Wabunge CHADEMA wakubali yaishe, CUF watengwa!

Wabunge CHADEMA wakubali yaishe, CUF watengwa!

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2016
Posts
17,505
Reaction score
16,006
Msigwa alishawahi kusema 'huwezi kutatua kosa kwa kutumia akili hiyo hiyo iliyosababisha kosa hilo'....akaendelea 'haiwezekani akili kubwa kutawala akili ndogo'. Akakazia 'wanaomuunga mkono Lowassa wakapimwe akili'.

Katika kampeni za Mwaka jana hoja kuu ya Chadema ilikuwa 'mabadiliko' ati wote walioongoza serikali katika kipindi cha miaka 50 iliyopita waondolewe sababu 'hawajafanya chochote ndani ya miaka 50 ya uongozi wao. Katika kuhakikisha wanaelekea katika mabadiliko hayo sasa wanalazimika kutumia 'akili ileile iliyosababisha matatizo ili kutatuta matatizo yale yale'. Kwa sasa Chadema hawawezi kufanya lolote bila kupata malekezo toka kwa Lowassa na Sumaye. Sasa akili ndogo inatoa ushauri kwa akili kubwa', wanapewa hadi maneno ya kuzungumza bungeni na kwenye mikutano ya siasa. Amri ni moja tu, ole wake mbunge wa chadema atakayezungumza kauli tofauti na maelekezo ya Sumaye na Lowassa...'atakiona cha mtema kuni'.

Ajizi nyumba ya njaa, wabunge wa chadema wamekubali yaishe kuwa Hemedi Alli ndiye mkuu mpya wa idara ya Habari na Propaganda Chadema. Tafsiri yake ni kwamba Tundu,Lema,Sugu na wenzao watalazimika kujifunza mila na tamaduni za chadema kutoka kwa Hemedi Ali. Hemedi Ali alijiunga Chadema tarehe 29.07.2015 siku Lowassa anatambulishwa kwa wanahabari kama Mgombea wa Chadema na baadaye Ukawa. Huyu alikuwa ni mwenyekiti wa 4U Movement. Ole wake Tundu aropoke, atawajibishwa..Msemaji ni mmoja tu Hemedi Ali.Bavicha mpya inakuja, vijana wa 4U,Ulipo Tupo na TeamLowassa kutawala nafasi za uongozi Chadema.

Katika hatua nyingine wabunge wa CUF wametengwa katika mazungumzo yaliyosimamiwa na Lowassa na Sumaye. Sasa ni kama watoto 'yatima', Seif hana habari nao.

Hakika wiki katika siasa ni sawa na mwaka katika maisha mengine, siku zinaenda kasi.
 
Kwamba akili iliyotengeneza matatizo ya nchi yetu kwa miaka 50(Lowasa&Sumaye) ndiyo akili hiyo hiyo inatumika na Chadema kuyatatua matatizo hayo, kinyume na kile anachoamini Mh. Msigwa wa Chadema. Akili ndogo inatawala akili kubwa.
 
Nakuambia Tanzania bado hatujapata upinzani wa kweli,
Watasema mchawi ni Ccm kumbe ni wao wenyewe.

Mwananchi aliye choka na chama kimoja
Ili umpeleke chama kingine
Ni lazima uwe na mambo mapya
Watu wapya na hoja zenye mashiko
Ajabu
Wale aliye wachoka Ccm aende kuwakuta cdm
Tena ndio waamuzi wa lolote ndani ya chama!!!

MSIGWA MUNGU ANAKUONA KWA KAULI ZAKO ZILE
HUONI AIBU!!!!
 
Kwani Binadamu hawezi kutubu na kubadilika?Lowassa n Sumaye waligundua kuwa hawako kwenye chama sahihi, kumbuku ukiwa kwenye chama unafata sera za chama si sera zako kama Furani anavyifata za kwake.....
 
Msigwa alishawahi kusema 'huwezi kutatua kosa kwa kutumia akili hiyo hiyo iliyosababisha kosa hilo'....akaendelea 'haiwezekani akili kubwa kutawala akili ndogo'. Akakazia 'wanaomuunga mkono Lowassa wakapimwe akili'.

Katika kampeni za Mwaka jana hoja kuu ya Chadema ilikuwa 'mabadiliko' ati wote walioongoza serikali katika kipindi cha miaka 50 iliyopita waondolewe sababu 'hawajafanya chochote ndani ya miaka 50 ya uongozi wao. Katika kuhakikisha wanaelekea katika mabadiliko hayo sasa wanalazimika kutumia 'akili ileile iliyosababisha matatizo ili kutatuta matatizo yale yale'. Kwa sasa Chadema hawawezi kufanya lolote bila kupata malekezo toka kwa Lowassa na Sumaye. Sasa akili ndogo inatoa ushauri kwa akili kubwa', wanapewa hadi maneno ya kuzungumza bungeni na kwenye mikutano ya siasa. Amri ni moja tu, ole wake mbunge wa chadema atakayezungumza kauli tofauti na maelekezo ya Sumaye na Lowassa...'atakiona cha mtema kuni'.

Ajizi nyumba ya njaa, wabunge wa chadema wamekubali yaishe kuwa Hemedi Alli ndiye mkuu mpya wa idara ya Habari na Propaganda Chadema. Tafsiri yake ni kwamba Tundu,Lema,Sugu na wenzao watalazimika kujifunza mila na tamaduni za chadema kutoka kwa Hemedi Ali. Hemedi Ali alijiunga Chadema tarehe 29.07.2015 siku Lowassa anatambulishwa kwa wanahabari kama Mgombea wa Chadema na baadaye Ukawa. Huyu alikuwa ni mwenyekiti wa 4U Movement. Ole wake Tundu aropoke, atawajibishwa..Msemaji ni mmoja tu Hemedi Ali.Bavicha mpya inakuja, vijana wa 4U,Ulipo Tupo na TeamLowassa kutawala nafasi za uongozi Chadema.

Katika hatua nyingine wabunge wa CUF wametengwa katika mazungumzo yaliyosimamiwa na Lowassa na Sumaye. Sasa ni kama watoto 'yatima', Seif hana habari nao.

Hakika wiki katika siasa ni sawa na mwaka katika maisha mengine, siku zinaenda kasi.
Sera za chama na si sera za mtu.......Wao walifata vile chama kinataka,
 
Mpaka wakati wa utawala wa George Bush Junior Donald Trump alikuwa ni mwanachama mkubwa tu wa Democrat. Kwenye siasa haya ni mambo ya kawaida tu, yasikuumize sana. Kuna mwanasisa aliwahi kujiapiza hadi Mama yake mzazi iwapo atarudi ccm, lakini alirudi na akapewa usemaji mkuu wa chama.
 
Kwani Binadamu hawezi kutubu na kubadilika?Lowassa n Sumaye waligundua kuwa hawako kwenye chama sahihi, kumbuku ukiwa kwenye chama unafata sera za chama si sera zako kama Furani anavyifata za kwake.....
Mbona Chademaa wanafuata sera za Lowassa? kwani Lowassa ni chama?
 
Nakuambia Tanzania bado hatujapata upinzani wa kweli,
Watasema mchawi ni Ccm kumbe ni wao wenyewe.

Mwananchi aliye choka na chama kimoja
Ili umpeleke chama kingine
Ni lazima uwe na mambo mapya
Watu wapya na hoja zenye mashiko
Ajabu
Wale aliye wachoka Ccm aende kuwakuta cdm
Tena ndio waamuzi wa lolote ndani ya chama!!!

MSIGWA MUNGU ANAKUONA KWA KAULI ZAKO ZILE
HUONI AIBU!!!!
Mkaachaga unafiki nyie watu,kama mnaona hatuna wapinzani Tanzania sasa mbona kila kukicha mnawadhibiti na kuwatungia makosa yasiyo na maana wewe sema Tanzania hatuna chama Tawala chama chetu ni polisi utaeleka sio unaonge pumba hapa
 
Mbona
Mbona Chademaa wanafuata sera za Lowassa? kwani Lowassa ni chama?
CCM wanapelekeshwa kwa sera za mtu m1? Na ukiangalia CDM wanafata sera zao kabla hata Lowassa hajajiunga nao,hata kama Lowassa alikuwa mchafu CCM;kuja CDM ni kama mtu mwenye dhambi aliyejigundua na kuamua kuokoka na kumfata yesu au njia za yesu,unaweza usifanye vzr ukiwa simba ila ukisajiliwa Yanga na ukapewa nafasi unafanya vzr zaidi Binadamu sio mlima.
 
Mbona

CCM wanapelekeshwa kwa sera za mtu m1? Na ukiangalia CDM wanafata sera zao kabla hata Lowassa hajajiunga nao,hata kama Lowassa alikuwa mchafu CCM;kuja CDM ni kama mtu mwenye dhambi aliyejigundua na kuamua kuokoka na kumfata yesu au njia za yesu,unaweza usifanye vzr ukiwa simba ila ukisajiliwa Yanga na ukapewa nafasi unafanya vzr zaidi Binadamu sio mlima.
Ni hivi ''chadema lazima ihitimu kutoka uanaharakati hadi chama cha siasa'.....Hivi huoni jinsi chadema ilivyobadilika kufuata sera za Lowassa?
 
Mpaka wakati wa utawala wa George Bush Junior Donald Trump alikuwa ni mwanachama mkubwa tu wa Democrat. Kwenye siasa haya ni mambo ya kawaida tu, yasikuumize sana. Kuna mwanasisa aliwahi kujiapiza hadi Mama yake mzazi iwapo atarudi ccm, lakini alirudi na akapewa usemaji mkuu wa chama.


mfano wako Wa Donald trump ni sahihi kabisa maana huto trump hapati urais Wa America
 
Kwani Binadamu hawezi kutubu na kubadilika?Lowassa n Sumaye waligundua kuwa hawako kwenye chama sahihi, kumbuku ukiwa kwenye chama unafata sera za chama si sera zako kama Furani anavyifata za kwake.....


kusaka urais Tanzania company limited ni
kampuni inayotakiwa kusajiriwa Na kiongozi au
mwenyekiti anatakiwa awe mh lowassa!!
kampuni hii ni kongwe sana tangia enzi za
Mwalimu Nyerere!!kampuni hii ni mabingwa Wa
kutengeneza mitandao hatari ndani ya chama ili
kuusaka urais kwa udi Na uvumba!!kampuni hii
haiamini kitu kingine Bali nguvu ya pesa Na
propaganda za uongo!! kampuni hii yenye kirusi
kibaya cha kutengeneza mitandao ilitaka
kuimaliza nchi kupitia CCM!!kama
kusingekuwepo antivirus Kali inayoundwa Na
wazee Wa CCM basi Leo tungekuwa
tunazungumza mengine!!kampuni hii ndiyo
iliyomweka rais mstaff madarakani japo
wapinzani wakiongozwa Na mh Mbowe walikuwa
wanamsema kuwa eti ni dhaifu!!chakushangaza
kwa sababu Leo kampuni hii hatari imehamia
chadema wanatamani Leo kama rais
waliyemdhalilisha mbele ya wananchi wake
angerudi madarkani wapate ahuweni maana rais
aliyeko madarakani kwa sasa amewakaba koo
wanashindwa kupumua!!
Tunamshukuru Mungu sana sana kuwa kampuni
hii imehama chama chetu japo masalia yapo!!
Nakionea huruma chama kilichopokea kampuni
hii maana kama Mwalimu nyerere aliiogopa
kampuni hii iliakuwaje chadema wakaipokea Na
kuikumbatia? kwa masikitiko makubwa ni
kwamba chadema si chama tena chakuwatetea
wanyonge kama ilivyokuwa awali!!
kirusi hiki kitaitafuna chadema mpaka pale
itakapokuwa Na wazee wenye busara
waliyotayari kupinga kampuni hii
 
Mkaachaga unafiki nyie watu,kama mnaona hatuna wapinzani Tanzania sasa mbona kila kukicha mnawadhibiti na kuwatungia makosa yasiyo na maana wewe sema Tanzania hatuna chama Tawala chama chetu ni polisi utaeleka sio unaonge pumba hapa
USITUDANGANYE. KAMA HAMNAXWAPINZANI MBONA TUNAAMBIWA HAKUNA MIKUTANO ILI KUIMARISHA ZAIDI UPINZANI? MBONA KUNA MKAKAKATI WA KUIVURGA CUF ILI KULETA UHAFIFU WA UPINZANI?
 
Imekugonga,ndio maana unaweweseka...jenga hoja na sio kubwabwaja.
Siwezi Jenga hoja kwa mabandiko yako yako coz inaonekana uwezo wako wa kufikiri ni Mdogo mno, ila naomba ujifunze kwa wasira alitokea wapi mpaka ccm wakampokea, na wakampa nafc gan kwenye serkali na ndani ya chama
 
Kwa hiyo Lowasa anazidi kuteka Kambi za Chadema...... taratibu Mbowe anazidi kupoteza ushawishi ndani ya Chama.

Hongera Lowasa kwa kuwafanya wabaya wako wakupigie Magoti.
 
Back
Top Bottom