Wabongo acheni kukariri maisha

Hivi kwa nini makanisani watu wanafuatilia sana mambo ya watu, halafu ndio wanaongoza kusengenya wenzao, yani shida tupu, hata mkeo unakwenda nae kanisani mwambie akae mbali na wapendwa.
Ni kawaida kabisa pale palipoonekana pasafi huwa pamefichwa uchafu mwingi sana na watu hutumia miavuli ya dini kujisafisha machoni pa watu.

Nikupe ushuhuda..... Muinjilisti na mchungaji walionifundisha mafundisho ya NDOA wote hawajielewi mchungaji ndio shetani mdogo fikiri mtu anakufundisha mambo mazuri ila yeye hatekelezi anadiriki kusema mbele ya usharika acheni mizigo yenu acheni dhambi acheni kutembea nje ya ndo ila yeye anachepuka na katibu wake hebu fikiri huo ukaribu hapo yaani humo humo kanisani unahubiri na humo humo unaanguka.

Muinjilisti nae anatufundisha ukaribu kwenye ndoa kuheshimiana anajiifia yeye na mumewe walivyo wafusi sahihi wa imani na yesu kristo ila nikaja kujua mumewe ni mlevi mavi akilewa anapaki mitaroni sasa mume wa muijilisti kweli akawe kwenye njia ya upotevuni inamaana hakuna imani hapo ni kujikinga kwenye mwamvuli wa dini
 
Uwakute Sasa wanahubiri aisee
 
Mkuu umetema madini flani ya kinyamwezi sana
 
Nilijua nimeandika mimi kumbe sio, tupo wengi na umeandika vyema sana kiasi sina la kuongeza...
 
Unachosema ni kweli, hakuna watu wanachakata kondoo kama hao jamaa, weka mke wako mbali asiwe na mazoea nao, akiwa mzuri mzuri kalio lipo, sura mashallah kaa kwa codes. hakuna cha mtume wala nabii hao wanachakata balaa.
 
kama ndo hivyo basi unapaswa umuweke wazi mwenzio kuwa wewe huna mpango kabisa wa kufunga ndoa ili na yeye ajuwe anaamua nini.

Maana nadhani kama angekuwa anaujua msimamo wako asingekuwa anakuhimiza hilo jambo
 
Mimi nmeishi na mwanamke miaka mitatu bila ndoa na sahv naona afadhali sijafunga ndoa maana mwanamke kawa jeuri hatare, na nmezaa nae ila namtaftia namna ya kuachana nae, maana mwanamke hataki kujishusha afu tukikosana kidogo basi anatoa matusi ambayo Mimi kama mwanamme siwezi kuyatamka namimi naona inapofikia nitampiga kitu ambacho nishaapishwa na mama yangu kamwe nisije kumpiga mwanamke ni heri kuachana nae
 
Una bahati sana, ungejua umefunga nae ndoa ndio ingekua imekula kwako, ungeteseka Hadi kifo kiwatenganishe, hapo unamvutia gap tuu la kumuacha
 
Ndoa inatambuliwa kijamii, kiserikali na kidini ndo kuna cheti cha ndoa, Mfano wew ukafariki ghafla na kuna mali mlichuna, ndugu watamkataaa mke wako na watachukua hizo mali, utaacha watt wako na mkeo wamekuwa watumwa, funga ndoa ndugu
 
Ujumbe wako n mzuri ila umeandika kihuni huni.

Kuna mambo yanaendelea huko makanisani na kwenye hizi dini ni aibu. Mtu wa kipato cha kawaida au cha chini utanyimwa kupewa huduma fulani kwa sababu fulani ila tajiri atapewa huduma hiyo hiyo bila kusita hata kama sababu ya kunyimwa ipo.
 
Unapoishi na mwenza bila ndoa ,,basi wote mnahesabika kama wazinzi.


Hata ukifa usingizini ukiwa na huyo mwenza wako unahesabika kama umekufa kwenye uzinzi ..

Nilichojufunza kuwa vijana wengi wa hovyo wanaogopa ndoa kwa sababu kuu 2..
-- majukumu
-- commitment..

Hakuna kitu kijana wa hovyo anaogopa kama kuwa na majukumu..
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…