Wadaiwa mikopo tuishitaki HESLB

Wadaiwa mikopo tuishitaki HESLB

Hiyo paragraph ya mwisho No3 Magufuli hakupi msaada wowote...never ever,yeye ndiye aliyewakurupusha hao jamaa waongeze riba kwa kiwango hiko ili kufidia mapengo ya makusanyo.unapomuona kwenye hotuba zake akijigamba hadhrani kwamba hatakopa popote hali biashara mijini zikizidi kuwa mbaya huku nyengine zikifungwa jua tunaokamuliwa ni sisi wananchi ili kujazia hiko kilichopungua.na kila mmoja ana aina yake ya ulipaji!
Ha ha ha eti kila mmoja ana aina yake ya ulipaji!! Duuh

Kweli aisee ITV, STARTV, CHANNEL TEN, CLOUDS TV, EATV, nk tuna lipa nao...

Sasa sijui wanyonge anao kuwa ana maanisha ni wapi?
 
Mi niliambiwa ni scholarship na hata huko nilipokua nasoma niliwekwa kwenye Kundi la Tanzania Government scholarship.
Nimepewa statement board ya mikopo Ina hela ya research na vitu kibao ambavyo sijawahi Fanya. Wananidai million 80.
Duuh
 
Wapuuzi kweli hawa bodi, miaka ya nyuma kabla ya kuanzisha bodi hizo pesa zilikuwa zinatolewa na wafadhili kuwezesha utoaji wa elimu ya juu kwenye state universities.

Inakuwaje bodi waje wadai pesa ambayo ilikuwa ni msaada kwa serikali kuwezesha utoaji wa elimu ya juu nchini. Pia, inakuwaje bodi iwadai watu wanaosoma kwenye vyuo vikuu vya umma kiasi kinachofika hadi milioni ishirini sawa na wale wanaosoma kwenye vyuo vikuu vya binafsi.

Hii imesababisha hata kushusha ushindani wa wanafunzi kushindania nafasi kwenye vyuo vikuu vya umma kama UDSM and SUA kwani hakuna unafuu wowote kati ya mtu aliyesoma state universities na hivyo vyuo vya binafsi vilivyoanzishwa kama uyoga.
 
Umewaza mbali rafiki, tatizo ni mfumo wa nchi yetu na current regime! No one will listen to you. Lipa tu ndugu, daima majani manyonge humbeba tembo!!!
 
siku 70%ya watu wanaolipa wakimaliza deni lao bodi ya mikopo itasambalatika kwani wameongeza 15% ili wapate nyingi kipindi hicho wanaomaliza vyuo hawana ajira.
 
Kuna tabia mbaya Watanzania tunafikiri mkopo ni Ruzuku! Mkopo lazima ulipwe na wengi ambao wakimaliza vyuo wanagangamala kutolipa walikuwa wanaandamana ili wapate MKOPO na mkopo lazima urejeshwe. Tusisahau huwezi kutajirika bila kukopa lakini mkopo lazima urejeshwe
Kumbuka kuna kitu kilikuwa kinaitwa meals & accommodation allowance je allowance inarudishwa? Alaf mtoa mada ameongelea kuhusu kupandishwa kwa % ya kurejeshwa mkopo je wadau walishirikishwa? Vp kuhusu interest rate pamoja na retantion fee waliambiwa kabla?
 
Mimi hawa Loan board nimewazilia mshahara wakate mpaka waache kuaashwa 1: wenzangu tuliokuwa grade sawa (40%) na cozi sawa wanadaiwa ,mimi nimeandikiwa 21m nimeenda mara nyingi dar kurekebisha wananiahidi tayari wamerekebisha lkn bado deni liko palepale.SITOKUJA KUWA MZALENDO KATIKA HII NCHI HADI NAIMGIA KABULINI NIKIPATA UPENYO NIKUINYOOSHA SERIKALI TU KWA KUIIBIA NO WAY OUT!!!!
Kabisa wanadai 21m???

Tchaaaa
 
wananidai 4.5m, nilisoma kwa miaka 4. namaliza kulipa 2022 mshahara ukibaki ulivyo.
kwangu walijichanganya ila tuko pamoja mkuu
 
Kuna Dada alisomea nje had sasa anadaiwa ka million 70 hv....aisee huko mbeleni ndoa zote lazima tuhakukiane ka hauna mkopo wa bodi
Mimi 45 lakini mi nimekubali wakaniuze utumwani libya Sina pesa ya kuwalipa
 
Lipeni hela hizo nyie na wadogo zenu wasome.....khaa!!
 
Mi natamani kweli kulipa mkopo wao ila ajira sina ntalipa na nini? Hapo hapo wameniwekea tena riba.
 
Hivi kuna watu mpaka leo hii mnalipa hii mikopo? Mnafuatwa nyumbani au kazini? Mbona mi sijawahi kuwaza kuhusu hiyo? Tulieni mle bata
watu tunakatwa 15% kwenye salary zetu af we unahoji utumbo gani huo!!??
 
Mi niliambiwa ni scholarship na hata huko nilipokua nasoma niliwekwa kwenye Kundi la Tanzania Government scholarship.
Nimepewa statement board ya mikopo Ina hela ya research na vitu kibao ambavyo sijawahi Fanya. Wananidai million 80.
Daaah!!
 
Back
Top Bottom