Patriot
JF-Expert Member
- Feb 11, 2008
- 5,745
- 4,852
Mi nakupongeza. Achana na hao watu ambao badala ya kujadili wao wanaona eti ni chuki. Chuki ya nini? Kenya hata kama m-TZ ataajniliwa kwa kazi ya kimataifa, bado wanaona ni tatizo kwao utadhani ni ajira ya serikali yao.WAKUU, katika utafiti wangu nimegundua kuna raia wa kenya wengi sana wameajiriwa katika public service, waganda pia wapo wengi, warundi na wanyarwanda wapo wengi sana. binafsi kufanya kazi katika private sector najua kuna sheria inayowaruhusu kama wakitimiza vigezo, lakini imefika kipindi wanaajiriwa serikalini wakiwa wamefoji vyeti vya kuzaliwa na passport na kujifanya watanzania. usalama wa nchi upo wapi hapo? mtu akifanya kazi serikalini na yeye sio mtanzania anaweza kupeleka siri zote nchini kwake, na akibadilisha vyeti, ndi kabisaa, watoto wake watahesabika watanzania hata bila kuwa naturalized, naiomba serikali ifanye hivi:
hapa juzi, Arusha walionekana wakenya na waganda wakiandikisha watoto wao kwenye vizazi na vifo.
- serikali ikague vyeti vyote vya wafanyakazi serikalini, kuanzia vyeti vya kuzaliwa, vyeti vya shule na vyuo, passport etc na wafanye check up na RITA, uhamiaji na shule wanazosema wamesoma etc.
- wananchi wa Tanzania watoe siri, ukiona unamtilia shaka raia yeyote anayefanya kazi kwenye public sector, peleka siri hiyo uhamiaji ili uahmiaji waje wamkague kujiridhisha.
- wengine wengi ni wanawake walioolewa na watz lakini bado hawajachukua uraia.
kuna wafanyakazi wengi tu mimi nimeshawaripoti, wengine wanafanya kazi sector muhimu kabisa za serikali, wamefoji vyeti vya kuzaliwa, passport, na vya shule ili waonekane walizaliwa hapa na kusoma hapa, lakini nyuma ya pazia wana vyeti na pass za nchi zao. ni lazima tushirikiane kufichua suala hili.
nchi inayokaa na wageni wa namna hii ni hatari sana kwa usalama wa nchi, no wonder hata kagame alikuwa na guts za kututishia kuwa atatupiga, kwasababu kuna wanyarwanda wengi wanaojifanya watanzania na wengine hata ukiwaangalia kwa sura tu hauulizi mara mbili. siwabagui lakini usalama wa nchi kwanza, uafrica mashariki baadaye. mtaniwia radhi. wakenya ndio wengi sana, mrundi mmuja nakumbuka alikamatwa anafanya kazi tume ya sayansi na technolojia, mwignine alikamatwa mkenya akifanya kazi tanzania investment centre, mwingine alikamatwa mganda akifanya kazi uhamiaji, kuna wengi sana hawajakamatwa lakini usalama wa taifa sijajua kama wamefanya shughuli yao vya kutosha. MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Binafsi naomba wa-TZ wote kama kuna mtu unamfahamu, peleka jina uhamiaji na ofisi ya katibu mkuu kiongozi maana uhamiaji walishaharibikiwa kwa miaka zaidi ya 10. wao wenyewe watu wa uhamiaji walikuwa wakiwasaidia wageni kuwa raia kwa njia za mkato.