Wagombea wa Urais 2015...

Wagombea wa Urais 2015...

Nimejiuliza sana hii spidi na utitiri wa watangaza nia ya urais kila kukicha list inaongezeka kwa kasi ya ajabu, je ni kweli wote wana nia ya kugombea ama kuna mbinu wanaitumia ili kumpata mmoja katika makundi yao mbalimbali? Watangaza nia hao ambao ni makada wa CCM ambao baadhi yao walipewa karipio kali na adhabu ya kutojihusisha na kampeni kabla ya wakati nao wameendelea na harakati hizo.

Spidi hiyo imewaibua hadi akina Kigwangwala nao wamo kwenye list ya utitiri huo!
Hizi ni mbwembwe tu au wamedhamiria kugombea?
kuna mtu mmoja nimemsahahu jina lake alisema kwamba ccm ni kama kambale kila mmoja ana sharubu sasa unashindwa kuelewa ni nani kiongozi au mkubwa wa ukoo
 
Kama wanaona mwenzao aliyeko madakani uwezo wake ni mdogo kuliko wao kwanini wasijitokeze,mimi nasubiri waniletee mmoja wa kupambana na wenzie wa vyama vingine ili nichague yule anaenifaa.
 
mleta mada mnaweza mkamshangaa lakini alichotabiri kina asilimia kubwa sana kutokea, dr slaa hakuna wa kumzuia asigombee na ndio chaguo la wananchi walio wengi kwa sasa (hata baadhi ya maeneo ya nchi anapokewa kama raisi na wenyeji mfano mbeya, mwanza, arusha), lowasa bado ana mtandao tihifu kwake na wenye nguvu za kimahamuzi na pesa (wafanyabiashara) ndani ya ccm, prof lipumba kule cuf bado kuna usultani, ufalme, uchifu, hakuna mtu wa kumpinga.
this is true
 
nimejiuliza sana hii spidi na utitiri wa watangaza nia ya urais kila kukicha list inaongezeka kwa kasi ya ajabu, je ni kweli wote wana nia ya kugombea ama kuna mbinu wanaitumia ili kumpata mmoja katika makundi yao mbalimbali? Watangaza nia hao ambao ni makada wa ccm ambao baadhi yao walipewa karipio kali na adhabu ya kutojihusisha na kampeni kabla ya wakati nao wameendelea na harakati hizo.

Spidi hiyo imewaibua hadi akina kigwangwala nao wamo kwenye list ya utitiri huo!
Hizi ni mbwembwe tu au wamedhamiria kugombea?
hizi ni propaganda za ccm kutaka kututoa kwenye swala la msingi kuhusu katiba mpya ya wananchi
ili kupunguza idadi ya wananchi kuwa na uelewa wakutosha kuhusu katiba mpya ya wananchi
 
Sasa angalia majimbo anayopokewa SLAA kwa wingi kwa mtazamo wako, subiri kinyume chake hiyo 2015, SLAA atalia vizuri sana kuliko alivyomlilia mtu ambaye chama chake ni chanzo cha kifo chake. Hivi kwanza MBOWE anajisikiaje kuwekwa kando na urais wa 2015? acheni kugombanisha watu jamani vibaya hivyo. Huyu ZITTO tuachane naye kisha washinda. Mnataka tena bifu ianze kati ya SLAA na MBOWE, yaani mnamfanya Mwenyekiti anakuwa kama mti wa kutupia jongoo.
shughuri unayofanya ni shughuri ya iblis (UCHONGANISHI)
 
Sio utabiri,ni maono. Hawa watatu ndio watakaokuwa Wagombea wa Urais wa Tanzania wenye nguvu 2015. Makwarukwaru ya kila aina yatapita vyamani mwao. Wao ndio watakaogombea. Ni hawa: 1. Dr. Wilbrod Peter Slaa- CHADEMA 2. Edward Ngoyai Lowassa-CCM 3. Prof. Ibrahim Haruna Lipumba-CUF. Ni vyema tukajielekeza kwao na kuandaa kura zetu za Oktoba 2015. Ndivyo itakavyokuwa...

Hivi CCM wanachomtakia EL ni nini? Mpunga anaowahonga? CCM lazima wamchague mtu ambaye atawachukulia hatua BMK na JK kwa uhujumu wa uchumi.
 
Hao ndio mmoja wapo atakuwa raisi.watanzania tusichanganywe na makundi ya watu wanao tajwa tajwa hiyo kutuzubaisha watanzania ili tushindwe kuwafuatilia udhaifu wao .

x.Dr.Slaa kutokana na kuwa bado na mvuto kwa watanzania kwani tayari anao mtaji wa kura wa 2,272,634 ambazo alizipata mwaka 2010 .Tofauti na wenzake ambapo kura za kikwete zitabakia kuwa za kikwete na wala hazitakuwa za Membe wala Lowasa .Wao itabidi watumie busara kushawishi wapiga kura.

Changamoto ambazo Slaa atakuta nazo kama atapita itambidi kuteua waziri mkuu toka wabunge wa ccm kwani kutokana katiba ya 1977 na hii mpya inayojadiliwa kuwa na vipengere vinavyo tamka kwamba waziri mkuu atachaguliwa kutoka chama chenye wabunge wengi ,psrq

Watanzania tuanze kuwapima hao mapema kama wanatosha au hawatoshi kwa kuangalia vigezo vya uadilifu,uwajibikaji na kuvumiliana.

Karibuni .
 
Tujadiliane bila ya kuchafuana ,kama mtu unamwona sio mwadilifu au ni mwadilifu wewe weka facts.
 
lowasa mwizi leo ukataka awe rais utakuwa na kichaa wewe, hivi record ya membe nii ipi mpaka nae tumfikukie kuwa rais...rais ni Dr Slaa tu. .
 
Hao ndio mmoja wapo atakuwa raisi.watanzania tusichanganywe na makundi ya watu wanao tajwa tajwa hiyo kutuzubaisha watanzania ili tushindwe kuwafuatilia udhaifu wao .

x.Dr.Slaa kutokana na kuwa bado na mvuto kwa watanzania kwani tayari anao mtaji wa kura wa 2,272,634 ambazo alizipata mwaka 2010 .Tofauti na wenzake ambapo kura za kikwete zitabakia kuwa za kikwete na wala hazitakuwa za Membe wala Lowasa .Wao itabidi watumie busara kushawishi wapiga kura.

Changamoto ambazo Slaa atakuta nazo kama atapita itambidi kuteua waziri mkuu toka wabunge wa ccm kwani kutokana katiba ya 1977 na hii mpya inayojadiliwa kuwa na vipengere vinavyo tamka kwamba waziri mkuu atachaguliwa kutoka chama chenye wabunge wengi ,psrq

Watanzania tuanze kuwapima hao mapema kama wanatosha au hawatoshi kwa kuangalia vigezo vya uadilifu,uwajibikaji na kuvumiliana.

Karibuni .

Edward Lowassa na Benard Membe wana SLIM chance ya majina yao kupenya kwenye CHUJIO la kamati kuu ya CCM
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom