Wakuu poleni na kazi. Niende kwenye mada, kuna jamii kubwa kwa sasa, wake kwa waume wamekuwa wakibeba mabegi migongoni, siyo shida wala hakuna neno, ni vizuri pia.
Ila, baadhi yao, wanapoingia ndani ya daladala hawayakulii namna ya kuyabeba, bado wanakuwa nayo migongoni na mbaya zaidi, konda anataka kusimama wawili wawili, hapo ndipo shida hutokea.
Wawili waliosimama halafu wamepeana migongo yenye mabegi, kivumbi chake si cha kitoto. Hali hiyo huwafanya kuinamia mpaka kwa abiria waliokaa kwenye siti ambao nao hunesa mpaka kulaliana.
Nashauri, tukiingia ndani ya daladala mabegi tuyashikie kwa chini ili kuondoa kero kwa wengine.
Na kama hoja ni ile kauli ya 'ndiyo usafiri wetu ilivyo' basi sawa, acha tuteseke tu.
Ila, baadhi yao, wanapoingia ndani ya daladala hawayakulii namna ya kuyabeba, bado wanakuwa nayo migongoni na mbaya zaidi, konda anataka kusimama wawili wawili, hapo ndipo shida hutokea.
Wawili waliosimama halafu wamepeana migongo yenye mabegi, kivumbi chake si cha kitoto. Hali hiyo huwafanya kuinamia mpaka kwa abiria waliokaa kwenye siti ambao nao hunesa mpaka kulaliana.
Nashauri, tukiingia ndani ya daladala mabegi tuyashikie kwa chini ili kuondoa kero kwa wengine.
Na kama hoja ni ile kauli ya 'ndiyo usafiri wetu ilivyo' basi sawa, acha tuteseke tu.