Wajamaa mnisaidie, hivi Nyerere aliwezaje kuvumilia haya?

MALCOM LUMUMBA

JF-Expert Member
Jul 26, 2012
20,897
63,784
Huwa najiuliza sana lakini sipati majawabu, lakini naomba wasomi wa humu ndani mnisaidie.

Hivi Mzee Nyerere alikuwa ana roho ya namna gani kuona mambo kama haya yakitokea kwa wananchi lakini bado hataki kubadilika na akaendelea kutumia mkono wa chuma kuhakikisha anasigina kabisa uwezo binafsi wa mtanzania kuweza kujikwamua kiuchumi. Ujamaa wa Tanzania hakuleta matokeo yoyote makubwa na ya kuchangaza ukilinganisha na kule Asia na Ulaya ambako walau walifanya mapinduzi ya sayansi na teknolojia.

Uchina walifanikiwa sana baada ya Raisi Deng Xiaping kuanza kuwaonea huruma raia wake akifahamu kabisa kwamba njia waliyokuwa wanaenda ilikuwa siyo sahihi. Aliruhusu watu waanze kumiliki mali zao binafsi na kufanya biashara. Najiuliza sana, miaka yote 18 ya Ujamaa, yalifanyika na kutokea mambo mengi mno kwa watanzania, kiasi kwamba kiongozi yoyote mwenye huruma na wananchi ni lazima angekaa chini na kujifanyia tathmini, lakini Raisi Nyerere hakufanya hivyo, aliendelea kuwa na moyo mgumu kama Farao. Hebu tuzingatie haya:

1. Sera ya utaifishaji wa mali, ilileta umasikini mkubwa sana kwa watu.
2. Kufuta vikundi ya ushirika (Cooperatives) na kuweka vile vya TANU kulididimiza mno sekta ya kilimo.
3. Kupiga marufuku watu binafsi kuagiza bidhaa nje ya Tanzania kulipelekea uhaba wa bidhaa na huduma muhimu.
4. Kuweka ugumu katika kusafiri (Travelling Restrictions) kulisababisha ukosefu wa ujuzi kwa watanzania.
5. Kuminya uhuru wa mawazo na kutumia nguvu ya dola kunyamazisha watu kulidumaza ukomavi wa demokrasia.

Mpaka kufika miaka ya 80's Ujamaa ulikuwa umefeli vibaya mno. Tanzania tulikuwa hatuna hata unga wa kupikia, mafuta, wala sukari. Mtaa mzima mlikuwa mnaenda kwa mwenyekiti kuomba sukari au sabuni kutoka maduka ya ushirika. Ukikamatwa na mafuta, sabuni au dawa za binadamu zilizolanguliwa kutoka Kenya lazima ushughulikiwe na dola. Kama ulisoma miaka ya 80's unaweza kukumbuka kwamba hata sare za shule zilikosa rangi, watu tukawa tunavaa vitu vya ajabu vilivyochakaa kama vile vichaa. Ukibahatika kukutana na wamishionari au taasisi za kidini ndiyo ulikuwa unaweza kupewa hata nguo, mahitaji na wazungu.

Yote haya yanafanyika, Mzee Nyerere na Sokoine wakaingia mtaani kuanza kushughulikia maelfu ya watanzania ambao wanahujumu uchumi. Ila ukifuatilia zile kesi nyingi, utafahamu kwamba hao wahujumu uchumi ni wale watanzania wenye akili za haraka ambao walijiongeza na kuweza kupata mahitaji muhimu ili kuhudumia familia zao. Wahujumu uchumi kwelikweli, ambao wengi walikuwa ni vigogo wa serikalini hawakuguswa. Kiukweli, kama nchi ina kiongozi mwenye huruma haya yote yasingetokea bila yeye kujirudi.

Hivi kwanini MTAKATIFU na MWENYEHERI, Raisi Nyerere hakuwa na chembe ya huruma moyoni ?
Kuna mambo nikikumbuka huwa naumia sana na nakosa majawabu. Hivi alikuwa anapenda kutuona sisi vile ?​
 
.Hivi kwanini MTAKATIFU na MWENYEHERI, Raisi Nyerere hakuwa na chembe ya huruma moyoni ?
Kuna mambo nikikumbuka huwa naumia sana na nakosa majawabu. Hivi alikuwa anapenda kutuona sisi vile ?​
Mkuu The Boy Wonder , asante kwa bandiko hili, hata hivyo majibu ya bandiko hili, hayatasaidia lolote kwenye ule mchakato, mchakato unaendelea!.
P
 
MTAKATIFU na MWENYEHERI,​
20231014_130156.jpg
 
Mkuu The Boy Wonder , asante kwa bandiko hili, hata hivyo majibu ya bandiko hili, hayatasaidia lolote kwenye ule mchakato, mchakato unaendelea!.
P
Hata wakimtangaza kuwa ni mungu hilo halinihusu hata kidogo, ila ntakachouliza ni kwanini huyu mnayemuita mungu wenu alikuwa na moyo mgumu, wa jiwe kama Firahuni ? Alikuwa anapata faida gani kutuona sisi tunaishi vile ?
 
Watawala wengi ndani ya bara la Afrika, hupenda madaraka kuliko kitu chochote.Ni heri taifa lipatwe na matatizo lakini wao,huwaza madaraka zaidi kuliko ustawi wa watu.

Kitendo cha kuua demokrasia na kuanzisha mfumo wa chama kimoja kipindi cha Mwl.Nyerere kilionesha nia ya wazi ya hulka ya viongozi wengi wa uroho wa madaraka.

Ndio maana aliona watu wenye maoni tofauti kama wakina Bibi titi,Kambona,Mtei,Mzee Sanga nk kuwa tishio la madaraka yake.Hivyo kulinda madaraka kwake lilikuwa jambo la kwanza kuliko kujali maisha ya watu walio wengi.
 
Huwa najiuliza sana lakini sipati majawabu, lakini naomba wasomi wa humu ndani mnisaidie.

Hivi Mzee Nyerere alikuwa ana roho ya namna gani kuona mambo kama haya yakitokea kwa wananchi lakini bado hataki kubadilika na akaendelea kutumia mkono wa chuma kuhakikisha anasigina kabisa uwezo binafsi wa mtanzania kuweza kujikwamua kiuchumi. Ujamaa wa Tanzania hakuleta matokeo yoyote makubwa na ya kuchangaza ukilinganisha na kule Asia na Ulaya ambako walau walifanya mapinduzi ya sayansi na teknolojia.

Uchina walifanikiwa sana baada ya Raisi Deng Xiaping kuanza kuwaonea huruma raia wake akifahamu kabisa kwamba njia waliyokuwa wanaenda ilikuwa siyo sahihi. Aliruhusu watu waanze kumiliki mali zao binafsi na kufanya biashara. Najiuliza sana, miaka yote 18 ya Ujamaa, yalifanyika na kutokea mambo mengi mno kwa watanzania, kiasi kwamba kiongozi yoyote mwenye huruma na wananchi ni lazima angekaa chini na kujifanyia tathmini, lakini Raisi Nyerere hakufanya hivyo, aliendelea kuwa na moyo mgumu kama Farao. Hebu tuzingatie haya:

1. Sera ya utaifishaji wa mali, ilileta umasikini mkubwa sana kwa watu.
2. Kufuta vikundi ya ushirika (Cooperatives) na kuweka vile vya TANU kulididimiza mno sekta ya kilimo.
3. Kupiga marufuku watu binafsi kuagiza bidhaa nje ya Tanzania kulipelekea uhaba wa bidhaa na huduma muhimu.
4. Kuweka ugumu katika kusafiri (Travelling Restrictions) kulisababisha ukosefu wa ujuzi kwa watanzania.
5. Kuminya uhuru wa mawazo na kutumia nguvu ya dola kunyamazisha watu kulidumaza ukomavi wa demokrasia.

Mpaka kufika miaka ya 80's Ujamaa ulikuwa umefeli vibaya mno. Tanzania tulikuwa hatuna hata unga wa kupikia, mafuta, wala sukari. Mtaa mzima mlikuwa mnaenda kwa mwenyekiti kuomba sukari au sabuni kutoka maduka ya ushirika. Ukikamatwa na mafuta, sabuni au dawa za binadamu zilizolanguliwa kutoka Kenya lazima ushughulikiwe na dola. Kama ulisoma miaka ya 80's unaweza kukumbuka kwamba hata sare za shule zilikosa rangi, watu tukawa tunavaa vitu vya ajabu vilivyochakaa kama vile vichaa. Ukibahatika kukutana na wamishionari au taasisi za kidini ndiyo ulikuwa unaweza kupewa hata nguo, mahitaji na wazungu.

Yote haya yanafanyika, Mzee Nyerere na Sokoine wakaingia mtaani kuanza kushughulikia maelfu ya watanzania ambao wanahujumu uchumi. Ila ukifuatilia zile kesi nyingi, utafahamu kwamba hao wahujumu uchumi ni wale watanzania wenye akili za haraka ambao walijiongeza na kuweza kupata mahitaji muhimu ili kuhudumia familia zao. Wahujumu uchumi kwelikweli, ambao wengi walikuwa ni vigogo wa serikalini hawakuguswa. Kiukweli, kama nchi ina kiongozi mwenye huruma haya yote yasingetokea bila yeye kujirudi.

Hivi kwanini MTAKATIFU na MWENYEHERI, Raisi Nyerere hakuwa na chembe ya huruma moyoni ?
Kuna mambo nikikumbuka huwa naumia sana na nakosa majawabu. Hivi alikuwa anapenda kutuona sisi vile ?​
Hatari sana
 
Mkuu The Boy Wonder , asante kwa bandiko hili, hata hivyo majibu ya bandiko hili, hayatasaidia lolote kwenye ule mchakato, mchakato unaendelea!.
P
Heshima kwako mzee Wangu.

Binafsi naona majibu ndo yatatoa uelekeo wa kujua wapi tulipo jikwaa kama taifa na kuleta dira sahihi ya nini kifanyike ili tusirudie makosa yale yale.

Najua wewe ni muumini wa sera za Mwl.Nyerere hivyo basi mchango wako ni muhimu sana katika mada hii.
 
Tuliiga mfumo wa Ujamaa huko Uchina, ambako Raisi Mao alishawahi kuua mamilioni ya raia wake bila sababu za msingi, kwanza kwenye The Great Leap Foward na The Cultural Revolution. Hadi kufika mwaka 1975, Uchina ilikuwa inaelekea njia moja ya USSR. Ila Mungu mwema, Uchina ikapata Raisi mwenye huruma, Bwana Deng Xiaoping ambaye alifahamu kabisa, With a current trajectory China was doomed to oblivion.

Mzee wa watu alifunga safari hadi Singapore ambako alipewa somo zito sana kuhusu uchumi na Waziri Mkuu wa Singapore, mtaalamu, Lee Kuan Yew. Baada ya kurudi Uchina ndiyo akaanzisha sera za Economic Liberalization ambazo ndizo zilijenga msingi wa Uchina kufika hapa leo. Ila huku kwetu hata baada ya kufahamu kwamba tumekosea, hata tuliowaiga wamebadilika, tukaendelea kushupaza shingo na kuumizana.

Kuna kipindi watanzania tulikuwa hata tukiona baiskeli, redio au televisheni tunaona vitu vya ajabu sana sanaa. Mtu akiwa anakula hata mkate na siagi, vitu ambavyo ni mahitaji ya kawaida duniani kote, tulikuwa tunamshangaa na kumuita tajiri. Tulitumia chemli, karabai na mishumaa kusoma, lakini MTAKATIFU ameshupaza tu shingo hataki kuona hata mtu unamiliki kijiko cha chuma kilichotoka Hong-Kong. Kiukweli huwa nashikwa sana na hasira nikikumbuka baadhi ya mambo.​
 
Hata wakimtangaza kuwa ni mungu hilo halinihusu hata kidogo, ila ntakachouliza ni kwanini huyu mnayemuita mungu wenu alikuwa na moyo mgumu, wa jiwe kama Firahuni ? Alikuwa anapata faida gani kutuona sisi tunaishi vile ?
Mkuu, Mzee PM ni muumini wa sera za Mwl.Nyerere hivyo basi usitegemee mchango wake hasi juu sera za Mwalimu katika kipindi cha utawala wake.
 
5. Kuminya uhuru wa mawazo na kutumia nguvu ya dola kunyamazisha watu kulidumaza ukomavi wa demokrasia.
Kwenye hili Nyerere alikuwa ndiye bingwa. Alikuwa kila anayemkosoa anahama nchi. Ni vile tu ukweli hausemwi na bahati mbaya Nyerere katawala ktk kipindi ambacho media outlets zilikuwa hakuna.

Redio ya taifa ilikuwa inaandikiwa nn cha kusema kuhusu rais kwenye taarifa ya habari.

¶ Nyerere ndiye aliyefanya Kambona kuishi ukimbizini maisha yake yote.
¶ Nyerere ndiye aliyechana vyeti vya Tuntemeke Sanga.
¶ Nyerere ndiye aliyemfunga kifungo cha nyumbani (alimuweka kizuini) Kasangatumbo
¶ Nyerere ndiye alimuondoa kwenye urais Abdul Jumbe halafu akamuweka kizuizini hapo Kigamboni mpk umauti.
¶> Nyerere ndiye aliyetunga hili katiba bovu lililomfanya yeye kujipa umungu wa Tanzania.

Nyerere ni dikteta asiyesemwa.
 
Tuliiga mfumo wa Ujamaa huko Uchina, ambako Raisi Mao alishawahi kuua mamilioni ya raia wake bila sababu za msingi, kwanza kwenye The Great Leap Foward na The Cultural Revolution. Hadi kufika mwaka 1975, Uchina ilikuwa inaelekea njia moja ya USSR. Ila Mungu mwema, Uchina ikapata Raisi mwenye huruma, Bwana Deng Xiaoping ambaye alifahamu kabisa, With the current trajectory China was doomed to oblivion.

Mzee wa watu alifunga safari hadi Singapore ambako alipewa somo zito sana kuhusu uchumi na Waziri Mkuu wa Singapore, mtaalamu, Lee Kuan Yew. Baada ya kurudi Uchina ndiyo akaanzisha sera za Economic Liberalization ambazo ndizo zilijenga msingi wa Uchina kufika hapa leo. Ila huku kwetu hata baada ya kufahamu kwamba tumekosea, hata tuliowaiga wamebadilika, tukaendelea kushupaza shingo na kuumizana.

Kuna kipindi watanzania tulikuwa hata tukiona baiskeli, redio au televisheni tunaona vitu vya ajabu sana sanaa. Mtu akiwa anakula hata mkate na siagi, vitu ambavyo ni mahitaji ya kawaida duniani kote, tulikuwa tunamshangaa na kumuita tajiri. Tulitumia chemli, karabai na mishumaa kusoma, lakini MTAKATIFU ameshupaza tu shingo hataki kuona hata mtu unamiliki kijiko cha chuma kilichotoka Hong-Kong. Kiukweli huwa nashikwa sana na hasira nikikumbuka baadhi ya mambo.​
Mbona uongo mwingi?:)
 
Watawala wengi ndani ya bara la Afrika, hupenda madaraka kuliko kitu chochote.Ni heri taifa lipatwe na matatizo lakini wao,huwaza madaraka zaidi kuliko ustawi wa watu.

Kitendo cha kuua demokrasia na kuanzisha mfumo wa chama kimoja kipindi cha Mwl.Nyerere kilionesha nia ya wazi ya hulka ya viongozi wengi wa uroho wa madaraka.

Ndio maana aliona watu wenye maoni tofauti kama wakina Bibi titi,Kambona,Mtei,Mzee Sanga nk kuwa tishio la madaraka yake.Hivyo kulinda madaraka kwake lilikuwa jambo la kwanza kuliko kujali maisha ya watu walio wengi.
Mifumo siyo tatizo, tatizo ni matokeo na jinsi watawala wanavyoyapokea. Ilifahamika kabisa kwamba Tanzania haiwezi kujikwamua kiuchumi bila wananchi kuwa na hisa kwenye uchumi wao. Tunasingizia vita vya Kagera, ila ukweli ni kwamba Tanzania ilianza kuumia miaka ya 70's kipindi kina Mtei wanamshauri Nyerere lakini hataki kusikia. Kukosea viongozi wote duniani hukosea, tatizo huja pale ambapo kiburi chako cha kukataa matokeo kinagharimu maisha ya mamilioni ya watu waliokuwa wanakuamini.

Hivi kwanini hakukubali mapema kwamba nchi ilimshinda hadi asubiri jeshi na waasi wamtumie ujumbe kwamba amechokwa ?​
 
Kwenye hili Nyerere alikuwa ndiye bingwa. Alikuwa kila anayemkosoa anahama nchi. Ni vile tu ukweli hausemwi na bahati mbaya Nyerere katawala ktk kipindi ambacho media outlets zilikuwa hakuna.

Redio ya taifa ilikuwa inaandikiwa nn cha kusema kuhusu rais kwenye taarifa ya habari.

¶ Nyerere ndiye aliyefanya Kambona kuishi ukimbizini maisha yake yote.
¶ Nyerere ndiye aliyechana vyeti vya Tuntemeke Sanga.
¶ Nyerere ndiye aliyemfunga kifungo cha nyumbani (alimuweka kizuini) Kasangatumbo
¶ Nyerere ndiye alimuondoa kwenye urais Abdul Jumbe halafu akamuweka kizuizini hapo Kigamboni mpk umauti.
¶> Nyerere ndiye aliyetunga hili katiba bovu lililomfanya yeye kujipa umungu wa Tanzania.

Nyerere ni dikteta asiyesemwa.
Haya mengine ya kisiasa ntayazungumzia siku ingine panapo majaaliwa. Ila kilichonileta hapa ni kuuliza kwanini bado aliendelea kutumia mabavu na kulazimisha sera zake hata pale ambapo mamilioni ya watanzania walikuwa wanapitia kipindi kigumu mno kimaisha. Najiuliza kwanini hakuwa hata na chembe ya huruma pale ambapo watanzania wengine walikosa chakula hadi kuchemsha pumba na huku wengine wakilala njaa ? Najiuliza sana, lengo lake haswa lilikuwa ni nini, lakini sipati majibu?​
 
Kwenye hili Nyerere alikuwa ndiye bingwa. Alikuwa kila anayemkosoa anahama nchi. Ni vile tu ukweli hausemwi na bahati mbaya Nyerere katawala ktk kipindi ambacho media outlets zilikuwa hakuna.

Redio ya taifa ilikuwa inaandikiwa nn cha kusema kuhusu rais kwenye taarifa ya habari.

¶ Nyerere ndiye aliyefanya Kambona kuishi ukimbizini maisha yake yote.
¶ Nyerere ndiye aliyechana vyeti vya Tuntemeke Sanga.
¶ Nyerere ndiye aliyemfunga kifungo cha nyumbani (alimuweka kizuini) Kasangatumbo
¶ Nyerere ndiye alimuondoa kwenye urais Abdul Jumbe halafu akamuweka kizuizini hapo Kigamboni mpk umauti.
¶> Nyerere ndiye aliyetunga hili katiba bovu lililomfanya yeye kujipa umungu wa Tanzania.

Nyerere ni dikteta asiyesemwa.
IMG-20220215-WA0000.jpg
JamiiForums-897008524.jpg
 
Back
Top Bottom