Wakenya, Waganda na Warundi Serikalini

Wakenya, Waganda na Warundi Serikalini

WAKUU, katika utafiti wangu nimegundua kuna raia wa kenya wengi sana wameajiriwa katika public service, waganda pia wapo wengi, warundi na wanyarwanda wapo wengi sana. binafsi kufanya kazi katika private sector najua kuna sheria inayowaruhusu kama wakitimiza vigezo, lakini imefika kipindi wanaajiriwa serikalini wakiwa wamefoji vyeti vya kuzaliwa na passport na kujifanya watanzania. usalama wa nchi upo wapi hapo? mtu akifanya kazi serikalini na yeye sio mtanzania anaweza kupeleka siri zote nchini kwake, na akibadilisha vyeti, ndi kabisaa, watoto wake watahesabika watanzania hata bila kuwa naturalized, naiomba serikali ifanye hivi:

  1. serikali ikague vyeti vyote vya wafanyakazi serikalini, kuanzia vyeti vya kuzaliwa, vyeti vya shule na vyuo, passport etc na wafanye check up na RITA, uhamiaji na shule wanazosema wamesoma etc.
  2. wananchi wa Tanzania watoe siri, ukiona unamtilia shaka raia yeyote anayefanya kazi kwenye public sector, peleka siri hiyo uhamiaji ili uahmiaji waje wamkague kujiridhisha.
  3. wengine wengi ni wanawake walioolewa na watz lakini bado hawajachukua uraia.
hapa juzi, Arusha walionekana wakenya na waganda wakiandikisha watoto wao kwenye vizazi na vifo.

kuna wafanyakazi wengi tu mimi nimeshawaripoti, wengine wanafanya kazi sector muhimu kabisa za serikali, wamefoji vyeti vya kuzaliwa, passport, na vya shule ili waonekane walizaliwa hapa na kusoma hapa, lakini nyuma ya pazia wana vyeti na pass za nchi zao. ni lazima tushirikiane kufichua suala hili.

nchi inayokaa na wageni wa namna hii ni hatari sana kwa usalama wa nchi, no wonder hata kagame alikuwa na guts za kututishia kuwa atatupiga, kwasababu kuna wanyarwanda wengi wanaojifanya watanzania na wengine hata ukiwaangalia kwa sura tu hauulizi mara mbili. siwabagui lakini usalama wa nchi kwanza, uafrica mashariki baadaye. mtaniwia radhi. wakenya ndio wengi sana, mrundi mmuja nakumbuka alikamatwa anafanya kazi tume ya sayansi na technolojia, mwignine alikamatwa mkenya akifanya kazi tanzania investment centre, mwingine alikamatwa mganda akifanya kazi uhamiaji, kuna wengi sana hawajakamatwa lakini usalama wa taifa sijajua kama wamefanya shughuli yao vya kutosha. MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Mi nakupongeza. Achana na hao watu ambao badala ya kujadili wao wanaona eti ni chuki. Chuki ya nini? Kenya hata kama m-TZ ataajniliwa kwa kazi ya kimataifa, bado wanaona ni tatizo kwao utadhani ni ajira ya serikali yao.
Binafsi naomba wa-TZ wote kama kuna mtu unamfahamu, peleka jina uhamiaji na ofisi ya katibu mkuu kiongozi maana uhamiaji walishaharibikiwa kwa miaka zaidi ya 10. wao wenyewe watu wa uhamiaji walikuwa wakiwasaidia wageni kuwa raia kwa njia za mkato.
 
Mi nikiangalia baadhi ya kauli za viongozi hawa nadhani sio raia wa tz
1. Hata watz wale nyasi lazima ndege inunuliwe-Mkenya
2. Watz wapigwe tu na akaruhusu polisi kujichukulia sharia mkononi-Mzambia
3. Tumbukiza kwenye kisima hao-Mnyawanda
4. Ningekuwa mimi ningewapoteza kabisa waliokuwa wanaimba-Mnyawanda
5.
6.
7.
8.
 
Shida ya waTz wengi ni chuki na wivu, kulaumu majirani wenu kwa masaibu yenu
So what? Kwani alichoandika analaumu jirani zetu? Anaeleza hali ilivyo nchini. Au wewe unafurahia tunyamaze? Wao kule Kenya na Rwanda na burundi , nk. wanaweza kunyamaza?
 
Acha kulalamika humu JF, peleka majina hayo kwenye vyombo vya dola. Peleka TISS. Kila wilaya ina ofisi za TISS. Peleka majina hayo kwa DSO au hata RSO yaani yule wa mkoa. Uwe na ushahidi usipeleke majungu. Ukifanya hivyo hoja yako itafanyiwa kazi, tena mara moja.
Tulia wewe, Kwani kazi ya TISS ni nini hadhi tupeleke majina? haya hao Tiss wameisha kamata watu wangapi kama sio wa5 au 6 tu!. Ni kweli hawa watu wapo wengi sana na Wananchi ndio tunafanya Kazi ya Kuwaficha!
 
Mkuu kuna wakati kulitokea wimbi la kupeleka watoto wetu kusoma huko Kenya na Uganda! Wengine walikuwa wakienda huko kuanza chekechea. Hapo pia kuna tatizo. Ukimuuliza mtoto atamtaja mwalimu mkuu wa shule ya Uganda ama Kenya utamwambia si raia.

Mkuu nakubaliana nawe, ndiyo maana nasema wakuhojiwa ni wazazi wao, hao ndiyo wachukuliwe jukumu la kuthibitisha uraia wao, waseme kijiji walicho zaliwa, majirani wao walikuwa ni akina nani,Walimu Wakuu wa Shule za msingi walikuwa wakina nani, kinacho takiwa ni kuhakiki Uraia bila ya kujali vizazi vilivyopita. Watoto wote walio soma chekechea nchi za nje wanajua origin za Ma Baba zao - sasa Baba zao ndiyo wa kufatiliwa.
 
warundi na wanyarwanda ni wenzetu tuu kumbukeni kabla ya WW2 tulikua nchi moja ya Deutche Ostafrica kama koloni la mjerumani, ni baadae ndo tuligawanywa..kwahio unaposema kuna wanyarwanda/warundi serikalini hio sio kweli ni watanzania wenzetu ila wamefanana tu na hao watu wa huko baada ya huo mgawanyo.Na wengi wao lugha yao ni Kiswahili na hawajui Kinyarwanda au Kirundi mababu wa mababu zao wote walizaliwa Tanganyika na generations over generations wako side ya Tz..tusibague watu kwa kuona au kusikia , ubaguzi haujengi ila unabomoa.
Look at your ID eti Mauza uza!. Shame on you
 
So what? Kwani alichoandika analaumu jirani zetu? Anaeleza hali ilivyo nchini. Au wewe unafurahia tunyamaze? Wao kule Kenya na Rwanda na burundi , nk. wanaweza kunyamaza?

Mkuu ukiona Mtanzania anabeza masuala nyeti kama haya basi weka question mark kwenye Uraia wake, maanake Raia anaye jitambua hawezi kuhoji uhakiki wa usalama wa nchi yetu.
 
Raisi wa awamu ya tatu ilisemekana nae........
 
Kwa kawaida kama unamshuku mtu yeyeto kuwa sio raia wa Tanzania na una ushahidi uliobayana unachotakiwa kufanya ni kwenda mwenyewe idara ya uhamiaji kuoa taarifa hizo na nakuhakikishia uhamiaji watalifanyia kazi hilo suala.Hii habari ya kumhisi mtu bila ushahidi kwa ajili tu ya chuki binafsi sio uungwana.Mipaka ya nchi nyingi za kiafrika haikuwekwa na waafrika wenyewe,kwa mantiki hiyo makabila mwengi yaliyoko Tanzania yana maingiliano na makabila au itikadi na utamaduni wa nchi za jirani.Ili kujiridhisha kuwa huyu ni mtanzania au sio ni suala la uhamiaji na mara tu wakikuona una nyaraka zinazothibitisha asili yako hata kama una baadhi ya ndugu zako kenya,una haki ya kafaidi haki zote kama mtanzania.Hizi habari za majungu tujaribu kuziepuka na hasa kama hakuna ushahidi.
 
Inashangaza sana katika dunia ya leo,mwafrica bado anaona nongwa mwenzake kupata isitoshe,ubaguzi wa rangi,kabila ndio chimbuko letu. Sio ajabu tuna laana.
Sioni tatizo mkenya,mrundi,au mnyaruanda, na wengine wote nchi jirani kufanya kaz tanzania mana nyinyi watz ni watu wa ajabu na washenzi.
Mimi ningekuwa magufuli nawaacha wafanye kazi na nitawalinda. Watz ni wavivu,wezi,wapenda starehe na kutia a tu.

Kweli kabisa!! Kumbe hakuna haja ya kuweka mipaka,waondoe vitambulizo vya Kitaifa/Passport, wapeleke mswaada UN wa ku-disolve mipaka yote ya Nchi 52+ za Kiafrica Bara lote liwe Taifa moja!!

Tusitake kuchanganya masuala ya usalama wa nchi yetu na mambo mengine, mtu ungetegemea kwamba kwa kuwa Taifa letu limewahi kukumbwa na vita basi at least Raia tungekuwa makini zaidi na watu ambao si raia wa Tanzania, walio sema "once bitten twice shy" si wajinga. Ambao hawakumbuki maafa hayo ya vita ndiyo wanakuja humu na hoja za kulahumu watanzania wenzao na vices chungu mzima eti sisi tuna wivu, wavivu and what have you - jaribu kwenda Kenya ujifanye unaweza kufanya lolote nani ya East Africa alafu uone litakalo kutokea -tumekalia usanii tu hata kwenye mambo ambayo ni hatarishi kwa usalama wetu.
 
Kwa jinsi
Kwa jinsi ulivyoandika inaokekana unaandika kichuki chuki tu na ukiambiwa wataje au waonyeshe sidhani utaweza, ijapokuwa inawezekana kweli wapo, kila mwananchi anatakiwa awe na uchungu na nchi yake na kuilinda, kama kweli umefanya utafiti na unauhakika na unayoyasema na unajua athari za watu kama hao, kwanini usiende kutoa taarifa idara zinazohusika na uwape ushahidi wako.
tulivyo wa Tz hata ukitoka taarifa ni bure, pia suala la kuwataja ni kujiongezea uhasama, mbona hayo mambo yapo tu hata kwenye secta binafsi waganda na wakenya wamejaa, mfano mdogo tu tembelea mkoa wa kagera kwenye viwanda vya kubangua kahawa utajionea mwenyewe.
 
Mkuu kukagua vyeti tu hakutoshi, hata RITA ni janga tupu wanatoa vyeti vya kuzaliwa bila ya ku counter check taarifa za muhusika, mtu anasema nimezaliwa kijiji fulani baba na mama majina yao ni haya, RITA hawafanyi upelezi wa kina kama taarifa ni sahihi au la - hawafanyi kabisa!! Kagame haijiamini bila sababu anatujua mpaka jikoni, sisemi ana nia mbaya na Taifa letu lakini watu wake wametapakaa sana nchini na wengi wao wameajiliwa kwenye taasisi nyeti na si Wanyarwanda tu hata Wakenya, sasa hii ni kitu hatarai likitokea la kutokea tutapata wakati mgumu - tusiji amini kupita kiasi.

Kuwadhibiti watu kama hawa ni kuwambia waseme shule ya msingi walisoma wapi, waseme na baadhi ya wanafunzi walio soma nao na mwalimu mkuu alikuwa nani, waseme na majirani wao hapo kijijini ni akina nani - majibu yao yafatiliwe mpaka vijiji wanavyo dai walizaliwa na kukulia, wakidai walikulia mjini basi Baba zao wafatiliwe na kubaini ukweli - tusilete mchezo kwenye masuala ya Usalama wa Taifa letu.
Mfumo wa sasa ni mbovu sana. Cheti cha kuzaliwa na nyaraka zingine zinazothibitisha utaifa/uananchi zinaweza kutolewa pale mtoto anapozaliwa, lakini hali ni tofauti, unakuta kijana wa kitanzania anatafuta cheti cha kuzaliwa pale anapotaka natafuta ajira tu. Serikali yetu haiko serious kabisa. Wanasema wanataka kuleta maendeleo wakati hawana taarifa za hao wanaotaka kuwaletea maendeleo!
 
Mkuu kukagua vyeti tu hakutoshi, hata RITA ni janga tupu wanatoa vyeti vya kuzaliwa bila ya ku counter check taarifa za muhusika, mtu anasema nimezaliwa kijiji fulani baba na mama majina yao ni haya, RITA hawafanyi upelezi wa kina kama taarifa ni sahihi au la - hawafanyi kabisa!! Kagame haijiamini bila sababu anatujua mpaka jikoni, sisemi ana nia mbaya na Taifa letu lakini watu wake wametapakaa sana nchini na wengi wao wameajiliwa kwenye taasisi nyeti na si Wanyarwanda tu hata Wakenya, sasa hii ni kitu hatarai likitokea la kutokea tutapata wakati mgumu - tusiji amini kupita kiasi.

Kuwadhibiti watu kama hawa ni kuwambia waseme shule ya msingi walisoma wapi, waseme na baadhi ya wanafunzi walio soma nao na mwalimu mkuu alikuwa nani, waseme na majirani wao hapo kijijini ni akina nani - majibu yao yafatiliwe mpaka vijiji wanavyo dai walizaliwa na kukulia, wakidai walikulia mjini basi Baba zao wafatiliwe na kubaini ukweli - tusilete mchezo kwenye masuala ya Usalama wa Taifa letu.
Mfumo wa sasa ni mbovu sana. Cheti cha kuzaliwa na nyaraka zingine zinazothibitisha utaifa/uananchi zinaweza kutolewa pale mtoto anapozaliwa, lakini hali ni tofauti, unakuta kijana wa kitanzania anatafuta cheti cha kuzaliwa pale anapotaka natafuta ajira tu. Serikali yetu haiko serious kabisa. Wanasema wanataka kuleta maendeleo wakati hawana takwimu za hao wanaotaka kuwaletea maendeleo!
 
Kwa jinsi

tulivyo wa Tz hata ukitoka taarifa ni bure, pia suala la kuwataja ni kujiongezea uhasama, mbona hayo mambo yapo tu hata kwenye secta binafsi waganda na wakenya wamejaa, mfano mdogo tu tembelea mkoa wa kagera kwenye viwanda vya kubangua kahawa utajionea mwenyewe.
Hatuwezi kuacha kutoa taarifa kwenye mamlaka husika eti kwa sababu taarifa zinaweza kupuuzwa. Xhenophobia iliyotokea Afrika Kusini ilitokana na tatizo la wageni wanaokimbilia nchini humo na kushika fursa nyingi huku serikali ikipuuzia tu. Wasouth wakaona isiwe tabu maana serikali yao iko kimya ndipo waliamua kufanya unyama mkubwa ili tu kupeleka ujumbe kwamba wageni hawatakiwi nchini mwao, serikali ya zuma ilipoona mambo yameharibika ikajifanya kuwaunga mkono wasouth ili kuficha uzembe wao, ikafika hatua polisi wa Afrika kusini anasaidiana na wananchi kuwaatesa wageni. Ni vizuri hatua zikachukuliwa mapema ili kuondoa shari inayoweza kutokea baadae.
 
Back
Top Bottom