Vodacom wamevujisha taarifa zangu(?) - Kuweni makini na matumizi yenu ya Simu

Status
Not open for further replies.
Yaan ndugu unaweza ukashtakiwa bila sababu maana umeandika taarifa za kulichafua kampuni bila hata kufikiria kwasababu umemuuliza baba mwenye nyumba kakataa umeconclude na kupost kwa social media hivi....unajua athari anazoweza pata vodacom kwa hii post...How sure ni Vodacom 100% na sio huyo baba mwenye nyumba....TAKE CARE USIKURUPUKE.
Why isiwe Vodacom?
 
Kwanza kabisa naomba kuwasalimu wote,

Baada ya hapo kama kichwa cha uzi kinavyojieleza naomba kueleza jinsi ilivyokuwa hadi mimi kufikia hatua ya kusema kuwa VodaCom wamevujisha taarifa zangu za mawasiliano

Leo majira ya saa nane mchana, niliwasiliana na mwenye nyumba wangu kuhusu tatizo la shoti ya umeme hapa nyumbani, kwanza nilipigia simu hakupokea, nikajua huenda amebanwa na shughuli zingine hivyo nikamtumia SMS ili atakapoiona anitafute, katika sms hiyo nilieleza kuhusu tatizo lililopo.

Baada ya kama dakika 10-15, nikapokea simu (naomba namba iliyonipigia niihifadhi) huyo aliyenipigia akanijulisha kuwa yeye ni fundi umeme ameagizwa aje kutatua tatizo lililopo hapa nyumbani, kwa hiyo nikamwambia sawa nitamsubiri, na hivyo akanihakiishia kufika hapa nyumbani baada ya muda mfupi, lakini ikabidi nimtafute mwenye nyumba kuthibitisha taarifa hizo maana sikuweza kuaminin kama mwenye nyumba amewasiliana na fundi moja kwa moja bila kunipigia mimi nimweleze hali ya tatizo,

Sasa baada ya kuwasiliana na mwenye nyumba akakataa kuwa yeye hajaongea na mtu yeyote kuhusu suala la umeme zaidi ya kupokea sms ambayo mimi nimemtumia, lakini pia mimi sikuwasiliana na mtu yeyote zaidi yake kuhusu suala la umeme lililotokea nyumbani.

Hivyo moja kwa moja nikapata wasiwasi kuwa mawasiliano hayo yamevujishwa na mtandao wa simu ninaotumia (VODACOM), baada ya hapo nikapiga simu huduma kwa wateja kuwaeleza kuhusu malalamiko yangu hayo hata hivyo walichoweza kunijibu hakikuwa na mashiko, kwa kuwa alinijibu tuu kwa kifupi kuwa wao hawana uwezo wa kuona taarifa za mtumiaji wa mtandao wao

Lakini pia kama si VODA waliovujisha mawasiliano haya basi miundombinu yao haina uwezo wa kuzuia wadukuzi wa taarifa za wateja

pia, nikapata wasiwasi mkubwa kuhusu uvujaji wa taarifa zetu watumiaji wa mitandao, kwa kuwa ikiwa taarifa yangu ndogo kama hiyo imevuja, najiuliza swali Je, ni watu wangapi wametapeliwa kwa sababu hii, ni watu wangapi wamevamiwa kwa kuvuja kwa taarifa zao za safari, fedha, biashara n.k,

Tutawezaje kuwa salama kama mitandao ya simu inaruhusu mianya ya taarifa za watumiaji kuvuja na hakuna anayesema, wote tunajua kuwa dunia ya sasa inaongozwa na taarifa/data na kama tutaacha tabia hii iendelee hatuwezi kuwa salama VODACOM BADILIKENI
Hujamuuliza aliagizwa na nani? Na ulichukua hatua gani zaidi? Yawezekana hata vodacom hawahusiki ndio maana wamekujibu hivyo
 
Pole ...iwe kweli au sio kweli ila nakampuni ya simu yameajiri kwenye customer care vijamaa very incompetent upstairs, huwa viatoa majibu ya kipuuzi sana kwa issue za msingi kibaya zaidi eti kanamaliza kwa kukuambia "je una tatizo lingine".....hata kama beio cheap labour ila vinauzi zana!
True that
 
Usipende sana kuhukumu kabla ya uchunguzi.
Angalie usijekugeuziwa kibano.
JF sio sehemu salama sana kutapika uchachu.
 
Sasa taarifa za fundi umeme ndo za kuja kulia liaa hapaa...??? Mumbwaa kabisaa
Taarifa yoyote ina thamani kubwa. Taarifa ni rasilimali. Kama leo ameweza kupata mchongo wa ufundi umeme, siku nyingine atapata taarifa ya nini? Hakuna taarifa ndogo.
 
Hili swala nilikutana nalo siku moja, nilienda kuweka pesa Mpesa wakala elfu 20 mara tu baada ya dk 20 nikapigiwa simu na mtu nisiye mjua ananiambia nimeka pesa hvyo nimejishindia kiasi fulani cha pesa.

Akaniuliza nimeweka kiasi gani na kwenye acc kuna kiasi gan? Nikapata wasiwasi nikamwambia endelea.

Kwa jinsi nilivyokuwa namjibu kwa ufupi badae nikamwambia chautapeli akanijibu atakula wapi hiyo ndyo kazi yake.
 
Kwanza kabisa naomba kuwasalimu wote,

Baada ya hapo kama kichwa cha uzi kinavyojieleza naomba kueleza jinsi ilivyokuwa hadi mimi kufikia hatua ya kusema kuwa VodaCom wamevujisha taarifa zangu za mawasiliano

Leo majira ya saa nane mchana, niliwasiliana na mwenye nyumba wangu kuhusu tatizo la shoti ya umeme hapa nyumbani, kwanza nilipigia simu hakupokea, nikajua huenda amebanwa na shughuli zingine hivyo nikamtumia SMS ili atakapoiona anitafute, katika sms hiyo nilieleza kuhusu tatizo lililopo.

Baada ya kama dakika 10-15, nikapokea simu (naomba namba iliyonipigia niihifadhi) huyo aliyenipigia akanijulisha kuwa yeye ni fundi umeme ameagizwa aje kutatua tatizo lililopo hapa nyumbani, kwa hiyo nikamwambia sawa nitamsubiri, na hivyo akanihakiishia kufika hapa nyumbani baada ya muda mfupi, lakini ikabidi nimtafute mwenye nyumba kuthibitisha taarifa hizo maana sikuweza kuaminin kama mwenye nyumba amewasiliana na fundi moja kwa moja bila kunipigia mimi nimweleze hali ya tatizo,

Sasa baada ya kuwasiliana na mwenye nyumba akakataa kuwa yeye hajaongea na mtu yeyote kuhusu suala la umeme zaidi ya kupokea sms ambayo mimi nimemtumia, lakini pia mimi sikuwasiliana na mtu yeyote zaidi yake kuhusu suala la umeme lililotokea nyumbani.

Hivyo moja kwa moja nikapata wasiwasi kuwa mawasiliano hayo yamevujishwa na mtandao wa simu ninaotumia (VODACOM), baada ya hapo nikapiga simu huduma kwa wateja kuwaeleza kuhusu malalamiko yangu hayo hata hivyo walichoweza kunijibu hakikuwa na mashiko, kwa kuwa alinijibu tuu kwa kifupi kuwa wao hawana uwezo wa kuona taarifa za mtumiaji wa mtandao wao

Lakini pia kama si VODA waliovujisha mawasiliano haya basi miundombinu yao haina uwezo wa kuzuia wadukuzi wa taarifa za wateja

pia, nikapata wasiwasi mkubwa kuhusu uvujaji wa taarifa zetu watumiaji wa mitandao, kwa kuwa ikiwa taarifa yangu ndogo kama hiyo imevuja, najiuliza swali Je, ni watu wangapi wametapeliwa kwa sababu hii, ni watu wangapi wamevamiwa kwa kuvuja kwa taarifa zao za safari, fedha, biashara n.k,

Tutawezaje kuwa salama kama mitandao ya simu inaruhusu mianya ya taarifa za watumiaji kuvuja na hakuna anayesema, wote tunajua kuwa dunia ya sasa inaongozwa na taarifa/data na kama tutaacha tabia hii iendelee hatuwezi kuwa salama VODACOM BADILIKENI
"alinijibu tuu kwa kifupi kuwa wao hawana uwezo wa kuona taarifa za mtumiaji wa mtandao wao"
Amekujibu vizuri sana na hilo ndio jibu lako.
 
Nawaruhusu voda wavujishe taarifa zangu kwa mtu yoyote isipokuwa kwa WALE WATEKAJI NA WAUAJI WA KIJITONYAMA...sasa wewe kama voda wamekutafutia fundi umeme kuna shida gani???!!! ( in mzee meko's voice), siku ukiumwa watakutafutia ambulance...
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom