trachomatis
JF-Expert Member
- Jun 7, 2011
- 3,758
- 736
Miezi miwili iliyopita nilikuwa jijini Dar...
Nilinunua vocha tajwa nikaikwangua(scratch),bahati mbaya ikakwanguka vibaya... Nilipowapigia kitengo cha huduma kwa wateja na kueleza tatizo langu,walisema niende kwenye ofisi za Airtel zilizo karibu na mimi.
Nilipouliza kama nikiwatajia "serial number" ya vocha hiyo hawawezi kunisaidia,walinijibu hawawezi zaidi ya ushauri wa kwenda kwenye ofisi za Airtel.
Ingawa nikiwa Dar,naishi Kinondoni,Block 41,sikuona ulazima wa kufunga safari ya kwenda kuomba kubadilishiwa vocha hiyo. Niliona ni usumbufu kwa mteja.
Nilikuja kuigawa kwa watoto wiki mbili zilizopita. Wao walifanikisha kuingiza tarakimu zilizoharibika,wakafaidika nayo.
Jana nilinunua tena ya thamani hiyohiyo,ikaharibika vibaya mno! Nikaitunza na nikaamua kununua nyingine na kumwambia muuzaji anikwangulie.. Jirani yangu naye alifika na kuagiza vocha ya aina hiyohiyo akakwangua vibaya naye pia. Naye akalazimika kununua nyingine.
Nikatoka hapo nikaenda kwenye duka lingine lenye kutoa huduma ya tigo pesa,airtel money,na m-pesa. Nilipohadithia kisa changu,dada mmoja alidakia na kusema alipata kuona mtu akipata hasara ya sh 2,000 kwa vocha aina hizo. Na bwana mmoja naye alisema yeye amepata balaa kama hilo mara sita!
Je wenzangu mmepata masahibu kama yetu?
Nilinunua vocha tajwa nikaikwangua(scratch),bahati mbaya ikakwanguka vibaya... Nilipowapigia kitengo cha huduma kwa wateja na kueleza tatizo langu,walisema niende kwenye ofisi za Airtel zilizo karibu na mimi.
Nilipouliza kama nikiwatajia "serial number" ya vocha hiyo hawawezi kunisaidia,walinijibu hawawezi zaidi ya ushauri wa kwenda kwenye ofisi za Airtel.
Ingawa nikiwa Dar,naishi Kinondoni,Block 41,sikuona ulazima wa kufunga safari ya kwenda kuomba kubadilishiwa vocha hiyo. Niliona ni usumbufu kwa mteja.
Nilikuja kuigawa kwa watoto wiki mbili zilizopita. Wao walifanikisha kuingiza tarakimu zilizoharibika,wakafaidika nayo.
Jana nilinunua tena ya thamani hiyohiyo,ikaharibika vibaya mno! Nikaitunza na nikaamua kununua nyingine na kumwambia muuzaji anikwangulie.. Jirani yangu naye alifika na kuagiza vocha ya aina hiyohiyo akakwangua vibaya naye pia. Naye akalazimika kununua nyingine.
Nikatoka hapo nikaenda kwenye duka lingine lenye kutoa huduma ya tigo pesa,airtel money,na m-pesa. Nilipohadithia kisa changu,dada mmoja alidakia na kusema alipata kuona mtu akipata hasara ya sh 2,000 kwa vocha aina hizo. Na bwana mmoja naye alisema yeye amepata balaa kama hilo mara sita!
Je wenzangu mmepata masahibu kama yetu?