Edwin Mtei
Senior Member
- Dec 13, 2008
- 181
- 342
Nchi yetu imekuwa na Mipango ya Taifa ya muda Mrefu ambayo imekubalika kwamba itatekelezwa. Kila mwaka wa fedha mipango hiyo hutengewa fedha kutegemea na jinsi mapato ya taifa yanavyogawanywa.
Mifano ni barabara. Makubaliano hata na nchi jirani yanataja kwamba barabara itajengwa toka Dodoma kwenda kusini kuunganisha na ile barabara inayotoka Dar es Salaam kwenda Zambia. Barabara itajengwa pia toka Dodoma kupitia Kondoa mpaka Arusha ili kuunganisha na iendayo Kenya. Kwa mtindo huo kuna mipango ya Reli kupitia Arusha mpaka Musoma ili Uganda waweze kutumia bandari ya Tanga. Pia kutakuwa na barabara na Reli kwenda Burundi na Rwanda. Vivyo hivyo kuhusu viwanja vya ndege au bandari.
Kama katika Mpango wetu wa muda mrefu (Long-term Plan) kuna miundombinu itakayotekelezwa. mgombea u-Rais asianze kuitaja kwamba eti chama chake kikipata ridhaa ya wananchi kitaitekeleza. Hakuna chama cha siasa kitakachofuta Mipango ya Muda Mrefu kuhusu miundombinu, huduma za kijamii au kiuchumi. Bandari, madaraja na vivuko pale ambapo vinahitajika vitajengwa na Serikali yoyote ile.
Vyama vya siasa vijikite katika kueleza mikakati yao ya kupata nyenzo ( pamoja na kuzuia ubadhirifu wa mali ya umma) ili kutekeleza hiyo mipango. Mobilization of resources, including human resources and technology) ili kuleta maendeleo viwe ndio themes za kutofautisha vyama vya siasa.
Mifano ni barabara. Makubaliano hata na nchi jirani yanataja kwamba barabara itajengwa toka Dodoma kwenda kusini kuunganisha na ile barabara inayotoka Dar es Salaam kwenda Zambia. Barabara itajengwa pia toka Dodoma kupitia Kondoa mpaka Arusha ili kuunganisha na iendayo Kenya. Kwa mtindo huo kuna mipango ya Reli kupitia Arusha mpaka Musoma ili Uganda waweze kutumia bandari ya Tanga. Pia kutakuwa na barabara na Reli kwenda Burundi na Rwanda. Vivyo hivyo kuhusu viwanja vya ndege au bandari.
Kama katika Mpango wetu wa muda mrefu (Long-term Plan) kuna miundombinu itakayotekelezwa. mgombea u-Rais asianze kuitaja kwamba eti chama chake kikipata ridhaa ya wananchi kitaitekeleza. Hakuna chama cha siasa kitakachofuta Mipango ya Muda Mrefu kuhusu miundombinu, huduma za kijamii au kiuchumi. Bandari, madaraja na vivuko pale ambapo vinahitajika vitajengwa na Serikali yoyote ile.
Vyama vya siasa vijikite katika kueleza mikakati yao ya kupata nyenzo ( pamoja na kuzuia ubadhirifu wa mali ya umma) ili kutekeleza hiyo mipango. Mobilization of resources, including human resources and technology) ili kuleta maendeleo viwe ndio themes za kutofautisha vyama vya siasa.