Wachawi wanikosesha usingizi usiku wa leo

Wachawi wanikosesha usingizi usiku wa leo

Ninapatwa na ukakasi hasa kuhusu uelewa wako katika biblia hiyo hiyo unayoisoma sasa kama si vizuri kutrace your origin Basi hata Yesu wako nina mashaka nae sababu aliyepo kwenye maandiko ukisoma Mathayo 1 yote ile ina trace origin asili ya Yesu zaidi ya vizazi vitano nyuma.......Waliona umuhimu ndiyo maana wakaliandika hilo...ukweli una shida somewhere there is missing part..

Hiyo historia ya Ukoo wa Daudi unafikiria iliandikwa ili kutoa nafasi yesu au ukoo wake "kuvunja" maagano na miti ya laana? Kwa hiyo Biography kwa mfano ya Ukoo wa Magufuli ipo ili kuonyesha kuwa huko nyuma kwenye ukoo wao kulwahi kuwa na Raisi na ndio maana na yeye akafanikiwa kuukwaa uraisi?
 
Hujajibu swali. Jibu swali.

Mimi si "Great Thinker". Na wala sihitaji uniite au unione great thinker.

"Great Thinker" kwangu ni tusi la kejeli.

Aristotle alikuwa "Great Thinker". Kwa sababu hiyo, alisimamisha na kurudisha nyuma maendeleo ya sayansi kwa miaka 1600.

Sitegemei umjue Aristotle wala kisa ninachozungumzia.

Kwa sababu unaonekana kuona "Great Thinker" kuwa ni sifa nzuri.



Sent from my Kimulimuli
Kuna ulazima wa kukujibu.kama ulazima upo,fungua uzi wako wa maswali nakuja kukujibu.na kama haupo mkuu unaweza kupita mdogo mdogo sitopata hasara
 
Basi
Hiyo historia ya Ukoo wa Daudi unafikiria iliandikwa ili kutoa nafasi yesu au ukoo wake "kuvunja" maagano na miti ya laana? Kwa hiyo Biography kwa mfano ya Ukoo wa Magufuli ipo ili kuonyesha kuwa huko nyuma kwenye ukoo wao kulwahi kuwa na Raisi na ndio maana na yeye akafanikiwa kuukwaa uraisi?

Basi huna tofauti na Mafarisayo ambao mpaka leo wana amini na wanasema mpaka leo Yesu sio Mfalme sababu hakutoka katika Ukoo wa Daudi.......
 
Haikuwa na ulazima wa wewe kumuongelea Mwakasege mkuu.wakati mwingine ni salama sana kukaa kimya na kuyaangalia maneno yako.

Kwani ungepita bila kusema chochote ungepungukiwa nini???

Kama unataka kumuongelea Mwl Christopher Mwakasege fungua uzi wako mkuu.usiniletee laana

Kama humpendi mtumishi fulani wa Mungu usimkashfu.ni vyema ukakaa kimya



Ungetaka asiongelewe katika uzi huu usingalimtaja! Haiwezekani umuongelee na mimi iwe dhambi kumuongelea.Mafundisho yake hayo si anayatoa hadharani sasa kuna kosa gani kumuongelea hapa? Kwani kwenye Uzi mama ulitahadharisha wachangiaji wasimuongelee?
 
Kuna ulazima wa kukujibu.kama ulazima upo,fungua uzi wako wa maswali nakuja kukujibu.na kama haupo mkuu unaweza kupita mdogo mdogo sitopata hasara
Kwanza kabisa weka alama ya kuuliza kwenye swali.

Vinginevyo utakuwa unaiambia dunia hujui kuandika.

Kuna ulazima wa kunijibu kwa mtu yeyote mwenye ubongo unaochemka.

Kwa sababu hoja haitakiwi kuachwa bila kujibiwa.

Kuacha kujibu hoja ni ishara ya woga na ukosefu wa hoja.

Hata kama jibu ni kukubali tu kwamba sawa, umeeleweka na umeshinda kwa hoja, utakuwa umejibu hoja.

Na uzi mwingine sitaki kufungua.

Kwa sababu hakuna sababu ya kufungua uzi mwingine kwa jambo ambalo tunaliongelea vizuri kabisa hapa.

Kama hoja imekuzidi kimo, unaweza kusema tu hilo nalo.

Si dhambi kukutana na hoja iliyokuzidi kimo.

Sent from my Kimulimuli
 
Hiyo historia ya Mababu zako toka Adamu na Hawa Mwakasege mdo anaifahamu vizuri? Yeye ndo anaweza kuzichambua vizuri historia za watu wote duniani? Yeye ya kwake nani alimchambulia? Baadhi ya Waafrika mulienda shule kukariri mambo au kung'azwa vichwa vyenu?
Mkuu naona unajichanganya aiseeh.hebu rudi kasome upya uzi wangu tena kwa umakini.maana yanakutoka maneno kibao.soma vizur mkuu unajibu sivyo.

Kuna mtu hapa anajaribu kukuelewesha lkn hueleweki.kuwa makini mkuu
 
Hivi kwanini usiku wanasema usiite chumvi sababu Ni nini

Sent from my TECNO W5 Lite using JamiiForums mobile app
Walikuwa wanabana matumizi tu hao itakuwa.

Mila nyingine zina sababu practical lakini zinewekwa kama miiko ya siri kubwa.

Zamani chumvi ilikuwa deal sana. Sehemu nyingine ilitumika kama hela.

Sent from my Kimulimuli
 
Basi


Basi una tofauti na Mafarisayo ambao mpaka leo wana amini na wanasema mpaka leo Yesu sio Mfalme sababu hakutoka katika Ukoo wa Daudi.......


Soma maandiko Matakatifu na uyaelewe vizuri.Historia ya Ukoo wa Yesu ipo kutuhabarisha tu juu ya chimbuko lake na sio kama hao wahubiri wenu wafanyavyo leo.Maudhui ya Biography ya Yesu ni kama ilivyo leo kwa Biography ya Nyerere,Nkurumah,Kenyata,Mkwawa, wewe na mimi.Jambo la msingi na la kujivunia ni kile alichofanya Yesu kwa kutokea katika ukoo huo:kufa na kufufuka kwa ajili ya kutuondoshea dhambi zetu.
 
Uja


Ujaelewa Boss.......Yaani yeye kama yeye aanze kujifahamu asili ya kwake kwa wale ambao wapo au apate mtu ambaye anawafahamu wao lada babu na bibi zake wazaa wazazi wake....ndivyo nilivyomaanisha Mkuu.
Mkuu pole unajitahidi kumuelewesha mtu ambae haelewi.naona anayoyajibu mengi yapo kinyume.

Anakera kweli.mshauri asome kwa umakini aelewe ndo yaanze kumtoka maneno.

Yani mimi muhusika nimekuwa mpole nachukua ushauri,..yeye yanamfumuka maneno utafikiri yeye ndo mkereketwa sanaaaaa.anaboa kwa kweli
Pole mkuu
 
Soma maandiko Matakatifu na uyaelewe vizuri.Historia ya Ukoo wa Yesu ipo kutuhabarisha tu juu ya chimbuko lake na sio kama hao wahubiri wenu wafanyavyo leo.Maudhui ya Biography ya Yesu ni kama ilivyo leo kwa Biography ya Nyerere,Nkurumah,Kenyata,Mkwawa, wewe na mimi.Jambo la msingi na la kujivunia ni kile alichofanya Yesu kwa kutokea katika ukoo huo:kufa na kufufuka kwa ajili ya kutuondoshea dhambi zetu.
Swali langu kama unaamini Biblia umeliruka. Hujalijibu.

Sent from my Kimulimuli
 
Sasa nan kakudanganya kuna maji ya baraka ??.

Sent from my GT-S5310I using JamiiForums mobile app
 
Isije kuwa ni Mshana alikuzukia kiaina, zidisha maombi mkuu

Sukumaland
 
Wachawi wapo na wanatutesa sana sisi tuliozaliwa kwenye dini.hatujui cha mganga wala nini.

Kuna sehemu niliajiliwa nilikoma nilikuwa silali nachelewa kuamka nikamuuliza jirani akanambia kama sina kinga ya mwili nitateseka. akasema huku hutoweza kuishi.

Niliteseka nikataka kuacha kazi mama alinipa moyo nisaliii yaan nikisali kama ndo nawaita kwa Kasi

Nilienda kanisani nikachukua maji ya baraka na rozali nasaliiiiii mwisho wakapungu.

Nilitoka nilipokwenda chuo sikurudi. Sasa hivi ni mkubwa najua jinsi ya kusali ahasaaa ni maneno gani ya kusali ninapoishi kwa sasa mjini kuna wachawi huwezi amini. Wasomi wake za watu wabibi, na wanaume wachache.

Sijui nini kinanitokea kwa sasa yaan nina uwezo wa kusali na kumwona mchawi tangu mnaingia ndani. Hata niende kutembea sehemu kama kuna wachawi usiku naangaika sipati usingizi na mchawi akiingia ndani lazima nimuone.

Siku moja nimelala nilimwona Ness fulani akaja kanichezea kaniniga, asubuhi nikamwambia mwenye nyumba akasema huyo nesi ni mwalim wa wachawi. Nikakumbuka nilisali kizembe usiku nilikuwa nimechoka Ikabidi niende dukani kwake kununua dawa. Nikamwambia "shingo inauma usiku kuna mama alininiga ila akirudi kwangu hatotoka atabaki ndani hadi asubuhi." Akajisemesha wewe una uwezo gani nilimwambia nasali huwezi kuingia kwangu nisikujue.alianza kuja kupitia sura za watuwengine.ila maombi ndo kila kitu

Biblia yangu inalala kwenye mto na rozali, maji ya baraka hayakosi.nalala vizuri

La kufanya sali sana kabla hujalala kama unavaaga night dress ivae kwa kuigeuza.na kama utaweza weka maji kwenye jagi yaweke nyumbani mchawi hawezi kukugusa. Hizo njia mbili kwao ni mwiko.

Akikuta umegeuza nguo atarudi. Na akikuta maji wanasema anaona kama bahali. Mchawi akiguswa maji dawa zake uisha nguvu.so hawezi kuingia ndani
Aiseeh hongera sana mkuu.

Kumbe mchawi hapatani na maji ee..vipi kuhusu kugeuza nguo mkuu??inauhusiano gani??
 
Sasa nan kakudanganya kuna maji ya baraka ??.

Sent from my GT-S5310I using JamiiForums mobile app


nakumbuka wakat nafundishwa masomo ya rc kuingia kwenye ndoa padri akanipa hayo maji,kuna muda akawa anaoneshaa anataka kusema kitu! mwisho wa sk akaja akasema kitu! nikamuuliza hv hayo maji nan anayabariki akaniambia ni wao! toka hapo huwa sielew hayo maji ya baraka! anywys ni iman zaid!
 
Kama umemsoma mleta mada vizuri huyo Mwakasege ndiye anayemjaza hayo mafundisho ya kichawi.Kuhusu hilo la Biblia kuongelea laana;una ufahamu gani juu ya Biblia? Hicho unachokisema juu ya kuandikwa kwenye Biblia umekisoma pia katika Lugha mama ya Kiyunani au Kigriki na kukuta maana hiyo hiyo ambayo imekusudiwa na tafsiri ya Kiswahili au Kiingereza? Soma kwanza Historia ya Uandishi wa Biblia kabla ya kujielekeza kufanya kazi ya tafsiri.Petro na Paulo hawakufanya kazi ya kutafsiri Maandiko Matakatifu kwa upotofu kama afanyavyo huyo Mwakasege.BTW, nyakati za Petro na Paulo hakukuwa bado na mkusanyiko wa Maandiko Matakatifu pamoja kama ilivyo hivi leo na wala hawakuwahi wao wenyewe kwa mafundisho ya mdomo au nyaraka zao kupotosha waamini kama anavyofanya huyo jamaa yenu.
Yani we mtu bhana sijui ukoje!!umesoma uzi wangu lkni au unadandia tren kwa mbele!!hebu kuwa makini bhana.halafu kama wewe huamini maandiko ya kwenye Biblia ni wew.sisi utuache na tunayoyaamini.si lazima unachokitaka wewe kiwe kitakuwa.angalia maneno yako mkuu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom