Wakati Serikali ikiendelea kuficha ukweli kuhusu COVID 19, baadhi ya Watanzania wenzetu inawatesa

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Pengine watu wanaweza kufikiri kuwa sisi baadhi yetu tunaisakama sana Serikali kuhusu COVID 19 kwa kutumwa na mabeberu, la hasha! Tunafanya hivyo kwa kuwa tunawapenda sana ndugu zetu na watanzania kwa jumla.

Inashangaza sana kuona serikali inayojiita serikali makini ikitoka hadharani na kuitambia dunia kuwa Tanzania COVID 19 imepungua sana na hitokaa itokee eti maambukizi yaongezeke. Matokeo yake watanzania wengi wameamua kuishi kwa namna ya ajabu kabisa. Haya ni matokeo ya kunyimwa ukweli na wakulaumiwa ni Serikali na Wizara ya Afya kwa jumla.

Ninasema hayo kwa kuwa nimeshuhudia ndani ya siku za hivi karibuni Watanzania wenzangu wakisimbuliwa na homa kali na kikohozi huku wakiwa na dalili nyingi za Corona! Serikali iko wapi?

Kama kwa hakika tutaendelea hivi na hii tabia ya kupuuza puuza kutokana na asili yetu watanzania na mbaya zaidi tunao sasa viongozi wanaoendana na asili yetu basi tutajikuta tuligharamika kwa kiwango kikubwa na matokeo yake ni nchi kuanza kupata midororo mikubwa ya kibiashara.

Nitoe Rai kwa serikali, kusema kuwa baadhi ya Wataznania wanasumbuliwa na Corona si dhambi, kutoa tahadhari na kuhimiza watu kujikinga si dhambi. Dhambi ni mwenenndo ambao kwa sasa tumeamua kusafiri nao.

Tuweke kumbukumbu ili siku moja tuje kusemezana bila haya
 
Korona ipo na inaendelea nasi tunahitaji kula na serikali inahitaji kodi lazima tuishi nayo anaeumwa atibiwe tusioumwa tuendelee kupiga kazi atakaekufa siku zake zimefika!

Ni wakati sasa tufunge mjadala wa korona ni hakika sasa ni old story na inakera sababu hatumudu lockdown kwanini tupoteze nguvu kuzungumzia korona?
 
Korona ipo na inaendelea nasi tunahitaji kula na serikali inahitaji kodi lazima tuishi nayo anaeumwa atibiwe tusioumwa tuendelee kupiga kazi atakaekufa siku zake zimefika! ni wakati sasa tufunge mjadala wa korona ni hakika sasa ni old story na inakera sababu hatumudu lockdown kwanini tupoteze nguvu kuzungumzia korona?!!
Fact
 
Mkuu, bandiko lako hili linaweza kuwa na maana sana kama wewe uliyeandika bandiko hili ni mtalaam wa tiba tena anayeona wagonjwa kila siku kwa lengo la kutibu. Unaposema kuwa kuna watu unaowaona wakiwa na vikohozi vyenye dalili zinazofanana na COVID 19, haina maana kuwa vikohozi vyao vinasababishwa na virusi vya Corona.

Nikushauri tu uwaache watalaam wa tiba wafanye kazi yao bila kuingiliwa na mambo haya ya kisiasa kwa sababu wao ndio wenye vipimo vinavyothibitisha kuwa kinachomfanya akohoe ni vijidudu vya aina gani. kama ni mwanahabari basi jikite kwenye maadili ya kazi yako, vinginevyo unaonekana kama mchochezi fulani hivi.
 
Tumezika watatu juzi hapa mtaani. Majeneza yamepigwa tepu na wamezikwa na wajuba wenye suti nyeusi.
 
Wewe ndio huwelewi au unajitia ujinga usio nao.

Wenyewe wenye mamlaka wamesema corona ipo na umchukue taadhari. Wamesema imepungua sio imeisha yote. Ingekuwa imeisha wasingesema tuendelee kuchukua taadhari. Sasa usichoelewa nini.

Weka siasa pembeni, jilinde wewe na umlinde mwenzio. Kama unahisi kuna mtu atakuja kukuhubilia kuhusu afya yako subiri.

PM juzi tu hapa kasema wagonjwa wapo 100, hii ni baada ya rais na ummy kusema wamebaki wanne hospital. Sasa unataka kuhubiriwa kama tupo Kenya?
 
G Sam,

Afadhali umetanabaisha kwamba tunaweza kufikiri mnatumiwa na Mabeberu, na huo ndio ukweli. Hivyo basi, fanya ulichotumwa ili upate ujira wako. Tunachofahamu ni kwamba Mungu amemtumia Rais wetu kutuonesha njia ya kuishi japo mnasema kunao huo ugonjwa.
 
Mkuu, bandiko lako hili linaweza kuwa na maana sana kama wewe uliyeandika bandiko hili ni mtalaam wa tiba tena anayeona wagonjwa kila siku kwa lengo la kutibu. Unaposema kuwa kuna watu unaowaona wakiwa na vikohozi vyenye dalili zinazofanana na COVID 19, haina maana kuwa vikohozi vyao vinasababishwa na virusi vya Corona.

Nikushauri tu uwaache watalaam wa tiba wafanye kazi yao bila kuingiliwa na mambo haya ya kisiasa kwa sababu wao ndio wenye vipimo vinavyothibitisha kuwa kinachomfanya akohoe ni vijidudu vya aina gani. kama ni mwanahabari basi jikite kwenye maadili ya kazi yako, vinginevyo unaonekana kama mchochezi fulani hivi.
Kwanini mamlaka hazijikiti kuhimiza watu wajihadhari na kuelezea uelekeo wa ugonjwa huo nchini? Yes nipo karibu sana na wanaoathirika na hili janga na kwa hakika katika mwezi huu wa sita hali imeendelea kuwa ya kutokuridhisha kabisa!
 
Afadhali umetanabaisha kwamba tunaweza kufikiri mnatumiwa na Mabeberu, na huo ndio ukweli. Hivyo basi, fanya ulichotumwa ili upate ujira wako. Tunachofahamu ni kwamba Mungu amemtumia Rais wetu kutuonesha njia ya kuishi japo mnasema kunao huo ugonjwa.
Kama njia inayotumiwa na watanzania kwa sasa kama tunavyoiona ni hiyo wanayosema Mungu kamtuma mtumishi wake tuishi hivyo basi huyo Mungu aliyemtuma hawapendi Watanzania.
 
G Sam,

Unajichanganya mwenyewe, corona ipo tena sana isipokuwa wengi wanaumwa na kupona wenyewe huo ndio ukweli, kwa kifupi huu ugonjwa tulitishwa sana na serikali ililitambua hilo, rejea tuliambiwa afrika tutaokota maiti barabarani viko wapi vitishi hivyo?? hata wewe waweza kuta corona ilishakupitia then ukadunda, kama hizo dalili unazozisema mimi nilizipata mafua ya kutosha wiki mbili zilizopita ila leo naendelea na yangu.
 
Kama Serikali yoyote inaongozwa kwa MHEMKO basi hapo Kuna MASHAKA ...KIVIPI?!!!!!

TUWEKE HISIA PEMBENI NA TUKUBALI KUWA CORONA IKO DUNIANI NA WENZETU WALITUTABIRIA VIFO ZAIDI YA UHALISIA....

UNAPOKUWA NA UGONJWA WA MILIPUKO la muhimu ni KUKUMBUSHANA tahadhari na WANANCHI wachukue HATUA.
(SERIKALI INALIFANYA HILI)

KUHUSU DATA ZA MORTALITY RATE SI jukumu la kila mmoja KULIJUA...Bali NI watu husika wa afya na serikali tu.
KWA NINI BASI?!!!
Jibu lake NI rahisi Sana....hebu jalia nchi yetu iko vitani...VIJANA wenzetu WANAPAMBANA mstari wa mbele HALAFU kila WAKIUAWA kwa WINGI mapambanoni,RAIS,CDF ama wizara ya ulinzi inatoa TAKWIMU ZA MASSES OF FALLEN COMPATRIOTS kweli?!!!!

TUTAFAKARI jamani.
Karibuni mchupa wa FARU JOHN hapa mbugani Sadani,nimekuja kufurahia baada ya HAPA KAZI TU.
 
Back
Top Bottom