Mkuu tuwe fair ili tuwasaidie baadhi ya wabunge wetu tunaowapenda, tukileta mahaba hatutawasaidia.Lusinde mtera nae cjui maana tumevumilia taarabu zake tumezichoka
Ukweli ni kwamba majimbo mengi ya vijijidi kama kwa lusinde bado yataendelea kubaki ccm kwa sababu nyepesi tu - uelewa wa watu huko bado ni mdogo, na pia mahaba yao kwa chama tawala ni ya kihistoria!.
Tukirudi kwenye majimbo ya mijini, hasa majiji makubwa huko watu wengi huwa hawana msimamo - wanapenda kumuona mbunge wao yupo active ktk kuwaondolea kero zao mbalmbal (bunge lililopita mnyika alifanya vzr eneo hili, hasa kero ya maji ubungo).
Majimbo ya mijini wapiga kura huwa ni vigumu kdg kuwadanganya (mjini shule!)
Kwa maoni yangu, wapinzani wengi mpaka sasa bado hawajafanya vzr majimboni mwao - na wakiendelea na "kasi" hii 2020 wengi watapukutika bungeni!!
Kwa upande wa chama tawala wao kdg ni tofauti, baadhi wanaweza kusalimika kwa upepo wa ngosha, ikumbukwe ngosha kwa kasi hii 2020 Mungu akituweka hai hatakuwa na mpinzani!!