Vyuoni huko - nani anamsaidia mwenzie?

WomanOfSubstance

JF-Expert Member
May 30, 2008
5,457
956
Huu msemo kuwa " wasichana/akina dada husaidiwa na akina kaka vyuoni" unatoka wapi?
Nijuavyo mimi kila mmoja awe msichana au mvulana hufuzu kuingia chuo baada ya kupitia mchakato.Hakuna njia ya mkato.Iweje akishafika chuoni basi akili zake hupotea hadi asaidiwe kufaulu?
 
Huu msemo kuwa " wasichana/akina dada husaidiwa na akina kaka vyuoni" unatoka wapi?
Nijuavyo mimi kila mmoja awe msichana au mvulana hufuzu kuingia chuo baada ya kupitia mchakato.Hakuna njia ya mkato.Iweje akishafika chuoni basi akili zake hupotea hadi asaidiwe kufaulu?

Nijuavyo mimi, watu wakiwa vyuoni huwa na vikundi vyao vya kujisomea na kila mmoja huweza kuchangia majadilino (discussion) kwa kadri alivyoelewa "topic" fulani ya somo husika. Na hapa haichagui msichana/mwanamke au mvulana/mwanaume, wote huchangia. Katika darasa langu la Bachelor kuna wasichana wawili walipata "First Class" (UDSM) na walikuwa vipanga kweli na si kwasababu walisaidiwa na wavulana. Kwa kifupi ni kuwa wote husaidiana.
 
Wenye mawazo muflisi na tegemezi ndo wanaingia chuo na akili hizo. Ila boys sometimes wanatumia gia hiyo kama ndio sehemu ya kupatia yale mambo mengine. Siunajua tena mambo yanaweza kuwa rahisi kama unakuwa karibu na mtu...hata kama hakutaki anaweza kukuonea huruma.
 
Inategemea huyu dada ameingiaje. Kuna wanaoingia kisiasa zaidi ili ku-equal idadi ya wavulana ktk fani husika.

Nakumbuka kuna mkakat flan nliwahi kuusikia wanafunzi wa kike walimwagma faculty ya engineering kwa fujo. Hawa walijiunga na chuo miezi kadhaa kabla wenzao wa mwaka wa kwanza waliochaguliwa kawaida hawajafungua chuo.
Lengo hapa lilikua kuwapiga msasa wadada hawa kabla ya chuo kufunguliwa.

Hebu mchukulie mdada alieingia ktk mpango huu wa 'ongeza idadi' tena engineering, what do you expect? Kutafuta mvulana (kumbuka hawa ndo wako wengi zaidi) ambaye atakua akimsaidia kimasomo.

Asante
 
Huu msemo kuwa " wasichana/akina dada husaidiwa na akina kaka vyuoni" unatoka wapi?
Nijuavyo mimi kila mmoja awe msichana au mvulana hufuzu kuingia chuo baada ya kupitia mchakato.Hakuna njia ya mkato.Iweje akishafika chuoni basi akili zake hupotea hadi asaidiwe kufaulu?

Yaani umenjibu swali ninalonikera mara nyingi. Huwa nahuzunishwa sana na dhana ya kuwa mabinti zetu wanapendelewa na wakufunzi wa kiume au kusaidiwa na vijana wa kiume. Tunasahau kabisa kuwa walifaulu darasa la saba, la kumi na mbili na la kumi na nne bila ya mkufunzi yeyote kuwapendelea, na bila mvulana yeyote kuwasaidia; wakienda ulaya huwa wanafaulu tu bila ya upendeleo wowote. Hii tabia ya kuwadhalilisha akina dada kuwa hawajitahidi inakatisha sana tamaa. Ni watoto wetu, ni dada zetu, ni mama zetu, hebu tuwape staha.
 
Inategemea huyu dada ameingiaje. Kuna wanaoingia kisiasa zaidi ili ku-equal idadi ya wavulana ktk fani husika.

Nakumbuka kuna mkakat flan nliwahi kuusikia wanafunzi wa kike walimwagma faculty ya engineering kwa fujo. Hawa walijiunga na chuo miezi kadhaa kabla wenzao wa mwaka wa kwanza waliochaguliwa kawaida hawajafungua chuo.
Lengo hapa lilikua kuwapiga msasa wadada hawa kabla ya chuo kufunguliwa.

Hebu mchukulie mdada alieingia ktk mpango huu wa 'ongeza idadi' tena engineering, what do you expect? Kutafuta mvulana (kumbuka hawa ndo wako wengi zaidi) ambaye atakua akimsaidia kimasomo.

Asante
Asante ndugu yangu.... hapo kwenye red hapooo! Kwani hao wasichana wachache ambao ni vichwa hawawezi kuwasaidia wenzao hadi watafute wavulana?...hebu dadavua zaidi...
 
Yaani umenjibu swali ninalonikera mara nyingi. Huwa nahuzunishwa sana na dhana ya kuwa mabinti zetu wanapendelewa na wakufunzi wa kiume au kusaidiwa na vijana wa kiume. Tunasahau kabisa kuwa walifaulu darasa la saba, la kumi na mbili na la kumi na nne bila ya mkufunzi yeyote kuwapendelea, na bila mvulana yeyote kuwasaidia; wakienda ulaya huwa wanafaulu tu bila ya upendeleo wowote. Hii tabia ya kuwadhalilisha akina dada kuwa hawajitahidi inakatisha sana tamaa. Ni watoto wetu, ni dada zetu, ni mama zetu, hebu tuwape staha.
Kwenye red.... nimekuwa nasikia na kusoma kuhusu hili na likanikera sana.. kitu watu wanasahau... kuna akina dada ambao nao wamejaaliwa kama kina kaka... je, akina kaka dhaifu huwatafuta wawasaidie au huenda kwa wanaume wenzao?

Kwenye blue...huko kote walibahatisha?
 
........Wanaume wanaolalamika kwamba wanawasaidia wadada huko vyuoni ni uzushi mtupu.
Mtu hadi kufika chuo ni juhudi za mtu mwenyewe binafsi, iweje leo kafika chuoni asubiri msaada wa mwanaume?

Ninavyojua mimi vyuoni kuna makundi ya discussion na vile vile watu mnaweza kusaidiana kimawazo iwe jinsia moja au tofauti. Ila kuna baadhi ya wanaume kama mlikuwa mnafanya discussion pamoja halafu akakutaka ili uwe mpenzi wake basi ukimtolea nje tu anaanza kuleta story hizi..........ohhh nilikusadia kukupa materials, mara nilikusadia kukufundisha topic hichi mara kile ilimradi tu apate kulalamika.

Kuna wadada wengi tu vipanga kweli kweli huko vyuoni, wanawasaidia wanaume kimawazo lakini huwezi kuta hata siku moja wanalalamika. Hivyo wanaume ondoeni hii kasumba ya kulalamika hapa kwamba ulimsaidia mdada..........tenda wema uende zako usingoje shukrani.
 
What is the 'cutoff' point for admission: is it the same for both males and females? Or is there any group that is given 'affirmative action'? Why? Why not?
 
Asante ndugu yangu.... hapo kwenye red hapooo! Kwani hao wasichana wachache ambao ni vichwa hawawezi kuwasaidia wenzao hadi watafute wavulana?...hebu dadavua zaidi...

WoS nadhani nature yenyewe inajieleza, like charges repel, unlike charges attract. Hahaha...

Hivi do u know how welcoming boys are?! Especially to a woman/girl in need!

Nadhani dada utakua shahidi wangu kua wanawake kwa wanawake bwana kufuatana kwa kwa ajili ya kupeana msaada wenyewe kwa wenyewe ni ngumu sana. Ni rare kwa kweli, sijui labda nyie wenzetu mnaelewa sababu.

Kwa kweli hii ni experience yangu wakati nasoma.
 
........Vile vile kuna tabia naona siku hizi inashamiri sana, mwanamke/mdada akiwa close tu na kiongozi wa siasa mwenye jinsia ya kiume basi mengi yanasemwa.......Ohhh anataka kupewa ubunge/uwaziri.
mwanamke huyo huyo akipewa position nzuri kazini basi watu wanaanza kuongea haswa wanaume. Je mwanamke ni mtu wa kubebwa kila mahali? Huyu kiumbe mwanamke hastahili position za juu ofisini hadi apendelewe?
Imefika kipindi inabidi tukubali tu kwamba mwanamke anaweza kufanya kitu kikubwa zaidi kuliko mwanaume. Kuna wanawake wana akili na wanajua kutumia akili zao kuliko wanaume.
 
........Vile vile kuna tabia naona siku hizi inashamiri sana, mwanamke/mdada akiwa close tu na kiongozi wa siasa mwenye jinsia ya kiume basi mengi yanasemwa.......Ohhh anataka kupewa ubunge/uwaziri.
mwanamke huyo huyo akipewa position nzuri kazini basi watu wanaanza kuongea haswa wanaume. Je mwanamke ni mtu wa kubebwa kila mahali? Huyu kiumbe mwanamke hastahili position za juu ofisini hadi apendelewe?
Imefika kipindi inabidi tukubali tu kwamba mwanamke anaweza kufanya kitu kikubwa zaidi kuliko mwanaume. Kuna wanawake wana akili na wanajua kutumia akili zao kuliko wanaume.
Asante Pretty kwa mawazo na maneno yako mazuri...
mimi nitaongezea na kusema kuwa.... uwezo wa mtu au kutokuwa nao ni kitu binafsi na siyo cha kiujumlajumla.... haina maana kuwa wanawake wote ni vilaza..au kuwa wanaume wote basi ni vichwa. Sote tumeshashuhudia uwezo tofauti wa hawa viumbe. Nadhani maneno haya ni sehemu ya watu kujifurahisha na kujaribu kujipa moyo kuwa jambo hili linawezekana au haliwezekana ( filosofia zaidi).Kwa wale wenye watoto nadhani watanielewa.... malezi huchangia katika kufunua au kufunika vipaji, akili, maarifa na uwezo wa watoto - wawe wa kike au wa kiume.
Kweli wapo wenye kupenda njia za mkato mkato... huendekeza starehe zaidi ya kilichowapeleka chuoni na huweza kutumia mbinu zozote kuhakikisha wanafaulu. Haijalishi ni wanawake au wanaume. Kuna wanaume/ au vijana wa kiume hutoa hadi rushwa ya pesa ili wanunue mitihani wafaulu. Hatujazungumzia wale wenye kutegemea wasichana wenye uwezo wawatafunie ( kuchambua maswala mazito) ili wao wameze kwa kutayarisha madesa!
Sehemu za kazi utawaona wale wababaishaji waliofaulu kimkandamkanda....hawamudu majukumu yao... ni wepesi kujipendekeza na kutafuta kupendwa na wakubwa ili wapewe nafasi - hii haijalishi mtu ni mwanamke au mwanaume.Hawa wakijikuta hawana kazi utawaonea huruma maana hupata aibu mitaani .... hawajazoea kuogelea bila boya la kuelea lol! KAAAZI KWELI KWELI!
 
Kulikuwa na akina dada pale FoE ambapo katika jitihada zao za kujiunga katika makundi ya Wanaume ili waweze kushiriki katika discussion mbali mbali ili kufanya vizuri katika assignments na mitihani Wanaume walikuwa wanawapiga chenga kwa kuwaona ni vilaza, basi wakaamua kuwa na kundi lao wenyewe na walikuwa wanafanya vizuri kuliko Wanaume wengi. Hakuna ukweli wowote kwamba kila mwanamke aliyebahatika kufika chuoni ni kilaza wengi wana uwezo mkubwa tu wa kimasomo wa kuweza kushindana na hata Wanaume vipanga na pia kufanya vizuri kuliko Wanaume wengi.
 
i studies abroad wote tulikuwa tunasaidiana girls and boys... to be honest men can be more helpful than women sometimes wanawake wanakuwa wanaringa mapozi halafu wivu sasa ndo usiseme...
 
i studies abroad wote tulikuwa tunasaidiana girls and boys... to be honest men can be more helpful than women sometimes wanawake wanakuwa wanaringa mapozi halafu wivu sasa ndo usiseme...
Asante kwa mchango wako. Hapo penye red --- huo wivu unatokana na nini au inakuwaje maana kama ni kwenda abroad wote mmekwenda kivyenu vyenu....hakuna alieyembeba mwenzie....
kusaidia au kutosaidia ni uamuzi wa mtu na kila mtu yuko huru katika hili.. nikikataa kukusaidia utasemaje nina wivu?Hapo juu nadhani BAK kasema kuna wavulana walikuwa wanawakacha wasichana kuwasaidia..ina maana hawa wakaka walikuwa wana wivu?
( usikwazike ndugu..nachangamsha mada ndio maana nauliza maswali haya)
 
Ukumbi wenu leo kina Dada ,jifaraguweni mtakavyo yatoweni yaliyomo moyoni mwenu .
 
Huu msemo kuwa " wasichana/akina dada husaidiwa na akina kaka vyuoni" unatoka wapi?
Nijuavyo mimi kila mmoja awe msichana au mvulana hufuzu kuingia chuo baada ya kupitia mchakato.Hakuna njia ya mkato.Iweje akishafika chuoni basi akili zake hupotea hadi asaidiwe kufaulu?

Si hivyo tu, wengine tulisikia wakati tukisoma pale mlimani kuwa akina dada wengi wanaishi style ya Mafiga Matatu:

1. BF wa Chuo anyemsaidia Masomo na Kuhakikisha anafaulu
2. Sugar Daddy wa Kumpatia Mahitaji yake
3. BF wa Kweli Chaguo la Moyo wangu.

Akikosa No. 1: Basi Lecturer ataingiwa kinamna namna . . . Sijui simulizi hizi zilitoka wapi?
 
Upande wangu mi nadhani tatizo akina dada wakiwa na akili nyingi wanakuwa wachoyo waku share vipaji vyao mara nyingi, labda kwa ma best wao tu.

Whereby akina kaka wengi atuna utamaduni huo, na ukiwa natabia hizo si jambo la ajabu kupewa label, hivyo mara nyingi utakuta makundi ya makaka wakisoma pamoja. Since akina dada wengi ni calculative kushinda akina kaka (again my opinion) huwa hawajali who they look for to get help, lao liende. Na hii mara nyingi hu changia average students (akina dada) kuingia makundi ya makaka kwenye revision not to mention makaka huongeza bidii kwa kuwafuruhisha akina 'hawa' wakiwa na agenda zao nyingine na wao.
 
Upande wangu mi nadhani tatizo akina dada wakiwa na akili nyingi wanakuwa wachoyo waku share vipaji vyao mara nyingi, labda kwa ma best wao tu.

Whereby akina kaka wengi atuna utamaduni huo, na ukiwa natabia hizo si jambo la ajabu kupewa label, hivyo mara nyingi utakuta makundi ya makaka wakisoma pamoja. Since akina dada wengi ni calculative kushinda akina kaka (again my opinion) huwa hawajali who they look for to get help, lao liende. Na hii mara nyingi hu changia average students (akina dada) kuingia makundi ya makaka kwenye revision not to mention makaka huongeza bidii kwa kuwafuruhisha akina 'hawa' wakiwa na agenda zao nyingine na wao.

Yeah nadhani ni ile kasumba ya " give and take" sasa mtu akiona mwenzie ni kupe tu anaachana nae, kama ulivyosema inawezekana wakaka wanakuwa wavumilivu kwa maana anatarget kitu kingine in reward japokuwa sio kwa kesi zote.
Kwa kuongezea tu mi hadi nafika kidato cha sita discussion groups zangu zilikuwa ni wadada tu na walikuwa capable sanaa.
Nilipokuwa chuo nikawa nashift wakati mwingine nadiscuss na wakaka wakati mwingine ni wadada tu na hakukuwa na tofauti sana.
 
Asante kwa mchango wako. Hapo penye red --- huo wivu unatokana na nini au inakuwaje maana kama ni kwenda abroad wote mmekwenda kivyenu vyenu....hakuna alieyembeba mwenzie....
kusaidia au kutosaidia ni uamuzi wa mtu na kila mtu yuko huru katika hili.. nikikataa kukusaidia utasemaje nina wivu?Hapo juu nadhani BAK kasema kuna wavulana walikuwa wanawakacha wasichana kuwasaidia..ina maana hawa wakaka walikuwa wana wivu?
( usikwazike ndugu..nachangamsha mada ndio maana nauliza maswali haya)

Ndiyo ukikataa kunisaidia kwenye elimu ntakuona una wive, Unapokataa kumsaidia mwenzio kwenye elimu inakuwa una wivu manake unadhani ukimsaidia mwezio atakuwa better than u... which is not true when u help others by sharing information u only help urself to understand the subject more... .. kama huo sio wivu ndio nini sasa...

Hata makazini watu wengine hawapendi kuwafundisha wenzao kazi kwa kuogopa watachukuliwa cheo chao... I always tell my colleagues that if you want to grow in ur career then you must teach others, otherwise u will stay in ur place forever...

na wale wakaka hapo juu walikuwa wanawivu if not intimidated...

hujanikwaza dada bring it on:)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom