Ni kweli adui wa mwafrika ni mwafrika mwenzake, hii trend huwezi kuiona kwa wahindi, wachina, wazungu au waarabu ni nadra sana, watu wenye hizo asili kuwauza watu wa asili yao hasa kwa waafrika, kidogo muarabu kumuuza muarabu kwa mzungu lakini sio kwa mwafrika sema ni nadra, ila kwetu sisi ni kugusa tu.
Wasichotambua wanaojiita wahuni ni kwamba, kabla yao alikuwepo mobutu seseseko naye alijipendekeza sana kwa wazungu, pesa alikuwa anaiba congo ana hifadhi belgium na uswisi, alivyokufa tu mali ikawa ya wazungu, wahuni pia siamini kama pesa wanazoiba wanazihifadhi humu ndani, lazima wanazipeleka nje halafu wote tunaonekana hatuna maana watu weusi, kumbe ni malimbukeni wachache.
Hiyo ya kuhusu congo, kwamba wanatupiganisha wazungu, ni baada ya kutupima uwezo wetu wa kufikiri na kugundua ni mdogo, halafu tumekalia almasi, wanajiuliza kwanini tusichukue?