Dada yangu pole sana kwa matatizo yaliyokupata.Habari wakuu zangu nawasaliimu sana.
Naombeni sanakama kichwa cha habari kinavyojieleza vyeti vyangu vyote vimeungua moto nzungumzia kuanzia form 4 mpaka chuo kikuu sasa nashindwa nianzie wapi kuvipata.Nawaomba mnifungue macho jamani nianzie wapi yeyote aliyewahi kutana na kitu hii anishauri wapendwa.
Je kuna uwezekano wakuvipata upya ?
nawasilisha?
Scanning haitoshi, hiyo ni nakala kama zilivyo nakala nyingine tu. Wenzetu wanaojua umuhimu wa cheti wanadiriki hata kuweka benki kama pesa ili viwe kwenye usalama. Lakini wabongo hatujali sana sehemu tunazoweweka nyaraka muhimu kama hizo mpaka zitakapopotea au kuliwa na mchwa ndiyo tunajua kumbe kilikuw akitu muhimu sana.tujifunze kwa makosa jamani tuwe tuna SCAN vyeti itakua kidigitali zaidi
Kama ni cheti kilichopatikana nje ya nchi mamlaka husika iliyotoa cheti hicho itahusika.Asante sana kipenzi kaka yangu mungu akubariki kwa muda na nguvuuliyotumia kunishauri.nin ahili tena
je cheti cha elimu ya juu nilisomea nje ya tanzania nitafanyaje sasa.hizi hizi police report zitanisaidia
Sheria gani ? tutajie tafadhali
Asanteni sana kwa ushauri na mawzo yakinifu lakini pi aninayo soft copy kwenye emails zangu.
yap,tena hiyo ni mbinu nzuri sana ya kuhfadhi vyeti,zingatia,lamination usifanye kwani hairuhusiwi kisheria.
Dada yangu pole sana kwa matatizo yaliyokupata.
Wote walioshauri hapo juu wapo sahihi. lakini zifuatazo ndiyo taratibu fupi zitumiwazo na Baraza la mitihani la Tanzania:
-Nenda polisi ukatoe taarifa ili upatiwe "Police Loss Report"
-Nenda ukatangaze kwenye gazeti la serikali (Habari leo, Daily News), gharama zake huwa ni kati ya Tsh 20,000-25,000. Hii ni mhuhimu incase ikatokea mtu aliokoa au aliokota mzigo/kifurushi kilichokuwa na vyeti vyako wakati wa tukio basi atakurudishia.
-Peleka Baraza la Mitihani nakala halisi ya Police loss Report na Ukurasa mzima wa gazeti lenye tangazo la upotevu wa Vyeti/cheti (Kwa vyeti vya sekondari tu). Unatakiwa kuwa na kitambulisho (ID) chochote amacho ni hai (validi) pamoja na picha moja ya Passport size kwa kila cheti kilichopotea. Ukishakamilisha nyaraka zote hizo tapewa fomu maalumu pale Baraza la Mitihani ambayo utatakiwa kuijaza ili upatiwe "Statement of Results" na sio cheti. Kumbuka hii SOR hutapatiwa wewe mkononi bali itatumwa kule ambako utataka kukitumia cheti/vyeti hivyo kwa wakati huo, baada ya kulipia benk kwenye Necta acc. Tsh 10,000 kwa njia ya rejesta kama ni ndani ya nchi.
Kumbuka cheti hutolewa mara tu, kuanzia sasa utacheza na SOR mpaka uzee wako. Taarifa muhimu unazotakiwa kuwa nazo ni Namba yako ya Mtihani kwa mwka husika uliofanyia mtihani wako na aina ya mtihani uliofanya kama ni CSEE au ACSEE.
Mkuu hiyo ni kweli kabisa, kuna siku nilienda pale Baraza kupata huduma,cha ajabu nilibaini karibia robo yawateja wote wa siku walikuwa wanaomba vyeti vipya, walipokuwa waliulizwa sababu kila mmoja alikuwa akitoa yake, huyu moto, yule kaibiwa, mwingine mafuriko ilimradi ni wengi sana.Maelezo hapo juu ni kweli kabisa, nilikumbwa na Tatizo kama la Nivea na nimeendelea kutumia utaratibu hapo juu,
Kitu cha Nyongeza ni kuwa utatakiwa kuwa na Barua kutoka Secondary ulizosoma kutoka kwa wakuu wa shule hizo kuonyesha kuwa ulisoma pale. Barua hizo zinahitajika na watu wa Baraza la mitihani
Pole sana Nivea, kimsingi usiwe disapointed maisha/Professional Career yako itaendelea; ukienda balaza la mitihani utagundua kuwa hili swala linawakumba watu wengi kwa namna tofauti tofauti.
Mkuu hiyo ni kweli kabisa, kuna siku nilienda pale Baraza kupata huduma,cha ajabu nilibaini karibia robo yawateja wote wa siku walikuwa wanaomba vyeti vipya, walipokuwa waliulizwa sababu kila mmoja alikuwa akitoa yake, huyu moto, yule kaibiwa, mwingine mafuriko ilimradi ni wengi sana.
Sio siri mkuu kuna risk nyingi sana, kwa sisi wa uswazi mende wanaweza kuvigeuza toilet na dinner au madogo wanaweza kufungia vitumbua ikala kwetu. Kama mbwai na iwe mbwai mi sijaacha hata kimoja vyote viko laminated. Sheria zao za kuombea rushwa wapeleke mbele huko.
Asante sana kipenzi kaka yangu mungu akubariki kwa muda na nguvuuliyotumia kunishauri.nin ahili tena
je cheti cha elimu ya juu nilisomea nje ya tanzania nitafanyaje sasa.hizi hizi police report zitanisaidia
ndugu
zangu kwa hili la
lamination msidanganywe...mimi vyeti vyangu vyote ni laminated, na
nimetipia sehem nying wkt natafuta kaz, ikiwepo mahakamani, na mwisho
nilipata kazi serikalini kwa kupitia procedure zote nikiwa na vyeti
vyangu laminated bt sijawahi hata kuulizwa badala yake nilikua nasifiwa
kua najua kutunza vyeti.