Wachimba makaburi wanavyoneemeshwa na watupa kafara

Wachimba makaburi wanavyoneemeshwa na watupa kafara

“Amezikwa miaka 20 iliyopita, lakini kila tunapochimba ili kuandaa kaburi jingine, tunamkuta kama alivyokuwa amelala, sanda haijagusa mchanga, wala ubao aliolaziwa haujaliwa na wadudu,” anasema huku akionyesha kaburi hilo.


Dalili njema mnoo kwa huyu kiumbe yaonekana alikuwa mchamungu.[emoji120] [emoji120] [emoji120]
Acha tu mjomba. Tumuombe mungu tuwe miongoni mwao.
 
Duuuh hongera jamani maana mm kwenda kizika siku moja tu nikirudi kichwa kinauma balaa
Hajawahi zika Mpendwa wako, sisi wengine tumezika mzazi na mtoto, kwa hiyo masuala ya mortuary na makaburi tunaona kawaida ingawa haizoeleki, ila kifupi umauma sana, nimesoma hii stori inatukumbusha mengi
 
Halafu unakuta mwingine analalamika "Ooo kazi ya ukonda ni ngumu"....
Nadhani Leo ndo jamii itajua IPI ni kazi ngumu zaidi !!!
Kama ya mortuary,unaziona maiti za kila dizain, kifo kinatisha ingawa ndio utaratibu wa kibinadamu
 
Akili kama zako ndio za kuweka milioni tisa juu ya kaburi kisha unarudi kinyumenyume mpaka kwenu ili ufanikiwe
We ndio zuzu mtu anasema kabisa alifundishwa na wataalamu wa kazi, hao wataalamu unafikiri madaktari wa muhimbili?
 
Lakini kumbuka jamaa anasema pesa walizoweka zilikuwa ni bandia...Na hao Waganga wa Kikongamani walikamatwa kwa kuwa na pesa bandia
Jamaa hata hajaelewa, wale wachimba makaburi kwa maelezo yao na wao inaonekana wamejizindika..
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] mujini shule
 
Duh, jamaa anakwambia amekula mbuzi mzima na hata kichwa hajaumwa.. [emoji23] [emoji23]
 
Hapo kwenye huyo mtu ambaye haozi nadhani hilo eneo halina bacteria wa kuozesha huo mwili au ulipakwa dawa ya kuzuia kuoza

Ni mtazamo tu
Mkuu tafuta mtazamo mwingine. Miili yetu imejaa kkila aina ya wadudu wanaosubiri kwa hamu tufe waozeshe miili yetu. Kwa kifupi hao wadudu huwa tunaingia nao humwo kaburini.
 
Akili kama zako ndio za kuweka milioni tisa juu ya kaburi kisha unarudi kinyumenyume mpaka kwenu ili ufanikiwe
Ila waliwaweza, zilikuwa bandia.
 
Ambacho sijaelewa ni wanaposema wanakuta au kuona mabaki kama hayo yasiyooza, je wanayakuta kwa kuwa wanachimba makaburi ya zamani au kwa kuchimba pembeni ya makaburi ya zamani ndio huyakuta/ kuyaona mabaki ya miili? Hakuna uwezekano wa eneo au kaburi, kuzikwa zaidi ya maiti moja kweli kwa wakati tofauti, maana Inashangaza baada ya miaka mingi na watu wengi sana kufariki, bado maeneo maarufu ya mazishi yanaendelea kutumika kwa mazishi, kana kwamba hayajai.
 
Back
Top Bottom