Wajue Mahasimu wa Januari Makamba

Huyu jamaa huwa anawalipa watu waje kumtetea mitandaoni pale kukiwa na Jambo!

Nakumbuka kwenye Kashfa Kumtumia Dada ake kupiga deals, ilikua hivi hivi....

Ni mtu wa ajabu sijawahi kuona....
Nchi hii ukifanya kazi njema utaonekana, ukiwa Jambazi, mla rushwa utajulikana....

Wanaomtetea hapa wapo kazini!
 
Makamba hamtamuweza... he is so smart upstairs....

CCM iko mikononi mwa maza..tulieni hamna namna nyie timu sukuma gang.. ni wakati wenu wa kusurubiwa...kutesa huwa ni kwa zamu.

Mwendazake kashaondoka bila kuaga...so tulieni kuhangaika na Makamba ni kujichosha tu..

Presidential material unahaingaika nayo..rubbish
Smart upstairs halafu akaiba mitihani ya secondary hadi akafutiwa matokeo?!

Makamba zaidi ya kubebwa na jina la baba yake hana rekodi yoyote ya maana kwenye utendaji, na mpaka ameanza "kuota ndoto" za urais anajua atabebwa awekwe ikulu na bosi wake, NEC, na polisi, hakafu ajiite "Rais wa JMT"
 
Asilimia 98 ya wachangiaji wanaonekana kutokubaliana eidha na tabia za Makamba nje ya utumishi wa Uma au ubadhilifu wa mali za Uma wakati akiwa katika utumishi wa Uma.

Hii iwe wito wa uamsho kwa Mhe.Rais kutambuwa yupo na waziri wa aina gani kwenye baraza lake.

Vinginevyo, jumba bovu litamwagukia kwa kukusudia kumlinda kwa maslahi yasiojulikana kama ni ya Uma au la!



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mageuzi makubwa yanayofanywa ndani ya TANESCO na Wizara ya Nishati yametengeneza makundi ya Chuki watu walizoea kujipa tender za ku supply nguzo, transforma, mita, vifaa, engine za kufua umem na mashine wamekuja juu kutaka Waziri Makamba aondoshwe wakihofia kupotezea tenda zao.

Ifahamike kuwa miaka mitano ilopita kipo kikundi kilihodhi tenda zote za mabilioni sasa wakati huu ambao mtu wao aliyekuwa Waziri hayupo kelele zimekuwa nyingi mitandaoni. Waziri wa sasa Januari Makamba ameendelea kuhimiza uwazi kwenye tender zote na pia kuhakikisha Tanesco na wizara wanapata supplier mwenye uwezo wa kutosha.

Kwa sasa kikundi kile cha walafi kimedhamiria kukwamisha serikali ya awamu ya Sita kwa kuchafua watu muhimu akiwemo Januari Makamba ili aondolewe na mtu wao apate nafasi tena waendelee kuneemeka.

Kiwanda chao cha nguzo sasa kinapumulia mashine wanawaza mabilioni waliyowekeza yatarudi vipi na sasa wameamua kupambana na Makamba.

Januari Makamba chapa kazi
Rais Samia anajua kazi yao
Waache walikosa tenda waendelee kukunanga mitandaoni
Ukiitazama hii picha na alichosema Makamba ni vitu viwili tofauti,hivyo anaukwamisha mradi wa bwawa la Mwl Nyerere kwa maslahi yake na team yake
JamiiForums-1782699355.jpg
 
Ni Waziri wakwanza aliyetumia akili nchi hii mifuko iliisha bila sisimizi kuumizwa
The man is incredible na nazan uwezo wake unawapa tabu sana
Kwa hiyo wewe ni 'chawa' wake, au ndio wenye 'tender' wapya!

Sehemu ya mada yako inaweza kuwa kweli kabisa, lakini unachafua ukweli huo na huu uongo mpya unaokuhusu wewe na Makamba wako.

Hivi huwezi kusimama na Tanzania bila ya kuegemea kwa hawa wapigaji wa kila upande?

Upigaji ni upigaji tu, haijalishi anayepiga ni Makamba au Kalemani.Wote ni maadui wakubwa wa nchi hii.
 
14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom