Lee Van free
JF-Expert Member
- Aug 14, 2024
- 2,685
- 8,349
Inasikitisha sana Kwa kweli kwa nchi ilipofikia.
Imekua nchi ya mfano kwa miaka mingi.
1) Ilikuwa nchi ya mfano kwa kupigania haki ya watu wengine duniani kote walikokua wanaonewa na watawala wa wa hovyo.
2) Sasa imekuwa nchi ya mfano wa mambo ya hovyohovyo na ya kijingajinga hapa duniani.
3) Sasa hivi kila kitu ni ujingaujinga tu.
- Uchaguzi ni wa kijingajinga TU
angalia chaguzi zote zinavyoendeshwa,mfano Oct2025
- Serikali ya ni ya kijingajinga TU
Angalia serikali inavyoendeshwa kuanzia matamko, hotuba na matendo ya Vyombo vya Dola.
Mfano mdogo TU,mtu anatangaza hakuna mikutano ya siasa,anakuja mwingine anaondoa katazo hilo.
Mmoja anasema tudai katiba mpya,wengine wanasema hatuhitaji katiba mpya.
Mmoja anasema nchini kuna magaidi,bila kujali athari.
Mwingine anasema hakuna magaidi
- BUNGE ni la kijingajinga TU
Bungeni huko ndio kama Kilabu Cha pombe za kienyeji,maisha ya huko ni mipasho TU. Mmoja anasimama bungeni anasema nchi hii Kuna Yuda Eskarioti, mwingine anasema hakuna Yuda
- Mahakama ni ya kijingajinga TU
MAHAKAMA kiasili ni sehemu takatifu, lkn hapa Sasa, ndio usiseme kabisa.
Dunia nzima inashangaa.
Majaji na wanasheria wa serikali wala hawajulikani wanataka Nini katika KESI za kisiasa.
Mwaka juzi Kuna mtu alishitakiwa kwa "ugaidi",alipotoka mahkamani akaenda ikulu kunya chai,kahawa na kashata na kupiga picha na wenyeji wa huko.
Mwaka huu Kuna mtu anashitakiwa peke yake kwa "uhaini"kutaka kupindua serikali.
Mipango ya kupindua aliifanya kwenye mkutano wa hadhara Tena kukiwa na waandishi wa habari, na nje Kuna polisi wakilinda mkutano.
Huyu mtuhumiwa ktk njama zake anatuhumiwa peke yake Hana Jeshi, wala kikundi Cha waasi.
Hana bunduki wala kisu.
IImefika wakati wananchi huko Nje ya nchi watakua wanaogopa kijitambulisha kama wao ni wananchi wa nchi hii.
Miaka kadhaa ijayo katika nchi nyingine watakua na vipindi mashuleni na vyuoni kusoma historia ya Taifa lililoongoza duniani kwa mambo ya kijingajinga.
Imekua nchi ya mfano kwa miaka mingi.
1) Ilikuwa nchi ya mfano kwa kupigania haki ya watu wengine duniani kote walikokua wanaonewa na watawala wa wa hovyo.
2) Sasa imekuwa nchi ya mfano wa mambo ya hovyohovyo na ya kijingajinga hapa duniani.
3) Sasa hivi kila kitu ni ujingaujinga tu.
- Uchaguzi ni wa kijingajinga TU
angalia chaguzi zote zinavyoendeshwa,mfano Oct2025
- Serikali ya ni ya kijingajinga TU
Angalia serikali inavyoendeshwa kuanzia matamko, hotuba na matendo ya Vyombo vya Dola.
Mfano mdogo TU,mtu anatangaza hakuna mikutano ya siasa,anakuja mwingine anaondoa katazo hilo.
Mmoja anasema tudai katiba mpya,wengine wanasema hatuhitaji katiba mpya.
Mmoja anasema nchini kuna magaidi,bila kujali athari.
Mwingine anasema hakuna magaidi
- BUNGE ni la kijingajinga TU
Bungeni huko ndio kama Kilabu Cha pombe za kienyeji,maisha ya huko ni mipasho TU. Mmoja anasimama bungeni anasema nchi hii Kuna Yuda Eskarioti, mwingine anasema hakuna Yuda
- Mahakama ni ya kijingajinga TU
MAHAKAMA kiasili ni sehemu takatifu, lkn hapa Sasa, ndio usiseme kabisa.
Dunia nzima inashangaa.
Majaji na wanasheria wa serikali wala hawajulikani wanataka Nini katika KESI za kisiasa.
Mwaka juzi Kuna mtu alishitakiwa kwa "ugaidi",alipotoka mahkamani akaenda ikulu kunya chai,kahawa na kashata na kupiga picha na wenyeji wa huko.
Mwaka huu Kuna mtu anashitakiwa peke yake kwa "uhaini"kutaka kupindua serikali.
Mipango ya kupindua aliifanya kwenye mkutano wa hadhara Tena kukiwa na waandishi wa habari, na nje Kuna polisi wakilinda mkutano.
Huyu mtuhumiwa ktk njama zake anatuhumiwa peke yake Hana Jeshi, wala kikundi Cha waasi.
Hana bunduki wala kisu.
IImefika wakati wananchi huko Nje ya nchi watakua wanaogopa kijitambulisha kama wao ni wananchi wa nchi hii.
Miaka kadhaa ijayo katika nchi nyingine watakua na vipindi mashuleni na vyuoni kusoma historia ya Taifa lililoongoza duniani kwa mambo ya kijingajinga.