Vodacom na bado mtafilisika kabisa

Vodacom na bado mtafilisika kabisa

Hawa si hawana MD, au ni kumuwekea mtego MD mpya akija kama akiwa mbongo wadai kaifikisha vibaya.nawaza kwa kina.
 
Mimi naendelea kukomaa tu na halotel ndo mtandao wangu usio na longolongo kweny internet mda wote
 
Niliacha kuweka vocha VODA last year li laini limekaa kwenye simu kama pambo.

Niligundua mchezo wa wizi wizi siku nyingi nikaona kwanini niumize roho yangu.
 
Mkuu umenicha njia panda ukivomalizia. Hiyo '..bure kwa sh 500' kama sijaielewa
Maana yake ukilipia 500 unapata dakika 30 vod to vod 20 all net pamoja na Mb500 whatsapp,facebook and instagram ni free.means unapotumia hizo tatu mb zako 500 hazikatwi had uingie kwenye sites zingine ndio hizo zitatumika...ila kwa wateja wa dar tu...nimetumia mitandao mikubwa yote ila voda inawikimbiza wote mbali saana
 
voda ukikwangua vocha ukasahau kuweka kwenye cm wanakata hata ikiwa mezani, ukanunua halaf hujaikwakungua jinsi walivyo waroho wanakutext "mbona hukwangui hio vocha? Ita expire ujue" wajamaa ni waroho kana kwamb hata kama simu imezima charge, ukipitsha vocha tu karibu cm inawaka au inavibrate kukushtua. Blv me, sisemag uongo wala hata sijui bang ikoje
 
Hawa Vodacom Tanzania nilishaacha kununua vifurushi vyao. Nimebaki natumia kwenye Mpesa tu.
Mara ya mwisho nimejiunga na kifurushi cha dar supa UNI wakanipa Data GB1 na madakika, ukiwasha data simu inasoma 4G ila huwez ku-browse website yoyote (hata gugo iligoma) nikahisi labda niko location mbaya nikaenda maeneo mengine pia mambo ni hayo hayo. Hadi wiki inaisha sikumaza hata MB 1. Nyie voda nyie Mungu anawaona
Hapana mkuu mnyonge mnyongeni na haki yake mpeni... mie huwa natumia TMk supa uni... wako vzuri sana kwa siku 7 unapata dk 150 voda kwenda voda,dk 50 mitandao mingine,sms 2000,GB 1 za internet then watsap na fb bure vyote hivo kwa sh. 2000/= sasa hapo kweli ntaanzia wapi kuwalaumu
 
voda ukikwangua vocha ukasahau kuweka kwenye cm wanakata hata ikiwa mezani, ukanunua halaf hujaikwakungua jinsi walivyo waroho wanakutext "mbona hukwangui hio vocha? Ita expire ujue" wajamaa ni waroho kana kwamb hata kama simu imezima charge, ukipitsha vocha tu karibu inawaka. Blv me, sisemag uongo wala hata sijui bang ikoje
Mmmmmhhh, tembelea JF uone maajabu
 
Kumbe ndiyo maana wamiliki wa vodacom walimteua mkenya kuwa mkurugenzi mkuu...wanajua tatizo liko wapi na namna ya kulirekebisha ilikuwa ni kumleta mtu anayeijua vizuri hii biashara.
 
Hapana mkuu mnyonge mnyongeni na haki yake mpeni... mie huwa natumia TMk supa uni... wako vzuri sana kwa siku 7 unapata dk 150 voda kwenda voda,dk 50 mitandao mingine,sms 2000,GB 1 za internet then watsap na fb bure vyote hivo kwa sh. 2000/= sasa hapo kweli ntaanzia wapi kuwalaumu
Mwenyewe natumia hii na inanisave sana.
 
Hapana mkuu mnyonge mnyongeni na haki yake mpeni... mie huwa natumia TMk supa uni... wako vzuri sana kwa siku 7 unapata dk 150 voda kwenda voda,dk 50 mitandao mingine,sms 2000,GB 1 za internet then watsap na fb bure vyote hivo kwa sh. 2000/= sasa hapo kweli ntaanzia wapi kuwalaumu
Hata mimi binafsi sina sababu ya kuhama voda kabisa.
Kwa sh 1500=150 min (voda-voda) 15 min (all ntws) 1gb +1gb night (total 2gb) ulimited sms, free facebook, whatsapp and instagram.
Kwa sh 2000 ndio kama ulivyosema hapo juu hata mimi ninacho cha Dar supa UNI.
Hivi ni mtandao gani naweza pata ofa hii! tigo wenyewe kifurushi cha chuo wanapewa sijui dk 100 tena za tigotigo na mb hazizidi 50,halafu kwa 1500 iyo hiyo.
 
Kampuni kubwa ya kimataifa haina mikakati ya kibiashara,mnachekesha mno,na kama hakuna MTU anayewahujumu basi pigeni chini management yote ya "Sales and Marketing".
yaani nyie mna tabia zote za kichawi, kila siku mnabuni mbinu za kuwakamua wateja wenu,matokeo yake mnapoteza zaidi ya mil 200 kila wiki,Mteja aliyekuwa akipata MB au vocha kwa sh 500 per week ,sasa hivi mmeweka eti sh 20,000 kwa mwezi,mnadhani pesa zinaokotwa?
kwa hiyo mmepoteza zaidi ya wateja 100,000 ambao mlikuwa mkipata zaidi ya mil 30 kwa siku faida tu,after tax payment, 100,000 x 300=30,000,000.
nawafahamu mno aina ya watu mliowaajiri,lazima mfilisike tu,sijui walisoma uchumi wapi,kwa tuliosoma uchumi tunatambua slogan hii " the less money,the more money, the more money, the less money".
wapunguze bei la sivyo tunasepa
 
Nikiwa kama mtumiaji wa Voda nasema voda ndio mtandao wenye viwango nchi hii kama unataka MB 500 na unaish Dar kuna kifurushi cha Dar mb 500 instagram,whatsapp and facebook ni bure kwa sh 500

Kama offers ni za huko dar tu basi tumieni nyie nyie wa huko dar
 
Nikiwa kama mtumiaji wa Voda nasema voda ndio mtandao wenye viwango nchi hii kama unataka MB 500 na unaish Dar kuna kifurushi cha Dar mb 500 instagram,whatsapp and facebook ni bure kwa sh 500
bado ni uhuni tu we nipe mb sio unichagulie face book au instagram
 
Nikiwa kama mtumiaji wa Voda nasema voda ndio mtandao wenye viwango nchi hii kama unataka MB 500 na unaish Dar kuna kifurushi cha Dar mb 500 instagram,whatsapp and facebook ni bure kwa sh 500
Wewe data yako ni maalumu kwa fb, insta na whatsapp?
Mb 500 kwangu siyo ishu
 
IMG_20180520_075615.png
 
Mbona umemtusi bila sababu? Kasema voda iko poa, umemrudishia matusi!

Ndo wabongo walivyo
Tena sasa hivi wameongeza kifurushi kingine kwa mia tano wanakupa units 500 kwa week ambapo unit moja ni sawa na dakika moja voda kwa voda (maana yake ni dkk 500 ) na units tano ni dakika moja kwa mitandao yote (maana yake ni dakika 100 ) na unit moja ni sawa na MB 1
 
Back
Top Bottom