Wakosoaji wa Serikali wanatumwa?

Wakosoaji wa Serikali wanatumwa?

Fact number moja: Serikali haijawahi kupunguza madai ya deni walilowadai barrick/Accacia ...kama una sehemu ya Taarifa ya serikali inayoonesha hilo iweke hapa jamvini.

Kwa kiashiria hiki kidogo tu ni wazi unadhihirisha kuwa umetumwa kulaghai umma kwa manufaa yako na waliokutuma.

Mnatumwa ndio kwa kuwa hamjawahi kuhoji matatizo halisi ya watanzania na mmekua chanzo cha kuanzisha mijadala isiyokuwa na tija kwa maisha ya kila siku ya mtanzania....yaani mnaanzisha mijadala ya kitaifa katika interests za mabepari na wafabyabiashara walioliibia Taifa.

Ulipotaka Rais atangaze njaa ni janga la kitaifa na ukatuaminisha ni janga ulikuwa hujatumwa?
Unajua kwanini umepata likes 2 tu na mtoa mada kapata likes 42?
 
Mkuu mleta thread, je hawa wanatumwa na nani;
wanaoteka na kuumiza wengine
wanaobambikia wengine kesi
wanaotesa watu
wanaonunua madiwani na wabunge
 
Fact number moja: Serikali haijawahi kupunguza madai ya deni walilowadai barrick/Accacia ...kama una sehemu ya Taarifa ya serikali inayoonesha hilo iweke hapa jamvini.

Kwa kiashiria hiki kidogo tu ni wazi unadhihirisha kuwa umetumwa kulaghai umma kwa manufaa yako na waliokutuma.

Mnatumwa ndio kwa kuwa hamjawahi kuhoji matatizo halisi ya watanzania na mmekua chanzo cha kuanzisha mijadala isiyokuwa na tija kwa maisha ya kila siku ya mtanzania....yaani mnaanzisha mijadala ya kitaifa katika interests za mabepari na wafabyabiashara walioliibia Taifa.

Ulipotaka Rais atangaze njaa ni janga la kitaifa na ukatuaminisha ni janga ulikuwa hujatumwa?
Sasa tunahoji zipo wapi Trillion 1.5 ? Zipo wapi zile bilion 252 zilipotea wizara ya ujenzi kwa kuwalipa makandarasi hewa? Zipo wapi bilion 8 za kivuko feki? Mtukufu malaika toka chato na Naibu Rais Maliyamungu Bashite wanachota pesa Hazina ( BOT) kienyeji wanazitumia kununua wabunge na madiwani kurudia chaguzi kwa gharama kubwa, huku akiwabambikia kesi, kuwapiga Risasi, kuwafunga jela Wapinzani na unyama mwingineo mwingi tu.
 
Wakosoaji wa Serikali wanatumwa?

Siku hizi ukisikiliza hotuba za Viongozi Wakuu wa Serikali ya Tanzania pamoja na maandiko ya Vyombo vya Habari vinavyoiunga mkono Serikali kama vile Jamvi la Habari, Habarileo, Uhuru nk utasikia au kusoma madai yanayojirudia rudia kuwa kuna Watanzania wanatumika na mataifa ya Nje kuidhuru nchi yetu. Madai haya yanayotolewa bila ushahidi wowote ni madai yanayoonyesha ni namna gani nchi yetu imeua kabisa utamaduni wa kukosoana.

Wakati wa mjadala wa mabadiliko makubwa ya sekta ya Madini aliyoyafanya Rais Magufuli kufuatia amri yake ya kuzuia kusafirisha makanikia, tuhuma dhidi ya baadhi yetu zilikuwa kubwa mno kiasi cha watu kuonekana wasaliti wa nchi yetu. Katika moja ya hotuba yake, Rais Magufuli alifikia hatua ya kusema kuwa ‘ msaliti dawa yake inajulikana ‘.

Haikuchukua muda Mbunge Tundu Lissu, aliyekuwa mmoja wa wakosoaji wakubwa wa Serikali alipigwa risasi na kukoswakoswa kupoteza maisha. Licha ya matusi yote tuliyotukanwa, madai ya $490bn ambayo Serikali iliyatoa kwa Kampuni ya Barrick yalishuka mpaka $300m ambazo hazijalipwa mpaka sasa na wala hazionekani kwenye vitabu vya Serikali kama Mapato tarajiwa ( receivables). Vijana wanatania mitandaoni kuwa tumetoka ahadi ya Noah kwa kila Mtanzania na kufikia ahadi ya Balimi 7 kwa kila Mtanzania. Hata hizo Balimi hazijapatikana.

Wakati wa mjadala wa Ndege yetu kukamatwa huko Canada, pia zilitengenezwa nadharia kuwa mimi na Tundu Lissu tumelipwa na mabeberu ili kuzuia ndege ile. Kampuni iliyowasilisha amri ya kushikilia ndege ile ililipuliwa na bomu na nchi kuingizwa kwenye taharuki bila sababu. Hatimaye Serikali imelipa zaidi TZS 60 Bilioni ili Ndege iweze kuletwa nchini. Wakosoaji wa Serikali walikosoa namna Serikali inajiendesha kana kwamba Tanzania ni kisiwa na madhara yake ni nchi kupata hasara kubwa Sana. Hivi sasa kuna kesi kadhaa Marekani na Uingereza dhidi ya Serikali yetu kutokana na mikataba mbalimbali ambayo Serikali imeshindwa kuiheshimu au Serikali ilifanya ubabe kuivunja bila kujali sheria za kimataifa. Jumla ya madai tunayodaiwa kwenye mahakama za nje ( ninayoyajua mimi na mengine kuthibitishwa na CAG kwenye Taarifa yake ya mwaka 2016/17 ) yanafika Dola za Kimarekani Bilioni 1.48 Sawa na Shilingi Trilioni 3.3 za Kitanzania [ Madai ya Standard Chartered Bank Hong Kong $614m+$148m, Madai ya Syimbion Power $600m, Madai ya Konoike $63m, Madai ya Airbus $59m ].

Hata sasa kwenye mjadala wa kutoonekana kwa matumizi ya TZS 1.5T Serikali imejaribu kutumia maneno hayo hayo ya kuwaita wakosoaji kuwa wametumwa. Majibu rasmi ya Serikali ndani ya Bunge yamewaita wakosoaji ‘ watu wasioitakia mema nchi yetu ‘. Rais naye alipokuwa anafungua tawi la Benki ya NMB Dodoma akasema ‘ watu wanatumwa na mabeberu ‘. Unachoshangaa ni Kwamba hoja hii ya 1.5T imetoka kwenye Ripoti ya CAG ambayo ndio mamlaka ya kikatiba kufanya Ukaguzi wa Fedha za Serikali. CAG ana mamlaka makubwa kiasi kwamba Rais hana mamlaka ya kumfukuza Kazi hata amchukie namna gani. Iweje utumie Ripoti ya CAG kuihoji Serikali uwe unatumwa na watu wa Nje?

Kwenye mjadala kuhusu zabuni ya pasi za kusafiria pia Gazeti la Jamhuri lilisakamwa na Gazeti la Jamvi kuwa wametumwa na mabeberu. Baadaye naona magazeti haya yalifanya mkataba wa amani ( ceasefire). Hata hivyo gazeti la Jamhuri lilikuwa linafanya Kazi yake ya kuhoji Serikali na kupasha Habari wasomaji wake.

Wakosoaji wa Serikali wanapohoji ni Kwa maslahi ya nchi na sio kwa kutumwa. Dhana kwamba watu wanatumwa ni dhana ambayo haina nguvu na inajaribu kuua Uhuru wa maoni na wajibu wa kukosoa. Kukimbilia kuita watu majina mabaya Kwa sababu ya kuhoji masuala ya Umma tena kwa ushahidi ni dalili za wenye mamlaka kukosa Majibu na hivyo kutumia nguvu dhidi ya wakosoaji. Nadharia kuwa ukosoaji ni kutumwa unaenda kinyume na Mwongozo wa CCM wa mwaka 1981 ambao ulijikita kwenye ‘ kukosoa na kujikosoa ‘ ili kujenga Taifa imara.

Marehemu Mzee Kingunge Ngombale Mwiru amenukuliwa na wanazuoni akieleza kuhusu Mwongozo wa CCM wa mwaka 1981 “ Wakati Mwongozo wa TANU wa 1971 ulijielekeza kwenye mapambano dhidi ya Ukoloni, Ukoloni-Mamboleo na Ubeberu ili kufanikisha Ukombozi wa Afrika na wa Mwafrika na kuweka mkakati wa ulinzi na usalama wa umma ili nchi iwe na uwezo wa kukabiliana na uvamizi wowote kutoka kwa ubeberu au na vibaraka vyake, Mwongozo wa 1981 umejikita katika kufanya uchambuzi kosoa wa kina na mpana juu ya hali ya kisiasa na kiuchumi iliyokuwepo nchini, hali ya maendeleo ya demokrasia nchini na ndani ya chama, n.k., na kutoa mapendekezo ya kuimarisha na kupanua demokrasia katika Chama na nchi”. Mwisho wa kunukuu. Inashangaza kuwa wana CCM wanaotawala sasa wanatafsiri ukosoaji kuwa ni uadui na kwenda kinyume kabisa na misingi ya Chama chao.

Kwa upande wa Chama ambacho mimi ni Kiongozi wake, Msingi wa kwanza Katika misingi kumi ni UZALENDO. Msingi huu unasema, nanukuu “ Uzalendo ndio moyo wa kuanzishwa kwa chama cha Wazalendo ikiwa ni tamko letu rasmi la kuipenda nchi yetu na utayari wa kuipigania na kuilinda. Ubora na umakini wa maamuzi yetu kama chama utapimwa kwa kuangalia ni namna gani maamuzi hayo yana faida kwa taifa letu na wananchi wake kwa leo na kesho”. Hivi sisi ACT Wazalendo kama Chama hufanya ukosoaji kwa kuzingatia maslahi ya Nchi yetu. Kila jambo tunalipima kwa kuangalia nchi inapata faida gani. Tulipoamua kukosoa takwimu za Serikali kuhusu GDP ( Pato la Taifa ) tulijua iwapo Serikali itaendelea na sera fyongo za Uchumi, Wananchi wataumia na nchi itaumia. Tangu tumetoa Tamko lile la Kamati Kuu Serikali imelegeza udhibiti wa ujazo wa Fedha kwenye Uchumi na ukuaji wake umefikia 8% kwa mujibu wa Taarifa za hivi karibuni za Benki Kuu.

Tulipoamua kuzungumzia soko la bidhaa za mbaazi, choroko nk sio kuwa tunainanga Serikali bali tunataka Serikali itimize wajibu wake Kwa raia kufuatia kuanguka kwa soko la mbaazi lenye thamani ya $250m ( zaidi TZS 500 Bilioni) kwa mwaka.

Tulipoamua kuchambua Taarifa ya CAG ya mwaka 2016/17 na uchambuzi uliofutia wa majibu ya Serikali kwa Hoja hiyo ya Ukaguzi lengo letu ni kuisimamia Serikali ambayo ndio wajibu wa Wabunge na Vyama vya siasa visivyo madarakani. Hatukutumwa bali tulijituma na kujiongeza kuonyesha kuwa Fedha za Umma hazisimamiwi vizuri na Serikali ya awamu ya 5 iliyo chini ya CCM.

Wakosoaji wa Serikali wanatimiza wajibu wao kama Wananchi. Hawatumwi na mabeberu. Kwa mujibu wa Sheria za nchi yetu kutumwa na mabeberu kuchafua sura ya nchi ni uasi na adhabu yake ni kifo. Serikali badala ya kulalamika tu kwenye mikutano Kuwa wakosoaji wake wanatumwa, ichukue hatua za kisheria kuwashtaki hao wanaodhaniwa kutumwa ili wakosoaji wa kweli waendelee na wajibu wao. Tuhuma za kutumwa hakiwezi kuwa kichaka cha kujifichia na kukwepa kujibu Hoja za Msingi.

Wananchi sasa waanze kukataa nadharia za kitoto, zilizopitwa na wakati Kuwa wakosoaji wa Serikali wametumwa. Wananchi wahoji ushahidi wa madai hayo. Wasikubali tuhuma hewa zinazotolewa ili kuficha ukweli wa masuala yanayoibuliwa. Serikali ina Vyombo vyenye uwezo mkubwa wa kuchunguza, Wananchi watake ushahidi kutoka vyombo Hivi. Propaganda za ‘ wanatumiwa ‘ zikiachwa tu watu wataumia. Tutajenga Taifa la hovyo, la watu wasiohoji, wanaodanganywa tu.

Kwa mwananchi, hakuna uzalendo bora zaidi kuliko uzalendo wa kuikosoa Serikali ya nchi yako. Uzalendo mkubwa zaidi ni kuitetea nchi yako, si Serikali! NCHI yako.

Kukosoa Sio shida.Shida huwa lugha. Muda,Mahali na Malengo ya mkosoaji . Anayekosoa kwa dhati husifia pia. So kabla hujamaliza gazeti lako. Tafakari hayo Mambo.Kuhusu Lissu waza Motive ni nini. Kuna jambo gani. Je katika kuwaza tu Motive gani ina mashiko. Dalili ya kutaka kuchukua nafasi ya kugombea urais Katika chama chako Au kuzima kelele tu za hadharani.
 
Fact number moja: Serikali haijawahi kupunguza madai ya deni walilowadai barrick/Accacia ...kama una sehemu ya Taarifa ya serikali inayoonesha hilo iweke hapa jamvini.

Kwa kiashiria hiki kidogo tu ni wazi unadhihirisha kuwa umetumwa kulaghai umma kwa manufaa yako na waliokutuma.

Mnatumwa ndio kwa kuwa hamjawahi kuhoji matatizo halisi ya watanzania na mmekua chanzo cha kuanzisha mijadala isiyokuwa na tija kwa maisha ya kila siku ya mtanzania....yaani mnaanzisha mijadala ya kitaifa katika interests za mabepari na wafabyabiashara walioliibia Taifa.

Ulipotaka Rais atangaze njaa ni janga la kitaifa na ukatuaminisha ni janga ulikuwa hujatumwa?
Hapo alijituma mwenyewe tu kama na wewe ulivyojituma kuandika haya iliyoandika. Au na wewe umetumwa?
 
Mh. hoja zako ni za msingi sana kwa ustawi wa Taifa. Ila Watanzania walio wengi wana tatizo la uelewa. Sijui kama watakuwa wamekuelewa. Naona wengine wanatoa mapovu humu yasiyo endana kabisa na hoja zako, wengine bado wanadhani unapinga jitihada za serikali za kuleta maendeleo na wengine bado wanadhani unatumwa na mabeberu…..IQ za wabongo ni shida
Tenda ya kuwatetea CCM mitandaoni ilichukuliwa na Le mutuz, Cyprian msiba na Jerry muro watu ambao ni wajinga wajinga sana tena sana na sasa zaidi unategemea nini? Wameajiri vijana Wajinga wajinga vilaza kama wao ndiyo wanawatumia kusumbua watu wanaoikosoa serikali ya wakoloni wa kisukuma mitandaoni.
 
Wewe ndiye huna akili na hujui taifa linatoka wapi na kwenda wapi. Wewe kichwani umejaza minyoo ndiyo maana huna ubongo, hujui nchi hii ilitaka kuwa mikononi mwa wachache, wewe ni hohehahe kwa sababu hujui zito alishazoea kuleta taharuki ili baadaye aombe rushwa ( yaani anaanzisha tuhuma hasa hizi za kutetea wazungu, then wanampatia hela), sehemu kubwa ya mali za zito ni za rushwa
Hiki si kigezo cha kuacha kuikosoa serikali ya kidhalimu, acha kuishi kwa kukariri Propaganda za CCM za huko nyuma, sasa tunaangalia yanayoendelea sasa kwani hata history ya Mtukufu huko nyuma ni mbaya kuliko Mtanzania yeyote.
 
Duh...Kweli shughuli ipo, ni madai mazito sana sana, yanatutisha raia...sijuwi watayajibu haya?!
Yote yanahitaji maelezo...
Nashangaa wanaotetea serikali yetu hawataki kujibu haya ya Mh. Zitto hata moja?! Sana sana wamebakia kujibu povu tu, tunawaomba wajibu tuhuma moja baada ya nyingine humu kama ifuatavyo, na siyo kukashifu, wakae kwenye hoja, wachambuwe kama kina @kafulila au Kitila Mkumbo, moja baada ya nyingine..

  • ...madai ya $490bn ambayo Serikali iliyatoa kwa Kampuni ya Barrick yalishuka mpaka $300m ambazo hazijalipwa mpaka sasa na wala hazionekani kwenye vitabu vya Serikali kama Mapato tarajiwa ( receivables). Vijana wanatania mitandaoni kuwa tumetoka ahadi ya Noah kwa kila Mtanzania na kufikia ahadi ya Balimi 7 kwa kila Mtanzania. Hata hizo Balimi hazijapatikana.
  • Hatimaye Serikali imelipa zaidi TZS 60 Bilioni ili Ndege iweze kuletwa nchini.
  • Jumla ya madai tunayodaiwa kwenye mahakama za nje ( ninayoyajua mimi na mengine kuthibitishwa na CAG kwenye Taarifa yake ya mwaka 2016/17 ) yanafika Dola za Kimarekani Bilioni 1.48 Sawa na Shilingi Trilioni 3.3 za Kitanzania [ Madai ya Standard Chartered Bank Hong Kong $614m+$148m, Madai ya Syimbion Power $600m, Madai ya Konoike $63m, Madai ya Airbus $59m ].
  • ..kutoonekana kwa matumizi ya TZS 1.5T Serikali imejaribu kutumia maneno hayo hayo ya kuwaita wakosoaji kuwa wametumwa.
  • Tulipoamua kuzungumzia soko la bidhaa za mbaazi, choroko nk sio kuwa tunainanga Serikali bali tunataka Serikali itimize wajibu wake Kwa raia kufuatia kuanguka kwa soko la mbaazi lenye thamani ya $250m ( zaidi TZS 500 Bilioni) kwa mwaka.
 
Zitto hiyo ni mbinu mbadala wanayootumia ccm kujilinda.
Sasa kwakua ishakua hivyo, fikirieni jinsi gani mnaisambaratisha.

Upinzani msipo kuwa ngangari 2020 habaki mtu mle ndani
 
Rais kuna mda anajibebesha zigo la misumali yeye mwenyewe alafu anaanza kulalamikia wengine. Swala la hizo trillions 1.5 yeye anazungumza maneno anaacha kutizama kilichomo ndani ya maandishi, hapo wangeeleza tu km hazijaibwa zimetumika ktk matumizi gani?...
Swala la kusema wametumwa tena jukwaani mm naona ni kujishushia hadhi tu, inatakiwa atoe majibu yale majibu ya kusema hazijaibwa...hayatoshi wamalizie majibu zimetumika wapi?. hata kama zmetumika ni kinyume na taratibu hivyo serikali inapaswa kushauriwa ili isirudie kosa la kufanya matumizi pasipo kufuata taratibu. Ngosha atusaidie wananchi kuelewa km kweli hazijaibwa hizo pesa, swala la nyie kutumwa aeleze baada ya kujibu kwa usahihi tuhuma anazoelekezwa!
 
Duh...Kweli shughuli ipo, ni madai mazito sana sana, yanatutisha raia...sijuwi watayajibu haya?!
Yote yanahitaji maelezo...

  • ...madai ya $490bn ambayo Serikali iliyatoa kwa Kampuni ya Barrick yalishuka mpaka $300m ambazo hazijalipwa mpaka sasa na wala hazionekani kwenye vitabu vya Serikali kama Mapato tarajiwa ( receivables). Vijana wanatania mitandaoni kuwa tumetoka ahadi ya Noah kwa kila Mtanzania na kufikia ahadi ya Balimi 7 kwa kila Mtanzania. Hata hizo Balimi hazijapatikana.
  • Hatimaye Serikali imelipa zaidi TZS 60 Bilioni ili Ndege iweze kuletwa nchini.
  • Jumla ya madai tunayodaiwa kwenye mahakama za nje ( ninayoyajua mimi na mengine kuthibitishwa na CAG kwenye Taarifa yake ya mwaka 2016/17 ) yanafika Dola za Kimarekani Bilioni 1.48 Sawa na Shilingi Trilioni 3.3 za Kitanzania [ Madai ya Standard Chartered Bank Hong Kong $614m+$148m, Madai ya Syimbion Power $600m, Madai ya Konoike $63m, Madai ya Airbus $59m ].
  • ..kutoonekana kwa matumizi ya TZS 1.5T Serikali imejaribu kutumia maneno hayo hayo ya kuwaita wakosoaji kuwa wametumwa.
  • Tulipoamua kuzungumzia soko la bidhaa za mbaazi, choroko nk sio kuwa tunainanga Serikali bali tunataka Serikali itimize wajibu wake Kwa raia kufuatia kuanguka kwa soko la mbaazi lenye thamani ya $250m ( zaidi TZS 500 Bilioni) kwa mwaka.
Makinikia yanakwenda nje kiimya kiimya na pesa inapigwa kiimya kiimya, madini na pesa zote walizokamata mipakani na Airport anajimilikisha yeye binafsi zingine anagawana kiimya kiimya na Naibu Rais Maliyamungu Bashite, Ukisikia wamekamata kitu cha thamani jua moja kwa moja hicho kinakuwa Mali yao binafsi , wasukuma wawili washamba wao wameamua kuchukua pesa zao mapema hawataki kuiba mwisho mwisho kama kikwete na mkapa, wanapiga pesa mapema kisha baadae wawafunge jela watu wengi sana kwa kesi za Ufisadi wakiamini watanzania ni wepesi wa kusahau ya nyuma na kushabikia yaliyopo kipindi hicho hicho.
 
Rais kuna mda anajibebesha zigo la misumali yeye mwenyewe alafu anaanza kulalamikia wengine. Swala la hizo trillions 1.5 yeye anazungumza maneno anaacha kutizama kilichomo ndani ya maandishi, hapo wangeeleza tu km hazijaibwa zimetumika ktk matumizi gani?...
Swala la kusema wametumwa tena jukwaani mm naona ni kujishushia hadhi tu, inatakiwa atoe majibu yale majibu ya kusema hazijaibwa...hayatoshi wamalizie majibu zimetumika wapi?. hata kama zmetumika ni kinyume na taratibu hivyo serikali inapaswa kushauriwa ili isirudie kosa la kufanya matumizi pasipo kufuata taratibu. Ngosha atusaidie wananchi kuelewa km kweli hazijaibwa hizo pesa, swala la nyie kutumwa aeleze baada ya kujibu kwa usahihi tuhuma anazoelekezwa!
Trillion 1.5 chenji yake ipo tumboni na mifukoni mwa Mtukufu malaika toka chato na Naibu Rais Maliyamungu Bashite, baada ya kuzitumia kuwanunua wabunge, madiwani, kurudia chaguzi kwa gharama kubwa, uchakachuaji, kuwabambikia kesi, kuwapiga Risasi, kuwafunga jela Wapinzani, kujenga Chato Airport, kukomboa ndege na kununua ndege kwa cash kienyeji, pesa nyingi imepotelea hapo na bado wanaendelea kuchukua pesa Bank kuu kienyeji.
 
Ukiona mtu kila siku yeye ni kukosoa tu ujue huyo ni adui wa maendeleo.

Wapinzani wanatakiwa kuwa washirika wa maendeleo sio maadui. Hawatakiwa kukosoa tu kila kitu. Wanatakiwa kukosoa kwa malengo ya kuboresha.

sasa kama anakosoa akiwa na hoja ambazo hazipewi majibu kwanini umhukumu kama mpinzani wa maendeleo. unatakiwa kumpa majibu. mpe majibu ili uma wote ujue kuwa ni mpinzani hewa. mmekalia kusema tu kuwa wapinzani wanapinga kila kitu. hoja za kitoto kabisa kama huna majibu kwa hoja zao. wape majibu. kwa taarifu huyo ni mkereketwa wa maendeleo kwa sababu ana uthubutu wa kusema pale mambo yanapoharibiwa na kuligharimu taifa. tatizo la watu wa aina yako ni upofu wa kuabudu rangi ya nguo badala kutanguliza maslahi ya taifa kwanza. wapinzani ni washirika wa maendeleo ya taifa kwa kuleta hoja mbadala ambazo kwa kweli ndizo zinazofanya kazi kuliko hizo zingine. hawakosoi kila kitu na wanachofanya ni kukusoa ili kuboresha
 
Habari wanajamvi

Mh. Zito Zuberi Ruyangwa Kabwe ni mwanasiasa ambaye hafanyi siasa tu, ni mwanasiasa ambaye anafanya siasa za kisomi ambazo anatumia muda mwingi kukusanya facts na pindi anapozitoa facts hizo huleta taharuki katika jamii, Pongezi hizi za Mhe Zito hakuna mwenye uwezo wa kuzichukua wala kumpoka. Mhe Zito ni strategist mzuri sana uthibitisho wa hili ni pale alipofukuzwa CHADEMA na kuanzisha ACT WAZALENDO akajitupa kwenye ubunge na akaupata ikiwa ni utofauti wa miaka miwili tu kabla ya uchaguzi mkuu.

Jambo ambalo watu wengi au wanasiasa wengi wanapata taabu na Mhe. Zito, kwakua ni mtu anayetumia muna mwingi kujipanga hata akija na uongo (sio mara zote) ni vigumu sana kupata hoja ya kupinga hoja yake papo kwa hapo. Mhe. Zito anatakiwa apate mtu ambaye anaweza kum PRE-EMPTY kwakua ukichelewa akatoka yeye kwanza, utahitaji muda uleule aliotumia ili kuweza kumkabili.

Nawasilisha
 
sasa kama anakosoa akiwa na hoja ambazo hazipewi majibu kwanini umhukumu kama mpinzani wa maendeleo. unatakiwa kumpa majibu. mpe majibu ili uma wote ujue kuwa ni mpinzani hewa. mmekalia kusema tu kuwa wapinzani wanapinga kila kitu. hoja za kitoto kabisa kama huna majibu kwa hoja zao. wape majibu. kwa taarifu huyo ni mkereketwa wa maendeleo kwa sababu ana uthubutu wa kusema pale mambo yanapoharibiwa na kuligharimu taifa. tatizo la watu wa aina yako ni upofu wa kuabudu rangi ya nguo badala kutanguliza maslahi ya taifa kwanza. wapinzani ni washirika wa maendeleo ya taifa kwa kuleta hoja mbadala ambazo kwa kweli ndizo zinazofanya kazi kuliko hizo zingine. hawakosoi kila kitu na wanachofanya ni kukusoa ili kuboresha
Halafu cha kushangaza wanafikiri kila anayetaka majibu ni mkinzani au mpinzani?! Wao wajibu tuhuma moja baada ya moja, Mh. Zitto kaja na maswali yake, wao wajibu hivyo hivyo kwa kupanguwa yote..
Sasa wamekalia kukashifu na kutoa mapovu, wangejuwa tu wengine sie siyo wapinzani, ni raia tusio na vyama, ni raia wa kawaida tusiotaka kuambiwa kila kinachokosolewa ni kutaka kuvuruga amani..Inatutia wasiwasi sana kwa kweli....
 
Trillion 1.5 chenji yake ipo tumboni na mifukoni mwa Mtukufu malaika toka chato na Naibu Rais Maliyamungu Bashite, baada ya kuzitumia kuwanunua wabunge, madiwani, kurudia chaguzi kwa gharama kubwa, uchakachuaji, kuwabambikia kesi, kuwapiga Risasi, kuwafunga jela Wapinzani, kujenga Chato Airport, kukomboa ndege na kununua ndege kwa cash kienyeji, pesa nyingi imepotelea hapo na bado wanaendelea kuchukua pesa Bank kuu kienyeji.
nadhani alitaka kuzima nguvu ya mahakama, nguvu ya bunge. Ili abaki yeye serikali peke yake na ndio maana akawa anafanya vurugu kila upande...nadhani kadri siku zinavyosogea anajifunza taratibu itafika siku ataelewa na atajutia mambo aliyokuwa anayafanya pasipo kufuata utaratibu na kuheshimu mihimili mingine
 
Kinachosikitisha hata watu na elimu zao PhD wanaweza chukua vyeti wakajaza lori wao nao wanakuja na kusema mmetumwa na mabeberu, hahaha! wasomi wa bongo wanachekesha sana. Wakishindwa kuargue kwa hoja wanatafuta cha kusema ambacho kitawapa support ya majority na wote tunajua majority Tanzania ni watu wasio na elimu, ukisema chochote ukamalizia na sentensi "nimejitoa kwa ajili ya watanzania, mungu nisaidie" basi wajinga wote watakuunga mkono. Only that simple sentence hata kama umetoa order uue kijiji kizima utapata wajinga watakuunga mkono.
 
Naona Zitto unasema ni bora mshitakiwe. Shida ni kuwa mkishtakiwa mtasema serikali inakandamiza uhuru wenu wa maoni. Mkipatikana na makosa mahakamani mkatakiwa kufungwa/ kulipa faini mtasema maagizo kutoka juu. Haieleweki mnataka nini..
 
Fact number moja: Serikali haijawahi kupunguza madai ya deni walilowadai barrick/Accacia ...kama una sehemu ya Taarifa ya serikali inayoonesha hilo iweke hapa jamvini.

Kwa kiashiria hiki kidogo tu ni wazi unadhihirisha kuwa umetumwa kulaghai umma kwa manufaa yako na waliokutuma.

Mnatumwa ndio kwa kuwa hamjawahi kuhoji matatizo halisi ya watanzania na mmekua chanzo cha kuanzisha mijadala isiyokuwa na tija kwa maisha ya kila siku ya mtanzania....yaani mnaanzisha mijadala ya kitaifa katika interests za mabepari na wafabyabiashara walioliibia Taifa.

Ulipotaka Rais atangaze njaa ni janga la kitaifa na ukatuaminisha ni janga ulikuwa hujatumwa?

Tena?
wewe je umetumwa na nani?
 
Back
Top Bottom