulindia hii nchi yako Wewe. Acha ' uboya ' tafadhali na tena utuheshimu kweli vinginevyo bila Sisi hii nchi Idi Amin Dada angeshaichukua siku nyingi mno na si ajabu pengine sasa Wewe ungekuwa unawafulia tu Waganda ' Chupi ' zao huko Kwao.

Ifike muda Watanzania wote popote pale mlipo muwe na adabu na heshima na Watu wa Mkoa wa Mara ( Musoma ) vinginevyo mtatuudhi halafu ' tutalegeza ' na kuwaachia Warwanda na Wamalawi na hata Wakenya waingie kiurahisi na ' waipige ' Tanzania yenu hii.

Tangia lini nchi ikalindwa na Wahaya, Waha, Warangi, Wanyiramba na Wanyaturu?
 
Ndiyo wanaokulindia hii nchi yako Wewe. Acha ' uboya ' tafadhali na tena utuheshimu kweli vinginevyo bila Sisi hii nchi Idi Amin Dada angeshaichukua siku nyingi mno na si ajabu pengine sasa Wewe ungekuwa unawafulia tu Waganda ' Chupi ' zao huko Kwao.

Ifike muda Watanzania wote popote pale mlipo muwe na adabu na heshima na Watu wa Mkoa wa Mara ( Musoma ) vinginevyo mtatuudhi halafu ' tutalegeza ' na kuwaachia Warwanda na Wamalawi na hata Wakenya waingie kiurahisi na ' waipige ' Tanzania yenu hii.

Tangia lini nchi ikalindwa na Wahaya, Waha, Warangi, Wanyiramba na Wanyaturu?
Kweli nimeamini wewe jamaaa ata kweny post unazoshindiliwa Kwa uongo ni kweli maana huwa unasahau unachokisema na unachokiandika,wewe ni muongo nawatu Hilo tunalijua, kuna post moja watu wanakushambuliaa Kwa sababu ya uongo wako,ukawa mdogo kama chupi ya mtot mdogo tena wakike,kweny post ile ulinijibu wewe sio mkurya,Leo hii umethibitisha wewe ni mkurya,afu huwa unakataaa,Kwanza unapnda kujamu,hasira za kijinga,ujuaji mwingi kumbe mbele Giza,badilika wewe dada
 
Shida yenu ndio hiyo,(kama wewe ni mmoja wao) hamtaki kukosolewa. Ruhusuni mawazo tofauti. Vinginevyo mtaendelea kuonekana vituko.
Uzuri sisi huwa hatufanyi mambo kwa kuogopa mtu au makabila eti yatatuchukuliaje, huwa tunafanya kile tunaona kinatufaa, hatuendeshwi na watu back...! Maana huwa mnajisumbua nyie kuhangaika na sisi ila sie hatuna habari tunafanya yetu....! Kama lugha unayo yako na wewe ongea
 
Kweli nimeamini wewe jamaaa ata kweny post unazoshindiliwa Kwa uongo ni kweli maana huwa unasahau unachokisema na unachokiandika,wewe ni muongo nawatu Hilo tunalijua, kuna post moja watu wanakushambuliaa Kwa sababu ya uongo wako,ukawa mdogo kama chupi ya mtot mdogo tena wakike,kweny post ile ulinijibu wewe sio mkurya,Leo hii umethibitisha wewe ni mkurya,afu huwa unakataaa,Kwanza unapnda kujamu,hasira za kijinga,ujuaji mwingi kumbe mbele Giza,badilika wewe dada

Kumbe shida yako na inaonekana ni ya muda mrefu ni kutaka tu kujua GENTAMYCINE ni Kabila gani? Sikujua kuwa Wewe ni ' Mpumbavu ' wa Kiwango cha Kimataifa hivi. Ni mara ngapi nimeshaweka ufafanuzi wangu humu wa hasa Kabila langu? Ni majuzi tu hapa nimesema wazi wazi kuwa Mimi ni nusu Mtanzania na nusu Mnyarwanda na kwa hapa Tanzania nimechangia makabila mawili la Zanaki na Makua lakini pia huko nchini Rwanda natokea Kabila la Kitutsi. Nadhani kama kuna Member ambaye hana huu ufahamu wa GENTAMYCINE ni Wewe tu peke yako na ningekuona una maana ungekuja tu ' straight ' kuwa Mimi ni Kabila gani kuliko kuzunguka hivi mbali kama Chupi ya Malaya inayoshindikana kuvaliwa.

Kuhusu Mimi kuwa Muongo wala sikatai na sikasiriki kwakuwa Kiutafiti tena kutoka kwa Wanasayansi ' wabobezi ' imegundulika kwamba Watu ambao ni Waongo Waongo pamoja na Matapeli wana uwezo mkubwa sana wa akili ( IQ ) halafu huwa ni ' Wabunifu ' wa mambo mengi na kama wakipata ' Fursa ' katika maeneno yao ya Kiuwezo wanaweza wakafanya makubwa yenye Tija.

Na pengine ni huu huu Uwongo wangu ndiyo unanifanya GENTAMYCINE niwe nafuatiliwa na almost 75% ya Members wengi wa JF kila wanapoingia humu Jamvini ili kutaka tu kujua nimekuja na nini ili waburudike, wacheke, wachangamke na wahabarike pia. Na yawezekana pia ni huu huu Uwongo wangu ndiyo unaonifanya kila siku GENTAMYCINE niweze kupokea ' Notifications ' za ' Followers ' wapya ambapo mpaka sasa ninao 40 na sijui ' Mpumbavu ' Wewe kama unae hata mmoja.

Mwisho baada ya kupitia posts zako dhidi yangu nimegundua ukiachia mbali kuhangaika kujua Kabila langu pia unaonekana una ' Chuki ' ya waziwazi na Mimi halafu pia ' mvuto ' wangu mkubwa humu / hapa JamiiForums unakusumbua sana huku hapo hapo ukiwa umesahau kwamba kuna Watu wamezaliwa na ' Nyota ' zao hapa duniani na kwamba kadri unavyozidi kuwachukia basi ndiyo Kwanza Mwenyezi Mungu anawabariki na kukuacha Wewe na moyo wako mweusi na sura iliyokunjamana hovyo kama ' Tako ' la Kushoto la Kifaru.

Tulia chini isome na uielewe vyema sana maneno yaliyopo katika ' Signature ' yangu ' tukuka ' yanayosema ' Purely Talented, Charismatic Fella, Game Changer and Entertainer ' kisha naamini siku zingine wala hutokuwa unapata taabu na Mimi na kuzidi tu kutuanikia ' Upumbavu ' wako humu Jamvini kwani ' posts ' na ' threads ' zangu nyingi humu huwa zinataambaa na ' biti ' ya maneno ' Kuntu ' yanayopatikana katika hiyo ' Signature ' yangu.

Dozi na Jumapili njema pia.

Nimemaliza.
 
Shida yenu ndio hiyo,(kama wewe ni mmoja wao) hamtaki kukosolewa. Ruhusuni mawazo tofauti. Vinginevyo mtaendelea kuonekana vituko.
Kwani wakurya wanafanya nini cha ajabu kuwa na mijadala yote hii. Suala la ukeketaji ni kama linaenda kuisha kwa sisi wenyeji tunaojua historia yake. Suala la ubabe hizo ni hadithi mapokeo, hakuna watu rahisi kuishi nao kama wakurya usipoingilia mambo yao, kwanza si wachokozi, hawapendi makuu.
 
Kuna ukweli fulani ila kuwaita washamba hujawatendea haki ungewaambia "hawajaelimika"

Karne hii mtu bado anajivunia utemi ni ukuda huo.

Utemi ulikuwa zamani ndio maana Nyerere aliwajaza jeshini.
Naye alijua bila hivyo sijui wangekuwa vipi sahizi, mpaka wanaheshimu jeshi kuliko kazi yeyote
 
Back
Top Bottom