Comparison is the thief of Joy....maisha ya kujilinganisha na fulani ndo maana wanakuwa na visirani....na wanatoa nafasi ya watu kuwaumiza kwa masengenyo....wanasema kill them with happiness. lakini wakiendelea kuwa watu wa kulalamika,wanyonge na kuona kama kutokuolewa ni aina fulani ya ulemavu au laana na kuwa desperate wataishi kwa taabu sana.
Ukweli utabaki kuwa kuna vitu haviko ndani ya uwezo wako,huwezi lazimisha mtu akuoe au aone unafaa kuwa mke,ukifanya hivyo una utumwa wa maisha,kufurahisha dunia kumbe ndani unaungua..kaa karibu na Mungu wako na mwambie mapenzi yako yatimizwe,unipe furaha kwa lile ninalodhani nalihitaji ila hujanijibu kwa kuwa sababu waijua wewe.
Usijiulize nilipanga? kwa ufupi ni machache sana unayopanga,hukupanga kuzaliwa,kuwa mwanamke,kuwa na elimu uliyonayo,kuwa na mafanikio uliyonayo au hata mapungufu....acha kupoteza muda na maswali usiyoweza pata majibu mazuri, labda ujiulize mienendo yangu na tabia zangu zinawavuta watu sahihi kwangu?
Ukimaliza muombe Mungu na urekebishe pale inapobidi the rest muachie Muumba wako aliyekujua hata kabla ya kutungwa tumboni kwa mama yako.
Last but not least....bado unaishi...subira na moyo wa shukrani kwa mazuri uliyonayo itakupa amani. Usiishi kuhesabu uliyokosa tu,tizama Mungu aliyokupa.