Wako wapi watu wako mliosoma wote

Wako wapi watu wako mliosoma wote

Mwanang side toka 2002 hadi leo japokua maisha yametutenga baada ya yye kuoa,John mjumbe toka 2008,mwanang wa chuo basilio! Life goes on …kifo kikiwa mbele yetu.
 
Aisee mmoja alikuwa ndezi saizi ni captain jwtz alikuwa anaitwa Mangulu yeye tumemaliza six Kaunga jeshi support ya familia ya kutosha saizi anakula mema ya inchi.......

Maisha ni fumbo bila support kutoboa sio rahisi
Mkuu huyo unasema alikua ndezi miaka ya mbeleni usichangae ukimuona akiwa Mkuu wa Majeshi au ofisa mkubwa wa ngazi za juu, Jeshini ukiingia na Elimu ya chini ni rahisi kupanda vyeo mpaka ngazi za juu, ni tofauti na yule anayeingia jeshini tayari akiwa na Elimu ya chuo kikuu, mtu kama huyu aliyeingia na Elimu ya juu anakua alijui jeshi vizuri tofauti na yule aliye ingia na Elimu ya kati anakua ameanzia chini.
 
-Aah nawaogopa Kwa sasa, Kwa sababu wengi wao nilikuwa nawadharau kipindi Niko primary kutokana na wao kufanya vibaya Mimi kufanya vizuri (kuwazidi shule) kimsingi nilikuwa nakuwa 1-3 hapo
-wengi wao sasa ni maaskari, police,jw, prison, immigration,tgs,tanapa, raia maafisa kwenye utumishi wa umma
-hata nikiwa na shida ya hela huwa siwapigi mizinga
 
Facing the future... Safari ya mtoto ndio imeanza wakati ya mzazi pengine ndio imefika.. Huyu anaenda kukutana na mengi tuliyojadili hapa
1749910647556.jpg
 
Eeeh bahn rafiki wa primary tulikuwa close yaan bandika bandua lakini alikuwa na umimi mwingi sikuwezana naye,

Tukatoka hapo nikaenda ordinary level nikapatana na mshkj mmoja then tukawa na crew ya watu kama kumi,

Mshkj wangu huyo hatukuweza kubond tukashindwana though baada ya kufika fom three alitaka tuendeleze urafiki lakini hapo katikati alikuwa akitembelewa na wazazi wake au his sis, lazima aniite sjui kwann, Ila hatukuwa na ugomvi Ila ni ile tuu me kipindi nilikuwa sipend mambo mengi hivyo naona jau,

Mshikaji tumekuja kuonana chuo from o level, tukawa tupo kiaina tuu tukapotezana Juzi nimekutana nae kwenye magenge ya kunywa supu hapo,

Sasa baada ya huyu kushindwana kama nilivyo sema nilikuwa na jamaangu mwingine Ila hatukuwa na bond kiivyo so tukaanza urafiki,

Katika ile crew nilikuwa nawafundisha, ko kila mtu anataka uwe rafiki ake wanafikia hatua wanapigana ili wakae na mm wakati wa kusoma 😂 utoto Raha sana, basi jamaangu huyu wa pili tuka bond ile crew nayo ikapoteza nguvu

sasa mshkj akienda kwao anasema nna jamaangu hv na hv mamake kaja visiting khee, anataka anione basi ndo urafiki na kuwa sehemu ya familia yao ukaanza

Tukaenda tumeua fom four fresh, picha linakuja Advance kila mtu shule yake me mwanza yeye Dom, basi tukawa tunawasiliana fresh kabisa six tukafuta,

Nakumbuka Arusha nna ndugu kibao Ila nilikuwa sifikii kwa aunt upande wa baba, sio kwa broh wala wajomba wala mama makubwa ni kwa jamaa angu, nimetoka JKT nikapita kwao, nikakaribishwa vzr kabisa,

Baada ya hapo nikasepa kuja Dsm, toka kipindi hiko hatujawah kuonana Tena, zaidi ya simu na WhatsApp

sasa ikafika mwaka jana ukimchek yupo busy, mara hv busy, atapatikana mara chache,

sasa mwezi wa tano Juzi nikamcheki hakupokea simu second time kumcheki akapokea direct proportion nikamuuliza tuna ugomvi? Tuna shida gani mzee ? Mbona simu zangu hushiki ? Basi akaeleza situation nzima ilivyo kuwa me nikamwambia fresh Babu nimekusoma ,

Hata saa hzi muda sii mrefu naona katuma text WhatsApp hapo,

Ila advance sikuwa na rafiki at all, ni ile tuu mmekutana disc au mpo table moja ya chakula basi,

chuo napo aaaah sikutaka mambo mengi nikaona nifokasi na mambo yangu, wana labda disc, au wale tuu mnaenda club lkn sio mtu wa kusema huyu naongea nae jambo serious,

Tunapoelekea kwa ambao hatujaoa rafiki wa kweli, washkj wa kweli naona ni familia unayoenda kuiunda,

Nakumbuka mzee alinambia kadri mnavyokuwa hata ninyi ndg wa kuzaliwa kila mtu atashika njia yake, kila mtu ata focus na mambo yake, hamtakuwa na muda wa kuwa pamoja kama mLivyokuwa watoto,

Pambana hakikisha una kazi, oa, usiishi ukisema unamtegemea ndugu yako, akipata tuu familia yake basi hao ndo atakaowaangalia zaidi,

Jumamosi tulivu kabisa kutoka Kigamboni Dsm,

cc secretarybird Hovering Dr am 4 real PhD
Nimetoka muda si mrefu hapo. Kigamboni upepo wa bahari unawapa raha sana. Mwigulu awaangalie nanyi muongezewe kodi.😂😂 Joke.

Niliambiwa marafiki utakaanza nao chuo ndio hao utamaliza nao. Hilo nimeprove.

Familia Yako kwa maana ya mke na watoto ndio watu wako muhimu zaidi.
Ni sahihi kabisa.

Wazazi wako ndio wanaokupenda kutoka moyoni na kamwe hawawezi kukuombea mabaya. Hili dhahiri.

Wakati wa dhiki ndio muda rafiki anapatikana. Sio wadau. Wadau ni muda wa maslahi.

Kuna watu Mungu anaweza pia waleta kwasababu maalum. Aidha washike mkono, wakushike mkono au mshikane mikono mvuke salama.

Shukrani kaka Monetary doctor
Nipe code, Kigamboni safi sana.
 
Nimetoka muda si mrefu hapo. Kigamboni upepo wa bahari unawapa raha sana. Mwigulu awaangalie nanyi muongezewe kodi.😂😂 Joke.

Niliambiwa marafiki utakaanza nao chuo ndio hao utamaliza nao. Hilo nimeprove.

Familia Yako kwa maana ya mke na watoto ndio watu wako muhimu zaidi.
Ni sahihi kabisa.

Wazazi wako ndio wanaokupenda kutoka moyoni na kamwe hawawezi kukuombea mabaya. Hili dhahiri.

Wakati wa dhiki ndio muda rafiki anapatikana. Sio wadau. Wadau ni muda wa maslahi.

Kuna watu Mungu anaweza pia waleta kwasababu maalum. Aidha washike mkono, wakushike mkono au mshikane mikono mvuke salama.

Shukrani kaka Monetary doctor
Nipe code, Kigamboni safi sana.
Naam ujumbe mzurii sana bruh,,

Kigamboni kupo poa na kutulivu kiasi upepo ndo mkali kidogo...
 
Back
Top Bottom