Wahitimu wa vyuo waokolewe

Wahitimu wa vyuo waokolewe

Mmmmmmhmn unajua ukishapiga degree akili yako inakuwa kama imefungwa unashindwa kufanya maamuzi ya kufanya kazi zingine nje ya taaluma.

Hii kiukweli msiwalaumu hawa wahitimu wa chuo. Kusoma masomo miaka mitatu ni kuwa programed kiakili kufanya hilo jambo. Hivyo mtihani wa kufanya jambo jingine ni mgumu sana kwa hawa raia.....

Watu hawajiongezi kabisa, Mimi ni graduate lakini nafanya kazi aiendani na mm kabisa Lakini maisha yakenyooka sana, Vijana tunapenda sana uofisa, Akat watu tunatindua ukuta Zama Darini chimba sana mitaro Maisha ni elimu tosha
 
Kama serikali imeshajua haiwezi kuajiri wanaohitimu kwann tuna gamble na pesa zinazowekezwa kwenye elimu kwa kuwapa wanafunzi mikopo ya masomo kwanini tusiweke katika bajeti ya mikopo ya biashara ili basi watu wajiajiri sasa kama tunavyotaka.
 
Suluhisho la hili tatizo ni ajira za kudumu ziondolewe, mtu aajiriwe kwa miaka 5 tu, baada ya hapo wakajiajiri....nadhani ikiwa hivyo itatatua hii changamoto ya ukosefu wa ajira, pia uchumi utakwenda kwa kasi kwa sababu sekta binafsi zitakuwa nyingi zikiongozwa na wasomi.
 
Kwa miaka ya karibuni imekuwa ni kazi kumpata HOUSE GIRL kuliko mtu mwenye MASTERS au BACHELOR. Hii imetokana na ongezeko la idadi kubwa ya vijana wanaomaliza vyuo kila mwaka kutoka vyuo mbali mbali vya elimu ya juu.

Hii imesababisha sintofahamu kwa wazazi juu ya future za watoto wao ambao wako mashuleni na wale ambao wamemaliza vyuo tayari.

Jambo la kushangaza zaidi ni baadhi ya kada kuwa na watu wenye elimu ndogo wanaolipwa mishahara ambayo inafanya wasomi wa juu wadharauliwe, embu imagine msomi anendesha BODABODA alafu dereva wa VX la waziri ni form four tena failure, Mwanajeshi anadrive BIMA graduate anaendesha bajaji ya BOSS, na kada nyingine nyingi

Wito wangu kwa serikali ni kurekebisha mifumo ya utoaji ajira ambayo itawafavour GRADUATES

Graduates pia wanaweza kuwa Madereva, Askari, Wanajeshi, wasaidizi wa viongozi, n.k

Lakini pia ni muda sasa wa kupitisha sheria ambayo itawataka taasisi kubwa zote Tanzania kuwa na Internships angalau asilimia 10 ya waajiriwa wote katika Taasisi fulani wawe interns nadhani tutapunguza ugumu wa maisha kwa hawa Graduates wanatia huruma kwakweli.
Kuwa graduate sio kizio cha utajiri
 
kuna kipindi nilikua nataka watu (2) wakushusha mizigo ya duka katoro uko.

mimi si mwenyeji wa kule hivo niliandika tangazo tu hapo mbele ya duka.
walikuja watu 16 .
kwa bahati mbaya/nzuri ni watu 3 ndo walikua na elimu ya form 4 ila 12 wote walikua wamefika chuo degree na diploma.
wa 4 walikuja na cv kabisa niliumia sana .

mmoja alikua na cv nzito mno mno ilibidi nijaribu kuisambaza kwa rafiki zangu asee
 
Sijawahi kusikia daktari bingwa wa upasuaji anakosa kazi; namaanisha tusome vitu au fani ambayo si kila mtu anaweza kufanya
Hujui unachoongea..ungia chimbo fanya utafit kidogo..vijana kuanzia 2013 wa MD weng wako mtaan..wengne wameshakata tamaa hata kujiendeleza kuwa mabingwa wamekata tamaa...kuna kad nying tu ambazo si kila mtu anaweza tena za science na engeneering na bado watu wako mtaan...miaka hii mi5 imekua mibaya snaa kwa wasomi wetu
 
Baadhi ya wahitimu huwa na mawazo yafananayo na yafuatayo:

1. Ajira maana yake ni serikalini au sekta ya umma. Ukisikia wanasema, hakuna ajira, maana yake sikupata ajira serikalini.

2. Wengi wanatafuta ajira, hawatafuti kazi.

3. Kozi za ufundi sanifu huonekana ni dhalili kwao, mfano za VETA.

4. Wengine huko vyuoni hawako siriasi na masomo. Ukiwaona, huwezi kuamini wamechukua mkopo ili waje shule. Shule ni kama pikiniki fulani ya kujimwambafai kitaa kwamba na miye niko chuo!

5. Baadhi huenda vyuoni kutafuta vyeti tu na siyo ujuzi wala maarifa.

6. Ukiwaambia wachukue vyeti bila kusoma, baadhi watakuwa radhi kufanya hivyo.

7. Mtaji wa kujiajiri uko wapi? Ni kisingizio tu.


Majuzi niliwauliza vijana fulani kuhusu kujiajiri, nikajibiwa "Mtaji!?" Nikauliza unataka shilingi ngapi ili uweze kujiajiri, jibu kizungumkuti.
 
Baadhi ya wahitimu huwa na mawazo yafananayo na yafuatayo:

1. Ajira maana yake ni serikalini au sekta ya umma. Ukisikia wanasema, hakuna ajira, maana yake sikupata ajira serikalini.

2. Wengi wanatafuta ajira, hawatafuti kazi.

3. Kozi za ufundi sanifu huonekana ni dhalili kwao, mfano za VETA.

4. Wengine huko vyuoni hawako siriasi na masomo. Ukiwaona, huwezi kuamini wamechukua mkopo ili waje shule. Shule ni kama pikiniki fulani ya kujimwambafai kitaa kwamba na miye niko chuo!

5. Baadhi huenda vyuoni kutafuta vyeti tu na siyo ujuzi wala maarifa.

6. Ukiwaambia wachukue vyeti bila kusoma, baadhi watakuwa radhi kufanya hivyo.

7. Mtaji wa kujiajiri uko wapi? Ni kisingizio tu.


Majuzi niliwauliza vijana fulani kuhusu kujiajiri, nikajibiwa "Mtaji!?" Nikauliza unataka shilingi ngapi ili uweze kujiajiri, jibu kizungumkuti.
Uko sahihi, ukiuliza ndio ana cheti...je anaweza kufanya kitu gani kinachoonekana...hapo ni blablaa, nadhani tusome fani zinazotuachia ujuzi fulani wa kutengeneza kitu na kukiweka sokoni, tukiwa tunalalamika umri unaenda na utatuzi hakuna, njia sahihi ni kupambana wewe mwenyewe kwa kutafuta ujuzi sahihi, ata ukiajiriwa na ukaachishwa kazi,uwe na uwezo wa kutengeneza au kutoa huduma fulani (kujiajiri).
 
Umekosea san kucompare mtu aliesoma fani na mwingne alieenda kusomea vyeti kwahyo toa hako na ujinga kichwani pili kunywa maji utulie

Hlaf ujiulize utafanya nn October kwenye box la mpiga kura

Over
 
Kama serikali imeshajua haiwezi kuajiri wanaohitimu kwann tuna gamble na pesa zinazowekezwa kwenye elimu kwa kuwapa wanafunzi mikopo ya masomo kwanini tusiweke katika bajeti ya mikopo ya biashara ili basi watu wajiajiri sasa kama tunavyotaka.
Ndio shida ya serikali zisizojitambua.

Wanakinga maji kwenye kapu la ukindu.

Mradi tu jua limechomoza na kuzama basi tunachanja tu mbuga kama gari-moshi lenye hitilafu ya kiteknikali.
 
Suluhisho la hili tatizo ni ajira za kudumu ziondolewe, mtu aajiriwe kwa miaka 5 tu, baada ya hapo wakajiajiri....nadhani ikiwa hivyo itatatua hii changamoto ya ukosefu wa ajira, pia uchumi utakwenda kwa kasi kwa sababu sekta binafsi zitakuwa nyingi zikiongozwa na wasomi.
Hio ndio suluhu, ajira ziwe za mkataba ili watu wawe phased out! Ina maana baada ya miaka 5 intake ya waajiriwa inabadilika. Itasaidia walau watu watakuwa na uwezo wa kimtaji.

Kikubwa tu walipwe mishahara mizuri ili hata wakiondoka wawe na mitaji yao tayari.
 
Hii mada ni muhimu sana,na inasikitisha sana,nikisikia vijana wanaambiwa wakitoka vyuoni wakajiajiri,huwa napatwa hasira sana,
Hivi mnajua kwamba,mfano watu waliopo kwenye ajira kuanzia miaka 5,wakiambiwa sasa waache hizo ajira,wengine wachukue na wao waende kitaa "wakajiajiri"asilimia kubwa watachanganyikiwa,full msongo,
Sasa Kama Hawa wanaogopa,kwenda kitaa kujiajiri,maana wanaona Giza Totoro,sembuse madogo waliotoka vyuoni na masalia ya boom kiduchu!!!!!
Hapa serikali na wadau inabidi tuje na mkakati madhubuti wakuwapatia Hawa vijana ajira wanapohitimu,tuzalishe wahitimu wazuri hata tuwauze kwenye mataifa mengine kama India,na Nigeria zinavyofanya,USA,kumejaa ma IT,madokta,wahandisi kutoka,naija na India,mi nafikiri tuige wachina,Malaysia,Philippine,china sasa hv ipo dunia nzima inafanya miradi,
Ebu fikiri,tungekuwa na kandarasi,Rwanda,Burundi,Malawi,Congo,na zote zinaajiri vijana kutoka hapa hm,
Tutafute bidhaa moja,tuiuze dunia nzima,
Kama Samsung kwa Korea,au Tecno kwa mchina,
Hapo umezungumza bonge la point....... Yaani kwa mfano hao wanaosema tujiajiri balaa lake hawalijui. Kujiajiri ni safari ya kurudisha akili yako the day kabla haujaenda shule ili ujiulize unaweza fanya nini na vipawa na vipaji vyako......

Sio jambo dogo kudadadeki.....

Tunachojua kuexport sisi ni pembe za ndovu na madini plus mawe ya almasi na tanzanite.

Vitu vingine ni chenga tupu.......
 
Watu hawajiongezi kabisa, Mimi ni graduate lakini nafanya kazi aiendani na mm kabisa Lakini maisha yakenyooka sana, Vijana tunapenda sana uofisa, Akat watu tunatindua ukuta Zama Darini chimba sana mitaro Maisha ni elimu tosha
Kumbuka hao watu wamekuwa trained kuwa maofisa na ndio maana wanabehave hivyo.....

Unapokuwa trained kama mtu wa aina fulani unategemewa kufanya majukumu ya huyo mtu.....

Huwezi ukasomea degree ya u daktari halafu uje kuwa mkulima au mhasibu. Hiyo ni kupoteza muda na pesa.

Kama tunajua watu wakisoma hawaajiriki then kwann tusiamue tu kusitisha hizo trainings za wasomi wa vyuoni tutumie hiyo pesa kufanyia mitaji ya biashara maana pesa ya miaka mitatu ya tuition fee plus accommodation ni pesa mingi sana.....
 
Back
Top Bottom