mukama talemwa
Senior Member
- Jun 14, 2011
- 160
- 28
Kwa hili hata mimi Dilunga sikuelewi,maana hata hao wabunge waliobaki bungeni katika michango yao wote ni kutufahamisha wananchi kuwa wako pale kupitisha muswada na si kutunga katiba kama wabunge CDM na wanaarakati wanavyo dai.Sisi wananchi kutoingia bungeni sikana kwamba hatuna akili tunaelewa vizuri kinachoendelea bungeni.CDM na wananchi wengine ambao si wa chama chochote cha siasa tunapinga huo muswada kuodhiwa na serikali.Bunge liliagiza kamati ya kudumu ya bunge kupita katika mikoa mbalimbali kupata maoni ya wananchi lakini spika aliikatalia tume kufanya hivyo kisa eti yeye yuko India kwahiyo hilo haliwezekani,kwahiyo maoni ya wananchi hayajachukuliwa.Kitu kikubwa na cha kutisha ni madaraka makubwa aliyopewa raisi katika kuteua kamati ya kuratibu mchakato wa kuchukua maoni.Sio siri viongozi wetu siku zote wamekuwa na mawazo ya enzi za "ZIDUMU FIKRA SAHIHI ZA MWENYEKITI WA CCM"Sasahivi huko tumeisha toka