Wakulima na Wafugaji Stadi Waunganishwa na Barabara Kuu Musoma Vijijini

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,903
945

KIJIJI CHA WAKULIMA NA WAFUGAJI STADI CHAUNGANISHWA KWENYE BARABARA KUU

Kijiji cha Kinyang'erere ni moja ya vijiji vinne (4: Bugwema, Kinyang'erere, Masinono, Muhoji) vya Kata ya Bugwema ya Musoma Vijijini.

Vijiji vyote vinne (4) vimo ndani ya Bonde la Bungwema ambalo Serikali imepanga kujenga miundombimu ya kilimo cha umwagiliaji.

TARURA inafanya kazi kubwa na nzuri sana ya kujenga barabara (km 11), yenye madaraja mawili (2), kwenye mito miwili (Sijati & Nyamagusu) kwa ajili ya kukiunganisha Kijiji cha Kinyang'erere kwenye barabara kuu ya Murangi (Musoma Vijijini)-Bugwema-Masinono-Manyamanyama (Bunda)

Mazao makuu yanayolimwa Kijijini Kinyang'erere ni: mpunga, dengu, choroko, mahindi, maharage na alizeti

Mifugo muhimu ya Kijiji hiki ni ng'ombe, kondoo na mbuzi

Barabara hiyo ya kilomita 11 inaunganisha Wilaya za Musoma na Bunda kupitia Kijiji cha mpakani kiitwacho Karukekere (Mwibara, Bunda)

Tafadhali sikiliza CLIP/VIDEO iliyoambatanishwa hapa - shukrani nyingi mno kwa Serikali yetu.

Usisahau kutembelea TOVUTI ya Jimbo letu ambayo ni:
www.musomavijijini.or.tz

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

Tarehe:
Alhamisi, 11.5.2023
 

Attachments

  • WhatsApp Video 2023-05-11 at 18.24.45.mp4
    16.4 MB
mbunge ameshindwa kuitoa lami buhare hata kuifikisha mkirira miaka yote hiyo
 
Back
Top Bottom