Wachina kuvamia usafirishaji ni Halali?

Wachina kuvamia usafirishaji ni Halali?

Wachina wanajua kula na wenye Nchi. Kuna mmoja mwenye malori yadi yake ipo lugalo jeshini. Sijui kama kuna mtanzania anaweza ruhusiwa hata kilometer 1 karibu na kambi ya jeshi la china.
 
wacha wachina waje ili wachangamshe wabongo coz hukisoma histolia ya marekani utaona wachina wamejenga reli sana kule na kunawachina wengi sana marekani wanafanya biashara mpaka leo na jua biashara ni ushindani mzee.
vijana watanzania hawana ajiri wanangaika sana siku izi wewe unakataa wachina wasifungue makampuni unafikili hutawajir ww?,wacha waje wengi wafungue makampuni vijana wapate ajira,nabado watakuja kila sekta bado kujenga nyuma za kuuza na kupangisha hapo ndio wabongo watalia sana.
 
uchumi wa nchi unayumba kila kitu kimeshafeli wachina utasikia hata wanachoma mahindi kariakoo usishangae.
kama wabongo wameshindwa kuchoma mahindi kariakoo wanaona aibu wataonekana masikini mbele za mademu zao, kwanini mchina asichome ili tununue? nyie endeleeni kuchagua kazi na kujifanya masharobaro kumbe mifukoni hamna kitu.
 
Ndg zangu naombeni kuhoji kupitia jamvi hili ili na nyie mnisaidie

Mimi ni mdau wa biashara ya usafirishaji kwa njia ya barabara.

Tumevamiwa na tena tunakandamizwa hatupumui hata kidogo na hawa wawekezaji wapya WACHINA.

Nikizungumzia mabasi, leo hii kuna wachina wanapeleka mabasi route zote kutoka Dar. Na wako radhi kupakia abiria kwa bei wanayopenda wao, na kuondoa gari na abiria hata watano.

Ikumbukwe hao wachina ndio mawakala wa mabasi ya Yutong na Zhongton ambayo yako kwenye chart sasa.

Je isingekuwa vyema kwa hawa wachina kuwa restricted kwenye kutuuzia tu mabasi na sisi tufanye biashara ya usafiri?

Kumbuka mchina mmoja ana mabasi zaidi ya 150.
Wale watanzania tunaojenga uwezo na vibasi vyetu viwili, vinne hadi kumi je tuta-survive?

Kwa uelewa wa kawaida pale ubungo kwa siku yanatoka mabasi yasiyopungua 200. Katika hayo wamiliki ni zaidi ya 100. Maana yake ni kwamba uchumi umesambaa mikononi mwetu wenyewe. Je tukimwacha mchina atoe mabasi 50 peke yake akaja ma mchina mwingine tena, wamiliki watanzania tutapona? Mbaya zaidi ni kuwa mchina anaweza kuweka basi mpya kila mwezi, sisi tunaweza?

Kwa wale msiofahamu, wachina wanauza mabasi ambayo wameshatumia yenye namba B na C yote kwa bei punguzo. Na mimi nimenunua hapo kadhaa. Lengo lao ni kuhakikisha wanaendesha mapya kila wakati na sisi yetu yanaendeshwa miaka mitano. Ndiyo uwezo wetu kitanzania.

Hawa wenzetu wana access to capital huko kwao. Sisi kama yatima tunapambana tangu mavumbini hadi tulipopata cent ya kununua kamoja. Je ni halali kutufutilia mbali kwa namna hii?

Hii sera yetu ikoje? Serikali iko wapi? Mbona mnatufanya kitu mbaya hivi?

Kwenye Malori hali ndiyo mbaya zaidi. Inaogopesha mno. Kuna kampuni 4 za wachina kila moja ina zaidi ya malori 400. Wanaenda mipaka yote ya nchi kwa bei punguzo.
Halafu hao hao wachina wamenunua kampuni za clearing. Kwa hiyo wanatoa mizigo wenyewe na wanagawana wenyewe. Ukifanya sensa ya watanzania wenye gari moja hadi 20 ni wengi mno tumetapakaa nchi nzima na uchumi unasambaa. Je huyu mchina akichuma hapa anatuachia nini sisi wa matombo, ileje,masasi,na kwingineko nchini? Kodi zenyewe hawalipi wanaingiza magari kwa msamaha wa kodi. Huu usingizi wa serikali utaisha lini jamani???

Ziko bank za kitanzania nazifahamu zimekopesha wachina malori yasiyohesabika. Leo hii wewe mtanzania ukitaka moja process itachukua miezi sita na unakata tamaa hata hulipati.... ! Agha! Basi bana siendelei .... 😡

kwa nini wenye mabasi mnafikiria matumbo yenu tu,haujiulizi unafuu wa nauli na usafiri wa raha utakaopatikana kwetu wasafiri wa kigoma tabora mza nk?
 
Kwa taarifa yako 95% ya mabasi yanayopiga mweleka ni scania, na matairi yanayoongoza kupasuka ni michelin na bridgestone ambayo hayatengenezwi china.

Unazungumzia Scania lorry zilizovishwa body ya bus
 
Wachina wanajua kula na wenye Nchi. Kuna mmoja mwenye malori yadi yake ipo lugalo jeshini. Sijui kama kuna mtanzania anaweza ruhusiwa hata kilometer 1 karibu na kambi ya jeshi la china.
tatizo wabongo wengi hawaaminiki, hata mimi akija mchina na mbongo kwangu nitampa priority mchina kwasababu ninajua hatutasumbuana kuaiana hela ambayo ni haki yangu, mnalipana kimkataba fresh, mbongo aanze kuleta undugu hapa na kupiga kiswahili, wanini? hata wewe ukijenga uaminifu unaweza kuweka malori yako hata magogoni. uaminifu ni mtaji hasa kwenye mambo ya pesa. wabongo wengi ukiawadhamini aisee wanakuachia lubega unaanza kuhangaika nalo.ndio maana hujapeleka malori yako pale.
 
Na kweli hatushindwi ! Lakini hatujafikia hapo na wala hatuwaxhukii watanzania kwa kiwango hicho!

Ila najiuliza, hivi nyie mnaosupport wachina ni watanzania Kweli?

Ah wapi, hamuwazidi ujanja hao watu, sisifu uchawi wala siufagilii ila ni noma kuliko watz. Ukiniambia mtawafanyia maombi naweza kukukubalia, lakini si ujanja mwingine, wanawazidi bana
 
Ndgu ushindani ndio biashara yenyewe na hakuna anayeogopa, tatizo hakuna fair ground btn foreign na local investors wao wanapata some exemptions ambazo mswahili utabaki kuzisikia tu! na hiyo ya kupanda nauli december sio kosa letu wasomi mnasema high demand lead to increase in price sasa tatizo la mfanyabiashara liko wapi hapo?

Kuongezeka kwa nauli ni high demand sio kosa la mfanyabiashara ila kushuka kwa nauli ni kosa la serikali?!!

Mkuu tusaidie msamaha gani wachina wanapata na nyinyi mnalipa hio kodi! Hivi hamna sheria kuwa mwekezaji lazima awe na mzawa kwenye shares?! Huko kwa wachina hamna ndugu zetu kweli?!
 
Mlishawahi kufikiria kuondoa hiyo hali ? Kwa sababu hao ndo wanapandisha bei ili wapate cha kwao !! Udalali kialsehemu, eti mtu ukienda kununua matunda Buguruni unauziwa na dalali ilhali mwenye machungwa kasimama hapo hapo, ukienda Karume kumnunulia mtoto viatu vya shule ndo utakoma zaidi, mwenye kuuza viatu yupo, lakini nakuachia unapigwa bei na dalali !!!! Yaani nyie, acha tu muendelee kukaribisha udalali kwa kila kitu. Kwani ukinunu gari, ufungue ofisi na kuwaajiri watu mwnyewe na usitoe ticket zako kwa mtu mwingine huwezi kupakia ? Naomba ufafanuzi kwa kuwa fani yangu sio hiyo.

Mkuu tuanze na hilo la udalali sokoni, nimewahi kuhusika na study iliyonipitisha kwenye hayo masoko.

Hakuna mkulima yeyote anayeweza kuuza bila dalali. Wameshikilia kuanzia mfumo wa uongozi mpaka upangaji wa bei.

The same na mabasi, hawa wamiliki wa basi moja hawezi kupata abiria bila dalali. Ukiweka dalali hapa Dar likienda mikoani litakutana nao, na akifanya mchezo hata huko wanaweza kumwekea kauzibe. Wana network yao. Na hapa ndipo serikali inapaswa kuingia ili kudhibiti hali.

Hata hao wachina hawatumii ofisi zao tu kukatia ticket, wanatumia pia agents.

Anachoelezea mleta thread ni kuwa pawepo na fair ground na kanuni zinazomlinda mzawa, ingawa nao wanapaswa kuboresha biashara yao.
 
Hayo mabasi yetu mnayoyaita ngarangara Mengi( 90%) ni Scania 94. Zimetengenezewa body na na Say Dar coach. Ubora wa kutosha miaka 5 na zaidi

Hizo ngarangara zenu, siti zake ndogo na zimebanana, ziko fixed hauwezi kuadjust, ukifika mwisho wa safari duuu, ni kama ulikuwa unaendesha baiskeli ya Anita. Zile siti ziko kama EXCUTION CHAIR, na madirisha kufungua au kufunga mpaka muwe wanaume wawili! Mi nitapanda basi lenye ubora hata kama anamiliki SHETANI.
 
Acha kulaumu benki ....watanzania wengi wakikopeshwa mwezi wa kwanza tu wanaharibu! Hao wahindi,waarabu wanakopa wanalipa! Na benki zinawaomba wakope! Ifikie kipindi tujiangalie matatizo yetu na sio kila siku kutoa lawama zisizo na kichwa wala miguu! Benki haiangalii rangi inaangalia biashara watz wazawa wengi wakikopeshwa wanaharibu!
Zaidi ni msukumo wa chuki na wivu kwa ma bankers dhidi ya
wasio wasomi lakini wamefanikiwa.watasumbuliwa sana.
Banker kamaliza chuo lakini kwa mwezi anapata hela ambayo
mtu si msomi anaipata kwa siku.Siku akitaka mkopo ataona rangi
7 za ulimwengu.
 
Hizo ngarangara zenu, siti zake ndogo na zimebanana, ziko fixed hauwezi kuadjust, ukifika mwisho wa safari duuu, ni kama ulikuwa unaendesha baiskeli ya Anita. Zile siti ziko kama EXCUTION CHAIR, na madirisha kufungua au kufunga mpaka muwe wanaume wawili! Mi nitapanda basi lenye ubora hata kama anamiliki SHETANI.

Umenifanya nicheke sana
 
Hatimaye wafanya biashara wamekuja bongo they mean "STRICTLY BUSINESS" by the way Mkuu naomba nsaidie kutaja majina ya hizo kampuni niwe ata napata usingizi safarini nimechoka kusafiri roho mkononi
 
hivi wakati ule ninyi mnapopandisha nauli wakati wa xmass huwa mnafikiria wagonjwa, watu wanaosafiri kwenda kuona wagonjwa, misiba na mwingien kakopa nauli? huwa mnakuwa wazalendo kweli, nini huwa mnakuwa watz? hakuna watu wabaya kama TABOA hao wamiliki, kwanza mnawanyonya sana madereva wenu wanapata stress hadi wanadondosha magari, dereva akipata ajali akifa familia zao hamzijali, ninyi mnajali pesa tu. unafikiri ninyi ndio wazalendo? ninyi ndio mashetani wa nchi hii. bora wachina waje.

Hiyo ndio ile "mkuki kwa nguruwe...", ni ubinafsi tu!
 
Hatimaye wafanya biashara wamekuja bongo they mean "STRICTLY BUSINESS" by the way Mkuu naomba nsaidie kutaja majina ya hizo kampuni niwe ata napata usingizi safarini nimechoka kusafiri roho mkononi
mabasi ya wachina ni new force aisee, amesambaza njia zote nchini tena mabasi mawilimawili kwa safari moja kila eneo. songea mawili kwenda mawili kurudi, tunduma mawili, mbeya mawili, kahama, mwanza, everywhere. asubuhi mchina anasimama mlangoni anasimamia ukusanyaji hela na basi likiondoka yeye ndio anarudi kulala. wako vizuri sana.

basi lingine ni JM ni la mbongo, liko vizuri kuliko hata new force, sasa huyo jamaa naona kashindwa biashara na madeni yanamnyemelea aliyokopa kununua mangarangara na anakuja hapa kulialia. kama umeshindwa biashara rudi kijijini kalime.
 
Mkuu tuanze na hilo la udalali sokoni, nimewahi kuhusika na study iliyonipitisha kwenye hayo masoko.

Hakuna mkulima yeyote anayeweza kuuza bila dalali. Wameshikilia kuanzia mfumo wa uongozi mpaka upangaji wa bei.

The same na mabasi, hawa wamiliki wa basi moja hawezi kupata abiria bila dalali. Ukiweka dalali hapa Dar likienda mikoani litakutana nao, na akifanya mchezo hata huko wanaweza kumwekea kauzibe. Wana network yao. Na hapa ndipo serikali inapaswa kuingia ili kudhibiti hali.

Hata hao wachina hawatumii ofisi zao tu kukatia ticket, wanatumia pia agents.

Anachoelezea mleta thread ni kuwa pawepo na fair ground na kanuni zinazomlinda mzawa, ingawa nao wanapaswa kuboresha biashara yao.

Nimekupata Mkuu. Lakini hili jambo huwa linaniuma sana, mijitu inapata pesa tena nyingi tu bila kutoa josho ilihali mwenye mali kajinyima hata kukopa benki ili ajikomboe !!!
 
Hii biashara ya usafirishaji serikali ilijitoa, hivyo hakuna kosa la wachina kuhozi fursa hii, kwanza bado wako kwenye utafiti wa mabasi yao kwa kuanza na soko la East africa, kama mnakumbuka Yuotong za kwanza zilikuwa engine nyuma wakagundua kwa mwendo mrefu hazifai maana zinapata joto sana mpaka zinafeli, pia body zao zilikuwa mzito mno wakawa wanalipa zaidi kwenye mzani, hivi sasa youtong mpya zimebadilishwa engine mbele na zinafanya vizuri, sasa hivi ndio zinateka soko kwa ubora, Je, mnataka tuwatumie madreva wa kitanzania kwenye utafiti hiilhali matajiri wenyewe ni watoa kafara, gari hizi zitagundua lini matatizo wakati watafiti wote wamekufa?
 
bora wachina walivyo kuja kuwachachafya na mingarangara yenu,kuna haya magari mawili nahisi ni ya mtoa mada ambayo ni mbazi na chakito longway nimeapa sipandi tena magari yananuka,joto,full kutu siti zimebanana utasema wanakaa chekechea ...pambavu zenu
 
Watanzania wenzangu subirinindawa iingie vizuri

Kwanza nauli zenu ziko juu sana mnatukomoa watanzania wenzenu
Pili mkikopa benki mnapeleka pesa kwenye miradi mingine matokeo yake mnakimbia mikopo. Kumbuka Scandinavia bus
Sasa cha wachina watupe huduma kwa bei nafuu
 
kwahiyo hata makalio umenunua ya mchina yanayouzwa US na ulaya magaribi sio? hapo hujamkwepa mchina bado. yuko na wewe tu uendako.
mimi ninayo natural ya kinyatunzu chapa ya ng'ombe,sihitaji mchina
 
Back
Top Bottom