Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Kwa kila anaeangalia vipindi vya Bunge la Tanzania katika TV ataona ni jinsi gani wabunge wanavyoikanyaga Bendera ya Taifa hili la Tanzania ,kwa vyovyote vile iwavyo wanaidharau Bendera yetu hii ambayo inaposhushwa kwenye mlingoti haitakiwi iguse chini ,iweje wabunge wawe wameitandika kwa marefu na mapana na halafu wanaikanyaga kwa viatu vyao vilivyojaa mavi ya kuku ? Hii ni dharau na jeuri au ndio ustaarabu ? SIjawahi kuona Nchi yeyote ile imeweka bendera yake chini na viongozi wanaikanyaga iwe ndani ya bunge au sehemu nyengine yeyote ile.
Kwa kuhisia tu mbunge anapoikanyaga pale huwezi kujua anapitiwa na fikira gani zaidi ya kuwaza kejeli ?
Je huu ni uungwana maana hata Raisi hatandikiwi Bendera .
Naomba kuwasilisha hoja ya kuondolewa zulia hili la bendera ya Taifa ndani ya Bunge letu ili liwe tukufu vinginevyo halifai kuitwa Bunge takatifu wakati linaichafua na kuikanyaga bendera ya Tanzania kwa viatu
Kwa kuhisia tu mbunge anapoikanyaga pale huwezi kujua anapitiwa na fikira gani zaidi ya kuwaza kejeli ?
Je huu ni uungwana maana hata Raisi hatandikiwi Bendera .
Naomba kuwasilisha hoja ya kuondolewa zulia hili la bendera ya Taifa ndani ya Bunge letu ili liwe tukufu vinginevyo halifai kuitwa Bunge takatifu wakati linaichafua na kuikanyaga bendera ya Tanzania kwa viatu
Last edited by a moderator: