Ni Mimi Msiogope
JF-Expert Member
- May 28, 2012
- 352
- 201
Pasco umemaliza kila kitu. Watu sio kuwa wanamzuia kusema bali hizi tabia za tisha toto zinaonyesha anachotaka kusema (tena kwa wakati huu) kina malengo maalum. Hapa hajasema kitu tayari tafsiri zimekuwa nyingi kwa kadri kila mtu anavyotamani iwe. Hata kama hata sema tayari kuna damage fulani hivi ambayo ishatokea. Huyu bwana akija hapa na kusema " yale yote niliyosema mahakamani ndio ukweli wenyewe na MUNGU ni shahidi yangu kuna watu watasema kesha tishwa ndio maana kasema hivi.
Aliloonyesha Deus naungana nawe ni tabia za kike kabisa.
Sent from my iPad using JamiiForums
Acha kupotosha mkuu dialo kaingiaje kwenye Haki saga .umma wa watanzania unataka kujua who was behind chacha death
nimesoma nimekuelewa ndugu mallya
lakini ni lini utasema? Pia kinachonitia mashaka ya unachotaka kusema ni kujitokeza kundi linalopinga wewe kusema. Hili kundi ni la nani? Liko chini ya nani? Wanataka unyamaze kwa faida za nani?
Kuelekea uchaguzi tutasikia mengi sana. Tutaambiwa yooote yaliyo hovyo na ambayo hayasitahili kusemwa. Wewe mahakamani ulishindwa KUJITETEA na siri kila siku zinavuja unavyotumika vibaya kama dodoki. Wewe sema tu yote usitishie humu,maana wenzako walitengeneza Mkanda wa ugaidi ukweli ukajulikana. Na wewe sema ukweli tu.Salaam!
Kwa muda Mrefu nimekuwa nikipata msukumo unaonitaka kuzungumzia maneno yaliyosambaa mitandaoni na kwenye vyombo vya habari hivi karibuni kutoka kwa ndugu ma makundi mbali mbali.
Kimsingi sintajibu wanayotaka kwa sababu nimeendelea kupokea jumbe za Matusi na kejeli hata kuvamiwa na wanaodai ni wafuasi wa CHADEMA wakitaka niendelee kuwa Kimya!. Wapo walioamua kujitaja majina yao ili nijue ni kiasi gani wako 'Serious' kwenye kile wasemacho!.
Japo nilishatoa taarifa Polisi, kwa sasa nimechoka kuishi maisha ya kuwindwa ndani ya Nchi yangu. Nimechoka. Nitakachofanya ni KUONGEA na si KUJIBU kilichosemwa na yeyote kuhusu Mimi na 'Ajali ya Pandambili'
Naamini kwa Mungu siku zote
Naamini nikifa ni kwa Mpango wake
Nikifa ukweli Utaishi hadi vizazi vijavyo.
Deus Mallya
Dar es Salaam.
mbona mnahangaika sana? Kwani mmeshajua anachotaka kusema?
Mkuu Deus Mallya, kwanza asante kwa kuamua kutaka kusema!.
Moja ya tabia za kiume kwa mwanamume ni kuwa na msimamo thabiti, msimamo imara, akiamua kitu, ameamua na anasimama nacho mpaka mwisho wake, na ikibidi kufa, anakufa na msimamo wake huku akiitwa shujaa!. Sasa wewe kama ni mwanamume na unazo tabia za kiume, ulipoamua kukaa kimya na kunyamaza, ni lazima uendelee kukaa kimya na kunyamaza mpaka mwisho!.
Hili tishio la oh mara ntasema, au wakati wa kusema umefika!, hizi ni tabia za kike!, mwanamume akiamua kusema, hasemi ntasema bali husema!. Mwanamke ndio huamua kutishia aseme au asiseme, na hata akitong..zwa anajijua kabisa amekubali, atajifanya hataki ili uonyeshe kuhangaika kumpata!.
"Sizungumzi kwa utani nayajua ninayoyasema. Nilichoweka akiba ni kuwataja watu kwa majina. Wasidhani nikienda wizarani nikasema watu hawa wanakula rushwa wasidhani siwajui kwa majina, ninawajua; bali kwa sasa ninatoa muda kwa watu hao wajisahihishe. Mwenye masikio nadhani atakuwa amesikia," alisisitiza.
Raia Mwema - Mikwara hii ya Kikwete kwa wahalifu haisaidii
Hii ya wewe kutishia kuwa utasema, its as if ulilipwa kiasi fulani hapo mwanzo ili unyamaze, na ukanyamaza, sasa umeishiwa, unataka kuendelea kulipwa siku zote kwa kukaa kimya!, yaani ukimwa wako ndio ajira yako, ili uendelee kulipwa, unatishia kusema ili watishike na kukulipa tena ili usiseme, ukae kimya!.
Nakushauri, kama umeamua kweli kusema, amua moja na useme sasa!, hukupaswa kusema utasema, ulipaswa useme tuu tujue moja, kitendo cha kutishia nyau kuwa utasema, kinaweza kupelekea wale waliokulipa siku zote kukaa kimya, wakakuona you are not an asset, you are a liability which needs disposal kabla haijawa too risky or threat, hivyo ukanyamazishwa jumla!.
Ni ushauri tuu.
Asante.
Hiyo ni hatua ya pili ya kimahakama lakini ya hatua ya kwanza ni umma kuelewa andiko lake Deus Mallya kwanza kwa ufafanuzi wa kifasihi kama ilivyoonyesha na iwapo siyo kweli yeye yupo hapa jukwaani atakuja kukanusha.Wewe pia una matatizo makubwa, pengine kuliko huyu mgonjwa wa akili.
Hapo hatuongelei fasihi tunaongelea kosa la jinai. Kosa la jinai huthibitika kwa kauli yenye ushahidi usio na shaka. Hivi nikikuuliza maswali haya hapa chini una jibu la maana?
1) Una uhakika gani kuwa ni kweli Malya kuna watu wanamtishia maisha
2) Kuna ugumu gani kusema kuwa ametishiwa na mwanachama wa CCM au CHADEMA?
3) Hao wanachama wa CHADEMA waliomtishia kwa nini hawataji majina yao?
4) Polisi walimhoji kabla ya kupelekwa mahakamani, kwa nini hizo siri asizitoe huko polisi kama aliwaogopa watuhumiwa?
5) Kesi ya jinai huwa haina mwisho, kwa maana ya muda. Kama kuna chochote kilimfanya wakati akihojiwa kwa mara ya kwanza ashindwe kuwataja watuhumiwa, na sasa yupo tayari kuwataja, kwa nini asipeleke taarifa hizo polisi ili kesi ianze upya?
NB: Ukishabikia maneno ya kijinga toka kwa mwendawazimu ni dhahiri nawe ni mwendawazimu.
- HA! HA1 HA! HA! HA! mbona mnaaanza kutoka mapovu kabla mwananchi hjasema lililotokea mnajua kumbe kilichotokea ha! ha!
Le Mutuz
Mkuu unaandika humu JF kututishia au? Mbona JF sio mahali pake? Usisemee humu JF. Nenda kwa DPP au kwa IGP au kwa Werema, au Jaji Mkuu. Hao ndo watakusaidia. Watayapima maneno yako, wakiona yanafaa kwa lolote watayachukulia hatua.
Kutishiwa mbona jambo la kawaida tu. Hata kuuawa, mbona jambo la kawaida tu. Hujasikia binti aliyefanyiwa unyama wa kutisha wiki ilopita halafu bado wakauchukua na uhai wake, na kumweka uchi mtaroni?
Usiogope, sema lakini semea mahali stahiki, na ni kwa hao nlokuambia. Kama ulifungwa kwa kuonewa, nenda kwa walio tofauti na serekali. Tafuta msaada, Haki za Binadamu. Usitishie watu na weye kuwa unajua kuchonga. Amka asubuhi, chonga sana ila chongea penyewe wala usipotee njia mchongo wako ukapotea tena.
Hivi jamani,,ndugu yangu Ben Saanane yuko wapi..,mbona simuoni akitokwa mapovu kwenye thread kama hizi...yaani Mzee wake anakaribia kupelekwa lupango na yeye amekaa kimya kama hayamuhusu..njoo uwaambie umma wa JF kuwa hatuhusiki na atakachosema Mallya ni uzushi.
Ulikua wapi siku zote?, tuiite nini hii? maana ni zaidi ya njaa na unafiki uliokubuhu,
Nyie mnaoekti uana siasa ni washenzi sana......
Duh "Benazir" !
Sasa mimi naingiaje hapa? Povu ulilotoa hapa linatosha.Niongeze lingine la nini?