Wabunge CHADEMA wakubali yaishe, CUF watengwa!

Wabunge CHADEMA wakubali yaishe, CUF watengwa!

Kwani Binadamu hawezi kutubu na kubadilika?Lowassa n Sumaye waligundua kuwa hawako kwenye chama sahihi, kumbuku ukiwa kwenye chama unafata sera za chama si sera zako kama Furani anavyifata za kwake.....

Pumba.
 
Msigwa alishawahi kusema 'huwezi kutatua kosa kwa kutumia akili hiyo hiyo iliyosababisha kosa hilo'....akaendelea 'haiwezekani akili kubwa kutawala akili ndogo'. Akakazia 'wanaomuunga mkono Lowassa wakapimwe akili'.

Katika kampeni za Mwaka jana hoja kuu ya Chadema ilikuwa 'mabadiliko' ati wote walioongoza serikali katika kipindi cha miaka 50 iliyopita waondolewe sababu 'hawajafanya chochote ndani ya miaka 50 ya uongozi wao. Katika kuhakikisha wanaelekea katika mabadiliko hayo sasa wanalazimika kutumia 'akili ileile iliyosababisha matatizo ili kutatuta matatizo yale yale'. Kwa sasa Chadema hawawezi kufanya lolote bila kupata malekezo toka kwa Lowassa na Sumaye. Sasa akili ndogo inatoa ushauri kwa akili kubwa', wanapewa hadi maneno ya kuzungumza bungeni na kwenye mikutano ya siasa. Amri ni moja tu, ole wake mbunge wa chadema atakayezungumza kauli tofauti na maelekezo ya Sumaye na Lowassa...'atakiona cha mtema kuni'.

Ajizi nyumba ya njaa, wabunge wa chadema wamekubali yaishe kuwa Hemedi Alli ndiye mkuu mpya wa idara ya Habari na Propaganda Chadema. Tafsiri yake ni kwamba Tundu,Lema,Sugu na wenzao watalazimika kujifunza mila na tamaduni za chadema kutoka kwa Hemedi Ali. Hemedi Ali alijiunga Chadema tarehe 29.07.2015 siku Lowassa anatambulishwa kwa wanahabari kama Mgombea wa Chadema na baadaye Ukawa. Huyu alikuwa ni mwenyekiti wa 4U Movement. Ole wake Tundu aropoke, atawajibishwa..Msemaji ni mmoja tu Hemedi Ali.Bavicha mpya inakuja, vijana wa 4U,Ulipo Tupo na TeamLowassa kutawala nafasi za uongozi Chadema.

Katika hatua nyingine wabunge wa CUF wametengwa katika mazungumzo yaliyosimamiwa na Lowassa na Sumaye. Sasa ni kama watoto 'yatima', Seif hana habari nao.

Hakika wiki katika siasa ni sawa na mwaka katika maisha mengine, siku zinaenda kasi.

CUF watengwa kivipi? unajua agenda za kikao zilikuwa zipi? Huo ulikuwa mkutano wa chadema au Ukawa. Inamaana kile kikao cha CUF zanzibar CDM walitengwa? Ina maana CCM haina msemaji wa chama. Hizi propaganda za kizamani sana.
 
Nimepitia hii nyuzi, pamoja na comment zake naona huu mpambano ni kati Lumumba vs ufipa, tusubiri tuone nani mshindi
 
Toka Lowassa alipoachiwa agombee urais nilijua chama changu kimegeuzwa genge la wahuni.
 
Viongozi CHADEMA (Mbowe et al) hawana tofauti na enzi za Chifu Mangungo wa Msovelo aliyekabidhi ardhi kwa wageni (waliokatwa CCM) kwa bei chee..
 
Kwani Binadamu hawezi kutubu na kubadilika?Lowassa n Sumaye waligundua kuwa hawako kwenye chama sahihi, kumbuku ukiwa kwenye chama unafata sera za chama si sera zako kama Furani anavyifata za kwake.....
Teh Teh Teh Teh......
Kama Lowasa na Sumaye wawebadilika na kuwa wasafi; Natumai CCM pia imebadilikaa au itabadilika tyuuu....hivyo tuendelee kuipa ridhaa tena na tena
 
k
Mpaka wakati wa utawala wa George Bush Junior Donald Trump alikuwa ni mwanachama mkubwa tu wa Democrat. Kwenye siasa haya ni mambo ya kawaida tu, yasikuumize sana. Kuna mwanasisa aliwahi kujiapiza hadi Mama yake mzazi iwapo atarudi ccm, lakini alirudi na akapewa usemaji mkuu wa chama.
wa hiyo Trump ni nani hadi tumfate
 
Siwezi Jenga hoja kwa mabandiko yako yako coz inaonekana uwezo wako wa kufikiri ni Mdogo mno, ila naomba ujifunze kwa wasira alitokea wapi mpaka ccm wakampokea, na wakampa nafc gan kwenye serkali na ndani ya chama
post za wenye uwezo mdogo wa kufikiri unazikomentia nini jamani
 
bring back our mwanahalisi, enzi hizo kubenea hajanunuliwa
mwanah.jpg
 
hata Tanzania Daima lilikuwaga tamu nyieee acheni pesa iitwe pesa
IMG-20150723-WA0026.jpg
 
Kwani Binadamu hawezi kutubu na kubadilika?Lowassa n Sumaye waligundua kuwa hawako kwenye chama sahihi, kumbuku ukiwa kwenye chama unafata sera za chama si sera zako kama Furani anavyifata za kwake.....
Baada ya kutuibia ndio wametubu? Warejeshe walichotuibia hapo watakuwa wametubu bila hivyo ni tamaa ya madaraka hawana kipya
 
Back
Top Bottom