Ba Brio
Bora wachina mara mia, kwasababu mabasi yao ni bora, yana kiyoyozi, bei nafuuu na hawachinji kutoa makafara kama ninyi wabongo na mibasi yenu takataka mliyotengeneza bodi kenya. mmetunyanyasa vya kutosha na kwa miaka mingi sana mkipandisha bei mpendavyo, soko huria linaendelea itafika kipindi mtapaki hayo mangarangara yenu garage.
sisi abiria tunachohitaji sio basi la mtanzania, tunachohitaji ni usafiri bora, hatujali ni wa mtz au mchina au mzungu, na hata wewe ukipata hela yako mimi hainihusu ni yako wewe na watoto wako hivyo niko radhi hata kuungana na mchina ili basi lako life kama kutakuwa na maslahi. kwendeni zenu huko chinjachinja ninyi. mlizoea biashara za mabasi kwa uchawi mchina amekuja kufanya biashara kwa kutumia akili, au naye kawazidi nguvu kwa dini yake ya Confucianism?