Vyombo vya Habari Redio na TV havina mpango na kumbukizi ya kifo cha John Magufuli

Vyombo vya Habari Redio na TV havina mpango na kumbukizi ya kifo cha John Magufuli

Nkarahacha

Member
Joined
Oct 3, 2023
Posts
25
Reaction score
47
VItuo vya Tv na Redio ukitazama au kusikiliza huwezi kusikia kiashiria chochote kuhusu siku ya leo ikiwa ni kumbukumbu ya miaka minne ya kifo cha John Pombe Magufuli ila mitandao ya kijamii kila sehemu lazima ukutane na taarifa hii.

Serikali nayo kama haijui kinachoendelea labda kiongozi mmoja mmija kwa kujiongeza ndo anaamua kumkumbuka kwa namna yake na wengine wameenda chato kwenye Misa.

R.I.P JPM Mwamba.

Screenshot_2025_0317_130827.png
 
kama ccm wenzake wamempotezea wao akina nani?ugali mtamu ila sio wa jela.hilo ni funzo watakusifu ukiwa upo au una kitu ukiondoka au vikiondoka WATAKUSAHAU
 
Maisha yanaendeshwa kichawa. kama mama angetoa kauli ungesikia mapambio.

Ingebadilika kutoka kumbukizi ya Magufuli na kuwa Kumbukizi Ya Mama kwa Magufuli.
 
Kwenye katiba ya Tz kuna sehemu yeyote inayo sema kuwa kiongozi akifia madarakani basi atengewe siku maalumu ya kukumbukwa kitaifa?
Na vilevile kwenye Katiba hakuna sehemu iliyokataza Kiongozi aliefia madarakani asitengewe siku maalumu!!
 
Magufuli ndiyo Rais wa Kwanza kufariki akiwa madarakani,wenzake walikua tayari ni wastaafu!!
Rais akifia madarakani ndiyo anaendelea kuongoza hata akiwa kaburini hadi atengewe siku maalum ya kitaifa ya kukumbukwa?

Hata waliokufa wakiwa wamestaafu bado wana mchango sawa na aliyefia madarakani kwani wote hadhi yao ni moja (Marais).
 
Na vilevile kwenye Katiba hakuna sehemu iliyokataza Kiongozi aliefia madarakani asitengewe siku maalumu!!
Kwani ni ajabu sana Rais kufia madarakani?

Ama alikuwa na makubaliano na Mungu lazima astaafu ndiyo afe hivyo kitendo cha kufa akiwa madarakani ni kukiuka makubaliano hadi iwe kitu cha kushangaza?
 
Kwani ni ajabu sana Rais kufia madarakani?

Ama alikuwa na makubaliano na Mungu lazima astaafu ndiyo afe hivyo kitendo cha kufa akiwa madarakani ni kukiuka makubaliano hadi iwe kitu cha kushangaza?
Punguza chuki kwa Marehemu, maisha hayataki hasira!!
 
Waliojazana huko wengi walizungusha darasani huo ndio ukweli!
Alafu kutwa kujipiga selfie kwenye SGR....na kukenua tu wakiangalia bwawa la Mwalimu Nyerere....
R.I.P Mzilankende
 
Kwani magufuri ndo rais wa kwanza kufariki hapa tz ,kwa nn magufuri na si wengine?
Magufuli alikuwa rais bora ndani ya bara la Africa.
Kakaa ikulu muda mfupi sana lakini atakumbukwa kwa miaka mingi sana!.
 
Back
Top Bottom