Vyama vya upinzani jifunzeni kutumia unyanyasaji mnaofanyiwa kwa faida yenu - tumieni mahabusu kwa kuhamasisha maelfu kukamatwa dunia yote ione!

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Mara nyingine ili Magufuli na serikali yake waelewe kwamba wanafanya unyanyasaji usiokubalika kwa vyama vya upinzani, inatakiwa vyama vya upinzani waje na namna ya kutumia unyanyasaji huo kwa faida yao wenyewe. Wafuasi wa vyama vya upinzani wanapaswa kuelewa siku zote wale wanaopigania haki zao wasitegemee kwamba watapewa haki hizo kwenye sahani ya dhahabu. Historia imeonyesha hivyo.

NI wazi kwamba watu wa vyama vya uinzani mnaonewa sana, na ili msikilizwe anzisheni kampeni zenye kulenga kutumia unyanyasaji mnaofanyiwa kwa faida yenu. Imefikia mahali ambapo mnapaswa kufanya dunia yote ijue mnachofaniwa na soon or later dunia nzima itawasikililiza. Hiyo ndio dawa ya serikali ya Raisi Magufuli na CCM dhidi ya uonevu mnaofaniwa.

Tatizo ni kwamba wafuasi wa vyama vya upinzani mmeacha viongozi wenu wawe ndio chambo cha kunyanyaswa, kufungwa nk. Acheni tabia ya kuwatumia viongozi wenu kuwa ndi wawe wa kukamatwa kila siku. Wala msifanye uhalifu - fanyeni mambo katika masses ambayo hayana mshiko kufunguliwa mashitaka.

Kama mkikusanyika mkutano wa siasa polisi wakaja msikimbie. Mnapokuwa katika umati polisi wakapiga mabomu mkaanza kukimbia hapo ndipo wanapowashinda. Polisi wakija laleni chini wote. Acha wapiga picha waionyeshe dunia mnapigwa marungu mkiwa mmelala chini tuone Magufuli atafika wapi. Hao watu wanaowaita mabeberu watawafanyia kitu mbaya tu maana hawataki ujinga kama huo. Watawapiga kiasi, lakini hawatawaua kwa maelfu, wekeni hilo kichwani.

Wakiwakamata leo kesho tena fanyeni hivyo hivyo, na kesho kutwa na kesho yake. Wakimwaga ugali mwageni mboga.

Hamuwezi kubadili mfumo wa unyanyasaji mnaofanyiwa kwa kuwaweka viongozi wenu mbele kuwa watu wa kuwawakilisha katika kunyanyaswa na kuwekwa ndani. Tumieni huku kuwekwa ndani kama namna ya kupinga kuwekwa ndani . Someni historia za mikakati ya kudai haki na jifunzeni katika hayo. Tatizo ni kwamba serikali ya Magufuli na CCM wanatumia uoga wenu wa mahabusu kuwagawanya na kutia ndani mahabusu mtu mmoja mmoja.

Jifunzeni kutumia vyombo vya habari vya nje kuionyesha dunia unyanyasaji mnaofanyiwa. Mnapoitisha mikutano toeni taarifa kwa vyombo vya habari vya ndani na nje - CNN, BBC, Al Jazira, Sky News, DW etc. Waambieni kinachotarajiwa kutokea ili wajiandae vema kutoa taarifa ya matukio kamba hata hayajafanyika. Hamuwezi kubadili mfumo wa unyanyasaji mnaofanyiwa kwa namna ileile mliyotumia kwa miaka karibu mitano sasa.

Nyie ndio mnaendelea kuumizwa. Sasa ni wakati wa kuja na mkakatai tofauti, na hasa sasa tunapoelekea kwenye uchaguzi. Kama hawataki kuwasikiliza mnapotumia ustaarabu, dawa ni kufanya kilicha haki yenu kwa kulazimisha, na tuone hizo mahabusu wanazowatisha nazo kama zitawasaidia. Kumbukeni haumwezi kusikilizwa kwa dunia kwa kutumia barua.

Imefikia mahali ambapo mambo mnayofanyiwa na serikali ya CCM chini ya Magufuli na vyombo vyake vya dola yanakera hata sisi tusio na vyama vya siasa. Enough now. Nyie ni Watanzania wenzetu. Kosa lenu nini hasa hadi mfanyiwe yote haya, kuwa wapinzani wa CCM?

1592991571630.png

Hili halivumiliki wala kukubalika tena! Ni lazima kulibadili, kwa namna moja au nyingine
 
Vyama vya siasa vivunje sheria wakulaumiwa awe Magufuli !

Magufuli anaonewa sana na upinzani sababu amezidi kuwadekeza
Hamna kuvunja sheria hapa. Magufuli na CCM yake wanawaonea sana watu wa upinzani kwa kisingizio cha kuvunja sheria, na watu wote wenye akili wanaona hilo. Serikali inafanya propaganda kwamba wapinzani wanavunja sheria na kutumika na mabeberu hadi watu sasa wameanza kuamini, pamoja na wewe.

Magufuli na CCM wanavunja katiba na kutumia uvunjaji katiba kwa kulaumu wapinzani kuwa wanavunja sheria. Angalia, kwanza kama raisi unavunja katika kwa kuzuia haki ya vyama vya kisiasa kufanya mikutano, wakifanya mikutano unasema wamevunja sheria. Ujinga gani huo mtu mwenye akili ataukubali?

Enough sasa. Hii nchi ni ya Watanzania wote, sio CCM peke yao. Kama CCM hawawezi ushindani wa kisiasa waache siasa
 
Kwa sasa haiwezekani. Tusuburie miaka kadhaa ijayo. Sahvi watu hawako na tabu ya kuwafanya waingie barabarani.
 
This is super thread. Hivi ndiyo inatakiwa - kama ilivyokuwa George Floyd mass response.
Somebody has to tell these people wanahitaji kutafuta mkakati mpya wa kudai haki zao. Wanatia huruma sana. Kina Zitto wamesafirishwa usiku gari la wazi, kwa kosa gani hasa? Hata majambazi wauaji hawafanyiwi mambo haya.

Kina Lissu hadi leo wamekuwa wageni katika nchi za nje - kosa lao nini hasa, kumwambia Magufuli hapa unakosea tufanye kitu tofauti? Wat wa CCM wanatukana utafikiri mimba zao zilitungiwa kwenye vilabu vya pombe za kienyeji, hadi ndani ya Bunge. Hivi upinzani wanadhani Raisi Magufuli na CCM wataanza kuheshimu watu wengine kwa kuandika barua World Bank?
 
Kwa sasa haiwezekani. Tusuburie miaka kadhaa ijayo. Sahvi watu hawako na tabu ya kuwafanya waingie barabarani.
Mie nadhani kwa sasa kuelekea uchaguzi ni perfect timing wanaweza kuitumia. Na kama ni kweli Magufuli na CCM wamehusika na kuondoka kwa mabalozi wa Uingereza na Marekani even better. Mara nyingine desparate times call for desperate measures. Upinzani kwa sasa wako kwenye desperate times. Waache wasemwe wanatumia "mabeberu", it is justified ili kukomesha kunyanyaswa na kuonewa kwao.
 
Global influencing media zifikiwe na wawe na connection na contacts nazo... Mfano CNN, Al Jazeera, BBC , sky News, RT Today na nyinginezo. Hiyo ndio njia pekee ya kuonesha Walimwengu tunavyoongozwa na kutawaliwa na ccm na madhambi yote tunayofanyiwa pasipo haki...
 
Jaribu hata kufanya vurugu nyumbani kwako utafikiwa popote pale
Mkuu, wala hawahitaji kufanya vurugu. Na believe me, watakachofanya ni much better kuliko kinachofanyika nchi nyingine pale ambapo wapinzani wanakuwa forced kuchukua silaha na kuingia msituni.

Kumbuka huko nyuma chini ya Raisi Nyerere, ilifikia mahali tuliwaunga mkono kikundi cha Biafra katika serikali ya Nigeria kuchukua silaha dhidi ya serikali ya Nigeria. Kuwaambia wapinzani wakubali kukamatwa kwa kufanya mass movements sio measure desparate kiasi hicho. In fact ni measure ya amani inayokubalika duniani kote.
 
Sijui kwanini na hisia Maxence Mello atatafutiwa kosa hapa kabla ya uchaguzi

Mungu aepushie mbali
 
Nimekupa Like...bahati mbaya pia na sisi Watanzania ni watu wa hovyo tunavunjiwa haki zetu na nchi imehodhiwa na watu wachache sisi tunaona poa..aibu yetu
 
F2E9435B-A822-4673-B7D7-607F5B8C4499-14664-00000FFD67819263.jpg

FB5850D4-F0FE-465A-9989-FB3A7B52A6DB-14664-00000FFD4DC18833.jpg

Hii ndio tabia yao hasa huku Zanzibar kipindi kama hiki , ikifika saa moja usiku ukae ndani ufunge na Geti usisubutu kufungua, na mchana kama huna shughuli maalum kaa nyumbani, ndio Zanzibar, kipindi hiki huwa kama hell ,
 
Mie nadhani kwa sasa kuelekea uchaguzi ni perfect timing wanaweza kuitumia. Na kama ni kweli Magufuli na CCM wamehusika na kuondoka kwa mabalozi wa Uingereza na Marekani even better. Mara nyingine desparate times call for desperate measures. Upinzani kwa sasa wako kwenye desperate times. Waache wasemwe wanatumia "mabeberu", it is justified ili kukomesha kunyanyaswa na kuonewa kwao.
Wananchi bado hawana mwamko. Maana hakuna cha kupoteza. Maslahi ya wengi bado hayajaguswa. Na uoga bado mwingi.
 
Na wana Ccm wataandamana kupinga maandamano yenu
Mkuu, wala hawahitaji kufanya vurugu. Na believe me, watakachofanya ni much better kuliko kinachofanyika nchi nyingine pale ambapo wapinzani wanakuwa forced kuchukua silaha na kuingia msituni.

Kumbuka huko nyuma chini ya Raisi Nyerere, ilifikia mahali tuliwaunga mkono kikundi cha Biafra katika serikali ya Nigeria kuchukua silaha dhidi ya serikali ya Nigeria. Kuwaambia wapinzani wakubali kukamatwa kwa kufanya mass movements sio measure desparate kiasi hicho. In fact ni measure ya amani inayokubalika duniani kote.
 
Back
Top Bottom