Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,234
Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, ametoa onyo kali na kupiga marufuku waandishi wa habari ambao hawana ithibati kutoripoti kabisa uchaguzi mkuu kwani kufanya hivyo ni kosa la kisheria.
Amesema kuwa ni kosa la kisheria kwa mwandishi wa habari kufanya kazi bila kuwa na kitambulisho maalum kilichotolewa na Bodi ya Ithibati, hasa wakati wa uchaguzi, adhabu yake ni faini ya kati ya shilingi milioni tano hadi milioni kumi au kifungo cha miaka mitatu hadi mitano jela.
Akizungumza katika mkutano wa wadau wa sekta ya habari na utangazaji kutoka Kanda ya Mashariki uliofanyika jijini Dar es Salaam, Kipangula amewaonya wanahabari wanaofikiria kutumia vitambulisho kutoka Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) wakati wa uchaguzi, akisitiza kuwa INEC watatoa vitambulisho hivyo kwa wanahabari wenye Bodi ya Ithibati tu.
Amesisitiza kuwa Bodi ya Ithibati itaendelea kushirikiana na taasisi nyingine kuhakikisha kuwa sheria hiyo inatekelezwa kikamilifu ili kulinda weledi na maadili ya taaluma ya uandishi wa habari nchini.
Amesema kuwa ni kosa la kisheria kwa mwandishi wa habari kufanya kazi bila kuwa na kitambulisho maalum kilichotolewa na Bodi ya Ithibati, hasa wakati wa uchaguzi, adhabu yake ni faini ya kati ya shilingi milioni tano hadi milioni kumi au kifungo cha miaka mitatu hadi mitano jela.
Akizungumza katika mkutano wa wadau wa sekta ya habari na utangazaji kutoka Kanda ya Mashariki uliofanyika jijini Dar es Salaam, Kipangula amewaonya wanahabari wanaofikiria kutumia vitambulisho kutoka Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) wakati wa uchaguzi, akisitiza kuwa INEC watatoa vitambulisho hivyo kwa wanahabari wenye Bodi ya Ithibati tu.
Amesisitiza kuwa Bodi ya Ithibati itaendelea kushirikiana na taasisi nyingine kuhakikisha kuwa sheria hiyo inatekelezwa kikamilifu ili kulinda weledi na maadili ya taaluma ya uandishi wa habari nchini.