Wadau, ni sahihi kumpa talaka mke mjamzito?

Wadau, ni sahihi kumpa talaka mke mjamzito?

NIMEONA

JF-Expert Member
Joined
Aug 4, 2019
Posts
3,854
Reaction score
5,714
Habarini wadau!

Moja kwa moja kwenye mada kama ilivyo hapo juu;

Mume akihisi imelazimu kutalikiana na mke ambaye ni mjamzito, utaratibu ukoje (ukiwa una ujuzi wa maarifa ya kidini ya Kiislamu itapendeza zaidi)

Ahsanteni!

Korona ipo, tufanye alichoagiza mheshimiwa Raisi!
 
Sheria ya dini ipo hiviii
1.Huruhusiwi kumuowa mwanamke akiwa mjamzito had pale atakapo jifungua ndipo unaruhusiwa kumuowa.

2. Kumpa talaka akiwa na mimba unaweza ila unatakiwa uwajibike kutoa matumizi kwakua kile kiumbe kilichopo tumbon ni damu yako
KUBWA ZAIDI
Talaka ni halali ila inamchukiza sana Mwenyezi Mungu hivyo jaribu kutafuta suluhu au watu wenye elimu ya din wakupe elimu zaidi juu ya talaka ni somo ambalo unatakiwa ukae chin, kwasababu unaweza kufikiri umeacha kumbe bado kisheria hujaacha, au unaweza kufikiri hujaacha kumbe kisheria umeacha.


Sent using GunTrigger
 
Huna lolote unaogopa majukumu ya malezi ya kijacho wewe😏, ila usimwache bana hizo changamoto huenda ni kwa kipindi hiki cha ujauzito tu akijifungua atakua sawa.
ahsante, hata siogopi malezi lakini🤣🤣🤣🤣
 
Sheria ya dini ipo hiviii
1.Huruhusiwi kumuowa mwanamke akiwa mjamzito had pale atakapo jifungua ndipo unaruhusiwa kumuowa.

2. Kumpa talaka akiwa na mimba unaweza ila unatakiwa uwajibike kutoa matumizi kwakua kile kiumbe kilichopo tumbon ni damu yako
KUBWA ZAIDI
Talaka ni halali ila inamchukiza sana Mwenyezi Mungu hivyo jaribu kutafuta suluhu au watu wenye elimu ya din wakupe elimu zaidi juu ya talaka ni somo ambalo unatakiwa ukae chin, kwasababu unaweza kufikiri umeacha kumbe bado kisheria hujaacha, au unaweza kufikiri hujaacha kumbe kisheria umeacha.


Sent using GunTrigger
shukrani sana sana!! ndoa zinachangamoto sana wakati mwingine......sana!
 
Usitoe kwa sasa utatengeneza chuki kwa kiumbe kilichopo tumboni
 
shukrani sana sana!! ndoa zinachangamoto sana wakati mwingine......sana!
ikishindikana suluhu utoaji wa talaka 3 unataratibu zake pia mkuu kwahiyo nakushauri utafute mtu mwenye elim kdogo akueleweshe jins ya kuzitoa huwa hazitolewi kwa mara moja

Hivyo taufta mtu akupe elim hapa utaweza kukutana na upotoshaji kweny jambo zito

Sent using GunTrigger
 
KWELI MWENZETU YAMEKUKUTA,UNADIRIKI KUMPA TARAKA MJAMZITO TENA WAKATI HUU WA MAJANGA YA CORONA
hilo la corona si dogo, halafu tena mtu mwingine akuletee janga lingine!
 
ikishindikana suluhu utoaji wa talaka 3 unataratibu zake pia mkuu kwahiyo nakushauri utafute mtu mwenye elim kdogo akueleweshe jins ya kuzitoa huwa hazitolewi kwa mara moja

Hivyo taufta mtu akupe elim hapa utaweza kukutana na upotoshaji kweny jambo zito

Sent using GunTrigger
👏👏👏
 
ahsante, hata siogopi malezi lakini🤣🤣🤣🤣
unachoogopa kutoa Talaka ni nini? (kuna story nimeiona jana kwenye TV jamaa kawa kipofu halafu mke kawa kiburi mpaka kaenda kwao) akirudi na Mimba je
sasa mtu hulali naye huenda Dr kakwambia huwezi yeye kaja na Mimba ya unayemjua vile wanakusaidia
sizungumzii Dini, ila uhalisia km una uhakika mimba si yako na hujahusika p/se mpe haraka usije lea kiumbe si damu yako
 
Kwa uelewa wangu..
Dini ya kiislam hairuhusu talaka kwa mjamzito


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
habarini wadau!

moja kwa moja kwenye mada kama ilivyo hapo juu;
mume akihisi imelazimu kutalikiana na mke ambaye ni mjamzito, utaratibu ukoje (ukiwa una ujuzi wa maarifa ya kidini ya Kiislamu itapendeza zaidi)!

ahsanteni!
korona ipo, tufanye alichoagiza mheshimiwa Raisi!
Huo ni ukatili kiongozi, kwanini usimsubiri hadi ajifungue ndipo uchukue hayo maamuzi ya kibinafsi
 
unachoogopa kutoa Talaka ni nini? (kuna story nimeiona jana kwenye TV jamaa kawa kipofu halafu mke kawa kiburi mpaka kaenda kwao) akirudi na Mimba je
sasa mtu hulali naye huenda Dr kakwambia huwezi yeye kaja na Mimba ya unayemjua vile wanakusaidia
sizungumzii Dini, ila uhalisia km una uhakika mimba si yako na hujahusika p/se mpe haraka usije lea kiumbe si damu yako
yaani hakuna cha maana kinachojadilika ndani, hata salamu inageuka kuwa ugomvi.

mfano, unaweza kurudi kutoka mizunguko saa mbili usiku na kumkuta akipika. unamuuliza kiuungwana tu 'mbona unapika saa hizi kulikuwa na tatizo?'. anajibu 'nilikuwa nacheza tu'! tena anajibu kidharau huku mdomo ameupeleka pembeni.

ukijisahau kidogo kuacha kihela cha matumizi, huyo anatia timu kazini (maana kazini kwenyewe ni karibu tu na nyumbani)
 
Back
Top Bottom