Kama ukiwa unaangalia umbali wa mita moja kutoka usawa wa macho yako utaona hili ni jambo jema. Lakini kwa hakika hili ni jambo la hatari na la kulaaniwa kabisa. Tukianza kugawana bucha, tutakuja kugawana maduka, baadaye tutagawana hata visima vya kuchota maji, na mwisho wa siku hata barabara tutatakiwa kutengeneza za waislam na wakristo. Nasikitishwa sana na silence ya serikali juu ya jambo hili.Imetulia hii, tena inafaa mabucha yote yabandike lebo ya aina hii ili kila mtu achague nyama aipendayo vinginevyo tutalishana vubudu tuu, watu miaka yote wananyonga leo wanadai wachinje.
Tunachinja mpaka Mbogo..!
Hakuna haja ya kuwa na hofu.....duniani kote kwenye mchanganyiko wa imani huu ndio utaratibu.......kumbuka suala la kuchinja kiislamu ni la waislamu tu na halihusu imani zingine......mazoea tulokuwa nayo hayakuwa sahihi
Mkuu Safari_ni_Safari hofu yangu kubwa ni jinci issue nzima inavyokuwa handled.. Hilo ndilo linalonikosesha amani sana.. Kama imefikia watanzania kuchinjana ili kuzuia mwingine asichinje.. basi inaonyesha tumekosa mavumiliano na tutapelekwa kwenye next step ambayo nayo haitakuwa ya mwisho.. Tuna ombwe kubwa sana la uongozi wenye busara ambao ungeweza kulitatua hili bila ya damu kumwagika..!
Mkuu sosoliso, nakusihi wala usipeleke mawazo yako mbali. Lione hili kama jambo la kawaida tu. Kwenye baadhi ya nchi kuna maduka ya vyakula ambamo wanauza nyama halal na wanaandika na kunadi hivyo. Wala halionekani jambo la ajabu. Na hili tukilichukulia kama ni jambo la kawaida tu, wala hatutafika kule watu wanakohofia.
Naamini Mungu atasikiliza sala na maombi yetu jambo hili liishe kwa maelewanoMkuu Mpita Njia ingekuwa suala hili watu wazima wamekaa chini na kukubaliana kila dini iwe na machinjio yake wala licingenipa hofu hata kidogo.. Maendeleo yanapatikana kwa njia hiyo ya kujadiliana na kukubaliana bila ya mmoja kukiuka haki ya mwenzie.. Kinachonitatiza mie ni haya mabishano yaliosababisha kifo.. hawa wanadai haki ya kuchinja vitoweo vyao na wengine wanapinga haki ya wenziwao kuchinja vitoweo vyao.. Na kila kundi liko tayari kwa lolote.. iwe mvua iwe jua.. Kwanini..? Watoto wana haki ya kutuuliza wazazi kama sie tulikulia kwenye mazingira haya.. Tutawajibu nini..? Ninashindwa kuwajibu wanangu.. Naomba Mungu utusaidie waja wako..
Hii c dalili nzuri hata kidogo.. Tumeanza na mabucha.. Nini kitakachofuata baadae..? Maana tunashabikia lakini hebu tuangalie huko mbele kwa mwendo huu.. Ninawafikiria wanangu wanaokuwa katika mkanganyiko huu.. Ninawatengenezea mazingira gani ya kuishi kama Watanzania..? Naogopa sana.. Serious..
Hii c dalili nzuri hata kidogo.. Tumeanza na mabucha.. Nini kitakachofuata baadae..? Maana tunashabikia lakini hebu tuangalie huko mbele kwa mwendo huu.. Ninawafikiria wanangu wanaokuwa katika mkanganyiko huu.. Ninawatengenezea mazingira gani ya kuishi kama Watanzania..? Naogopa sana.. Serious..
Mkuu, hii picha imepigwa kutoka upande gani wa nchi hii?
Tiba
Ni kweli mkuu, hili sio suala la kushabikia hata kidogo! Inatakiwa serikali itoe amri kwa wote wanaoweka matangazo kama hayo wayafute kwani yanachochea sana mgawanyiko na yanaweza kusababisha madhara zaidi.