Wabunge CHADEMA wakubali yaishe, CUF watengwa!

Wabunge CHADEMA wakubali yaishe, CUF watengwa!

Kwani Binadamu hawezi kutubu na kubadilika?Lowassa n Sumaye waligundua kuwa hawako kwenye chama sahihi, kumbuku ukiwa kwenye chama unafata sera za chama si sera zako kama Furani anavyifata za kwake.....
Na hao waliokuwa kwenye hicho chama ambacho sio sahihi nao wao wamebadilika kama lowassa na sumaye haya waungeni mkono.
 
Kwamba akili iliyotengeneza matatizo ya nchi yetu kwa miaka 50(Lowasa&Sumaye) ndiyo akili hiyo hiyo inatumika na Chadema kuyatatua matatizo hayo, kinyume na kile anachoamini Mh. Msigwa wa Chadema. Akili ndogo inatawala akili kubwa.
Lumumba buana
 
Hi
Msigwa alishawahi kusema 'huwezi kutatua kosa kwa kutumia akili hiyo hiyo iliyosababisha kosa hilo'....akaendelea 'haiwezekani akili kubwa kutawala akili ndogo'. Akakazia 'wanaomuunga mkono Lowassa wakapimwe akili'.

Katika kampeni za Mwaka jana hoja kuu ya Chadema ilikuwa 'mabadiliko' ati wote walioongoza serikali katika kipindi cha miaka 50 iliyopita waondolewe sababu 'hawajafanya chochote ndani ya miaka 50 ya uongozi wao. Katika kuhakikisha wanaelekea katika mabadiliko hayo sasa wanalazimika kutumia 'akili ileile iliyosababisha matatizo ili kutatuta matatizo yale yale'. Kwa sasa Chadema hawawezi kufanya lolote bila kupata malekezo toka kwa Lowassa na Sumaye. Sasa akili ndogo inatoa ushauri kwa akili kubwa', wanapewa hadi maneno ya kuzungumza bungeni na kwenye mikutano ya siasa. Amri ni moja tu, ole wake mbunge wa chadema atakayezungumza kauli tofauti na maelekezo ya Sumaye na Lowassa...'atakiona cha mtema kuni'.

Ajizi nyumba ya njaa, wabunge wa chadema wamekubali yaishe kuwa Hemedi Alli ndiye mkuu mpya wa idara ya Habari na Propaganda Chadema. Tafsiri yake ni kwamba Tundu,Lema,Sugu na wenzao watalazimika kujifunza mila na tamaduni za chadema kutoka kwa Hemedi Ali. Hemedi Ali alijiunga Chadema tarehe 29.07.2015 siku Lowassa anatambulishwa kwa wanahabari kama Mgombea wa Chadema na baadaye Ukawa. Huyu alikuwa ni mwenyekiti wa 4U Movement. Ole wake Tundu aropoke, atawajibishwa..Msemaji ni mmoja tu Hemedi Ali.Bavicha mpya inakuja, vijana wa 4U,Ulipo Tupo na TeamLowassa kutawala nafasi za uongozi Chadema.

Katika hatua nyingine wabunge wa CUF wametengwa katika mazungumzo yaliyosimamiwa na Lowassa na Sumaye. Sasa ni kama watoto 'yatima', Seif hana habari nao.

Hakika wiki katika siasa ni sawa na mwaka katika maisha mengine, siku zinaenda kasi.


Hivi kucomment bila ya kumtaja Lowasa au sumaye unawashwa? Si uende mombasa kenya kuna wataalamu mafundi
 
Nakuambia Tanzania bado hatujapata upinzani wa kweli,
Ni aibu kufanya kazi kwa kutegemea kwanza upate upinzani wa kweli. Kwani ukiahidi ajira, viwanda na mikopo ya elimu ya juu, hadi wapinzani wa kweli wakusemeseme ndio utekeleze ahadi? Tekeleza ahadi kwa kadiri ulivyoahidi, si lazima usukumwe!
 
Kwani Binadamu hawezi kutubu na kubadilika?Lowassa n Sumaye waligundua kuwa hawako kwenye chama sahihi, kumbuku ukiwa kwenye chama unafata sera za chama si sera zako kama Furani anavyifata za kwake.....
Kwa hiyo CDM ni chama cha waliotubu?
 
Uchumi unapanda kwa asilimia 7.9 lakini lengo ni kufikia 7.2. Ha, ha, ha, ni Bosi wa Malaika huyo.
 
kusaka urais Tanzania company limited ni
kampuni inayotakiwa kusajiriwa Na kiongozi au
mwenyekiti anatakiwa awe mh lowassa!!
kampuni hii ni kongwe sana tangia enzi za
Mwalimu Nyerere!!kampuni hii ni mabingwa Wa
kutengeneza mitandao hatari ndani ya chama ili
kuusaka urais kwa udi Na uvumba!!kampuni hii
haiamini kitu kingine Bali nguvu ya pesa Na
propaganda za uongo!! kampuni hii yenye kirusi
kibaya cha kutengeneza mitandao ilitaka
kuimaliza nchi kupitia CCM!!kama
kusingekuwepo antivirus Kali inayoundwa Na
wazee Wa CCM basi Leo tungekuwa
tunazungumza mengine!!kampuni hii ndiyo
iliyomweka rais mstaff madarakani japo
wapinzani wakiongozwa Na mh Mbowe walikuwa
wanamsema kuwa eti ni dhaifu!!chakushangaza
kwa sababu Leo kampuni hii hatari imehamia
chadema wanatamani Leo kama rais
waliyemdhalilisha mbele ya wananchi wake
angerudi madarkani wapate ahuweni maana rais
aliyeko madarakani kwa sasa amewakaba koo
wanashindwa kupumua!!
Tunamshukuru Mungu sana sana kuwa kampuni
hii imehama chama chetu japo masalia yapo!!
Nakionea huruma chama kilichopokea kampuni
hii maana kama Mwalimu nyerere aliiogopa
kampuni hii iliakuwaje chadema wakaipokea Na
kuikumbatia? kwa masikitiko makubwa ni
kwamba chadema si chama tena chakuwatetea
wanyonge kama ilivyokuwa awali!!
kirusi hiki kitaitafuna chadema mpaka pale
itakapokuwa Na wazee wenye busara
waliyotayari kupinga kampuni hii
Dah.
 
Pumb@vu wewe. Wewe mfagizi wa lumumba toka lini ukaijua chadema. Funga bakuli lako lisitoe shombo.
Tatizo unawaza kuwa serikali ya sasa inafanya vizuri..kama kungekuwapo tume huru ya uchaguzi bila kuingiliwa na vyombo vya dola ccm ingeshatoka madarakani. uchaguzi uliopita ccm ilishindwa vibaya hata wewe unajuwa hivyo
Mkuu huamini kwamba anafanya vyema hadi sasa?
Hujapanda Bomberdier mkuu? Madawati huko kwenu bado ni shida? Watoto hawasomi bure?
 
Uchumi unapanda kwa asilimia 7.9 lakini lengo ni kufikia 7.2. Ha, ha, ha, ni Bosi wa Malaika huyo.
Mkuj sikiliza vizuri. Uchumi umepanda kwa asilimi 7.9 kwa quarter ila annual forecast ni 7.2. Hivyo ikienda kwa kasi hiyo kutakuwa na postive variance ya 0.7
 
Serikali imesema kuwa ina mambo mengi ya kushughulikia katika elimu na siyo mikopo ya elimu ya juu pekee, hivyo wanafunzi wanatakiwa kuwa wavumilivu.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mhandisi Stella Manyanya bungeni Dodoma, wakati akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Kilolo, Mh. Venance Mwamoto aliyetaka kujua hatma ya wanafunzi wa elimu ya juu wanaolalamika kukosa mikopo.

Mhandisi Manyanya amesema kuwa hadi sasa tayari awamu ya kwana ya fedha za mikopo imekwisha toka, na kwamba kilichosababisha ucheleweshwaji ni zoezi la uhakiki wa wanafunzi ili kupata wanafunzi wenye sifa sitahiki.

"Siyo kila muombaji wa mkopo atapata mkopo, mikopo hii itatolewa kwa walengwa pekee ambao ndiyo wahitaji, serikali inashughulikia mambo mengi katika sekta ya elimu na siyo mikopo pekee, kwahiyo pesa nyingine zinatumika kwenye mambo mengine kama vile ujenzi wa mabweni, maabara na miundombinu mingine"

Aidha Mhandisi Manyanya amewahakikishia wanafunzi kuwa tatizo la mikopo litamalizika ndani ya wiki hii huku akisisitiza kuwa mikopo hiyo itakuwa ni kwa walengwa pekee na siyo wanafunzi wote.

Kufuatia suala la mikopo hiyo kuanza kutikisa bunge katika kikao chake cha kwanza hii leo, mwenyekiti wa kikao hicho ameiagiza serikali kuandaa maelezo kuhusu sakata hilo.

Chanzo: EATV
 
Mimi naona afadhali ya chadema inayo ongozwa na vichwa vya watu 3 Lowassa, Sumaye, na Mbowe. Lkn hebu itazame CCM. Hiki ni chama kinachoongozwa na fikra za mtu mmoja nae ni Magufuri.
Tuseme kweli ni jambo gani linaloweza kufanyika nje ya magufuri? Yeye ndo amekuwa farsafa ya chama, chama hadi sasa hakuna muelekeo kinafwata anachosema Magu. Ni mbuge au kiongozi gani anaeweza kupinga kauri ya Magu? Chama kimefikia hatua ya kutokujua kesho Magu atasema nn, ni Sera gani inayofatwa, na badiriko gani litatokea. Ngoma yoyote anayopiga Magu,chama hucheza. Serikali ndo imegeuka kuwa msimamizi wa chama badala ya chama kuisimamia serikali. Magu ndie amekua chama, serikali, bunge, na mahakama. KWELI NYANI HAONI KUNDULE
Ndio maana hata Kinana kajionea upuuzi mtupu, kakaa kimya kawaacha Mwenyekiti na Sendeka wajikanyage kanyage. Katibu Mwemezi Nape na Naibu katibu mkuu Luhwavi wanajisomea magazeti tuu kufuatilia matukio ya hao comedian
 
  • Thanks
Reactions: bne
Kwani Binadamu hawezi kutubu na kubadilika?Lowassa n Sumaye waligundua kuwa hawako kwenye chama sahihi, kumbuku ukiwa kwenye chama unafata sera za chama si sera zako kama Furani anavyifata za kwake.....
Ukihama chama akili zinabadilika pia .....
 
Mpaka wakati wa utawala wa George Bush Junior Donald Trump alikuwa ni mwanachama mkubwa tu wa Democrat. Kwenye siasa haya ni mambo ya kawaida tu, yasikuumize sana. Kuna mwanasisa aliwahi kujiapiza hadi Mama yake mzazi iwapo atarudi ccm, lakini alirudi na akapewa usemaji mkuu wa chama.
Hoja si kuhama chama. Msigwa aliwatuhumu hawa wahamaji kwamba wana AKILI NDOGO. Je akili zao zimebadilika baada ya kuhamia CDM?
 
Mkuu huamini kwamba anafanya vyema hadi sasa?
Hujapanda Bomberdier mkuu? Madawati huko kwenu bado ni shida? Watoto hawasomi bure?
Hawa vijana wanaishia kutukana tu ukiwaambia ukweli.
 
Back
Top Bottom