Wachawi wanikosesha usingizi usiku wa leo

Wachawi wanikosesha usingizi usiku wa leo

Kama kweli huyo mtu anamfahamu akikutana naye kwenye macho ya nyama lazima akimbie maombi tu hakuna kingine ndiyo walimuwahi ili asisikilize neno la mwl Mwakasege

Sent from my SM-T800 using JamiiForums mobile app
 
Rudia katika uzi wa awali.....nilikuuliza nini. Na kama huelewi Kiswahili tafuta mtu wa kukusaidia ajuaye hiyo lugha.
Kuniambia nirudie katika uzi wa awali usio na jina wala namba katika ulimwengu wa hyperlink kunaonyesha hama huna ulijualo, ama umepotea njia.

Post a link here.

Or shut up.
 
Tumeshajadili sana haya mambo humu kuhusu imani za uchawi,wachawi na pilikapilika zao lakini naona watu wana vichwa vigumu! Ninyi munaogopesha watu na hayo "madude" yenu hamna kazi zingine za kujiongezea kipato? Kanisa Katoliki halina mafundisho juu ya uchawi wala wachawi.Kanisa lilishaweka wazi kuwa hayo mafundisho ya kutapeliana na ni ya kukopa.Wewe Charismatic inakuwaje unapingana na mafundisho mama? Hamna njia nyingine ya kujipatia vipato hadi mchukue nafasi kutapeli watu namna hii?
Wewe hujawahi kupatwa na shida kama ya mwenzetu,
Shetani yupo na anafanya kazi tena kabisa.
Nina mke wangu alikuwa na shida za majini nafahamu karaha alizokuwa anapata hasa nyakati za usiku,au akiwa kazini.
Nashukuru kituo cha karismatiki kimenisaidia sana.
Wewe umeandik haya kwakuwa hayajakufika.
 
Wewe hujawahi kupatwa na shida kama ya mwenzetu,
Shetani yupo na anafanya kazi tena kabisa.
Nina mke wangu alikuwa na shida za majini nafahamu karaha alizokuwa anapata hasa nyakati za usiku,au akiwa kazini.
Nashukuru kituo cha karismatiki kimenisaidia sana.
Wewe umeandik haya kwakuwa hayajakufika.

Hayawezi kunifika kwa sababu hayapo! Mchunguze mkeo atakuwa na matatizo mengineyo tu ila wewe hujui tu.Hukupaswa hata kwenda huko Charistimatiki.Ungetumia tu counselling angeachana nayo hayo mambo.Wewe utakuwa mwanaume-mwanamke.Una homoni kiasi zinazokaribiana na za mwanamke.Hungekuwa hivyo,ungemu-counsel tu hayo anayohangaika nayo hayapo na hivi asongeshe maisha.
 
Sijasema usali kwa kuomba kitu kimoja tu Bali na-discourage kuomba kwa ajili ya vitu visivyokuwepo.Ni kupoteza muda kuomba dhidi ya uchawi,majini,mikosi na au laana.Mambo hayo hayapo na hivi ku-concetrate nayo ni kupoteza nafasi na nguvu zako.
Sawa
 
Nionacho mimi, kadri unavyojuhusisha na mambo hayo ndio hutoki ng'o. Ukifuatilia sana story nyingi za walokole ama wanaoamini sana waganga ni flani mchawi, flani kachezewa, ukiumwa umerogwa ama shetani etc. Maisha yote wewe unakuwa wa kupambana na uchawi na shetani tu.

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Hayawezi kunifika kwa sababu hayapo! Mchunguze mkeo atakuwa na matatizo mengineyo tu ila wewe hujui tu.Hukupaswa hata kwenda huko Charistimatiki.Ungetumia tu counselling angeachana nayo hayo mambo.Wewe utakuwa mwanaume-mwanamke.Una homoni kiasi zinazokaribiana na za mwanamke.Hungekuwa hivyo,ungemu-counsel tu hayo anayohangaika nayo hayapo na hivi asongeshe maisha.
Huko ndo nimefanikiwa mkuu,ndiyo ujue Yesu yupo na anaponya.kama ni ishu ya counseling,nikuombe siku moja ukiona mtu kapandisha mashetani umfanyie hiyo counseling
 
Huko ndo nimefanikiwa mkuu,ndiyo ujue Yesu yupo na anaponya.kama ni ishu ya counseling,nikuombe siku moja ukiona mtu kapandisha mashetani umfanyie hiyo counseling
Kuna tofauti kubwa sana kati ya mtu mwenye dini ya kikristo na mwenye imani ya kikristo.........

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Mzee unakula unashiba + matunda na maji ya kutosha?

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Duuh! Pole sana, kwa jina La Yesu Kristo wa Nazareth aliye hai nakutangazia uzima. Mapepo na madubwasha yote yanayokudumbua yakaungue kwa damu ya Yesu Kristo.
 
Kuniambia nirudie katika uzi wa awali usio na jina wala namba katika ulimwengu wa hyperlink kunaonyesha hama huna ulijualo, ama umepotea njia.

Post a link here.

Or shut up.


Ni kutaka kukufunza kuwa ujinga wa kuuliza swali hilo hilo kila mara unachosha.
 
Ni kutaka kukufunza kuwa ujinga wa kuuliza swali hilo hilo kila mara unachosha.
Huwezi kumfunza mtu ikiwa hata wewe mwenyewe huwezi kuuhakikishia umma wa JF kwamba hiyo post unayosema ipo kweli na si habari uliyoitunga tu.

Mpaka sasa unaonekana umetunga habari ambayo haipo halafu unazuga ujuaji kama Mzee Jongo.

Sent from my Kimulimuli
 
una matatizo Ya kisaikolojia, wala sio uchawi mkuu.
Tafuta wana saikolojia wakusaidie kukuweka sawa
 
Wachawi wapo na wanatutesa sana sisi tuliozaliwa kwenye dini.hatujui cha mganga wala nini.

Kuna sehemu niliajiliwa nilikoma nilikuwa silali nachelewa kuamka nikamuuliza jirani akanambia kama sina kinga ya mwili nitateseka. akasema huku hutoweza kuishi.

Niliteseka nikataka kuacha kazi mama alinipa moyo nisaliii yaan nikisali kama ndo nawaita kwa Kasi

Nilienda kanisani nikachukua maji ya baraka na rozali nasaliiiiii mwisho wakapungu.

Nilitoka nilipokwenda chuo sikurudi. Sasa hivi ni mkubwa najua jinsi ya kusali ahasaaa ni maneno gani ya kusali ninapoishi kwa sasa mjini kuna wachawi huwezi amini. Wasomi wake za watu wabibi, na wanaume wachache.

Sijui nini kinanitokea kwa sasa yaan nina uwezo wa kusali na kumwona mchawi tangu mnaingia ndani. Hata niende kutembea sehemu kama kuna wachawi usiku naangaika sipati usingizi na mchawi akiingia ndani lazima nimuone.

Siku moja nimelala nilimwona Ness fulani akaja kanichezea kaniniga, asubuhi nikamwambia mwenye nyumba akasema huyo nesi ni mwalim wa wachawi. Nikakumbuka nilisali kizembe usiku nilikuwa nimechoka Ikabidi niende dukani kwake kununua dawa. Nikamwambia "shingo inauma usiku kuna mama alininiga ila akirudi kwangu hatotoka atabaki ndani hadi asubuhi." Akajisemesha wewe una uwezo gani nilimwambia nasali huwezi kuingia kwangu nisikujue.alianza kuja kupitia sura za watuwengine.ila maombi ndo kila kitu

Biblia yangu inalala kwenye mto na rozali, maji ya baraka hayakosi.nalala vizuri

La kufanya sali sana kabla hujalala kama unavaaga night dress ivae kwa kuigeuza.na kama utaweza weka maji kwenye jagi yaweke nyumbani mchawi hawezi kukugusa. Hizo njia mbili kwao ni mwiko.

Akikuta umegeuza nguo atarudi. Na akikuta maji wanasema anaona kama bahali. Mchawi akiguswa maji dawa zake uisha nguvu.so hawezi kuingia ndani


lucky tumpe Mungu heshima pekee.Bwana anasema hatagawana utukufu wwke na sanamu.Huwezi omba Mungu na bado ukaweka maji au kugeuza nguo ukiamini kuwa ni njia ya kumzuia mchawi.Maana yakr huamini kama Mungu pekee anaweza unatfta njia zingine.hizo ni shirki yaani unamshirikisha Mungu na vitu vingine.Mungu anaweza waacha hao wachawi waendelee kuja sababu unaamini kuwa yeye Mungu anahitaji booster.akikulinda mchawi asije utaenda kushuhudia kuwa Mungu kakulinda na maji na kugeuza nguo kumekusaidia kama ulivyofanya hapa.Biblia inasema anasema "sitagawana utukufu wangu na sanamu.ndo maana wanaendelea kuja hao.Ukimuita Mungu anataka ashuke atende kwa utukufu wake ili ukisimama kushuhudia ushuhudie yeye tu.nakwambua anza kuomba tu bila kufanya hayo mengine utakuja uniambie.afu weka namba yako hapa nikufunze hao wachawu jinsi ya kucheza nao nakwmbia watakuja wakyshuhudoe mwenywe kuwa hawawezi kanyaga kwako tenaaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom