Vocha ya Airtel ya Tshs 1000/- ....... !!!

Vocha ya Airtel ya Tshs 1000/- ....... !!!

ukiwa na coin unakwangua lightly, sio utumie miguvu mpaka jasho linakutoka. Si kwa airtell tu bali mitandao yote

Sawa sijakataa.. Ila.. Kuna kitu kinaitwa malalamiko baada ya kuathirika.. Mi nimeanza kutumia simu ya mkononi tangu 2000. Mambo ya vocha mpaka nalalamika,ni kwamba yamenikuta na mpaka napost uzi huu,ni baada ya kusikia wengine wameathirika,na kuona mwenzangu akinunua mara mbili vocha.

Kwa maana hiyo suala si kukwangua kwa nguvu,maana vocha haziuzwi benki ili tuseme tukwangue kwa nidhamu. Hivyo nguvu hutegemea na mazingira unayoweka vocha yako. Wengine wanakwangulia juu ya goti,kwenye dash board ya gari,wengine hugeuza simu zao na kukwangulia juu yake,wengine wanatumia mchanga,wengine wanakwangua huku wakitembea..
Na wasipate matatizo yeyote na vocha nyingine isipokuwa za Airtel,tena za buku...

Anyway,ni mojawapo ya maoni...
 
Pole sana, ila kwa kuwa sasa umeshalijua tatizo, chukuwa tahadhari au mwachie anayekuuzia aikwangue kisha akusomee namba tu.

Asante kwa ushauri... Nami ndiyo hatua niliyochukua jana..
 
Trachomatis, unajua humu JF kuna watu wamezoea mizaha na hata kama jambo hawalijuia maadamu wana access na mtandao basi wataweka utumbo wao. Kama ingalikuwa katika mazungumzo basi ningaliwaita waropokaji.

Hoja yako ni ya kweli. Na kiuchumi inamadhara makubwa.

Siku alipokuwa anazikwa Mar Regia, nalinunua vocha za 1000/= mbili pale Moro mjini. Zote zilichubuka nikashindwa kuingiza. Nilipomwambia mwenye duka akaniambia hajui kwanini zinachubuka, kisha akanishauri niende ile ofisi ya Airtel Moro. Nilifanya kama nilivyoelekezwa.

Nilipofika pale ofisini, mhudumu kwa wateja (kijana wa kiume) akaniambia hana namna ya kunisaidia zaidi ya kuzichukua zile vocha na kuwajulisha Makao Makuu, wao wataniingizia muda wa hewani kwenye simu yangu. Akaniomba nimpe zile vocha. Akabandika kwenye karatasi na kando yake akaandika namba yangu ya simu.

Nikiwa namuhoji maswali mazito, ndipo akanionyesha karatasi nyingine 4 ambapo @ ilikuwa na wastani wa vocha 30-40 zimerudishwa. Pia kukawa na kopi 6 za namna ya karatasi hizo ambazo zile zenye vocha halisi alikuwa ametuma Dar. Akanambia kuna vocha zilizoletwa zina matatizo, hivyo wameitambua batch husika na wameizuia kuisambaza. Na zile zilizoingia sokoni hawajaanza kuzirudisha.

Hadi leo hii hiyo 2000/= hawajanirudishia. Niliwahi kuwapigia customer service nikawatajia serial no. zake wakaniambia nisubiri sekunde chache nisikate simu. Mara simu ikakatika, sikukata mimi. Toka hapo kila nikiwapigia naishia kwenye kale kawimbo tu. Sipokelewi.

Wiki iliyopita nilinunua vocha pale maeneo ya Manyanya. Ilikwanguka tarakimu tatu. Nimeitunza hiyo vocha ('cause that is money). Nangojea siku nitakaposaidia kwa hizo mbili, naunganisha na hiyo.

Sasa hebu tufikiri ni kiasi gani zipo kwenye mzunguko? Ni kiasi gani cha pesa ya watz kinapotea kwa huduma sifuri?

Airtel wanatakiwa kulishughulikia hili mapema kwa umakini na kuhakikisha halijirudii.

Mkuu Myamahodzo... Afadhali umenielewa na ni bahati kuwa wewe mwenyewe ni shuhuda wa tukio hilo. Tena ushuhuda wako ni kama vile umejibu hoja zangu na za waathirika wengine..

Kuhusu tabia za watu humu JF,ni kweli kuna watu wana matatizo hadi unashindwa kuelewa kama huko kuchangia nyuzi wamelazimishwa ama la...
 
Mkuu Myamahodzo... Afadhali umenielewa na ni bahati kuwa wewe mwenyewe ni shuhuda wa tukio hilo. Tena ushuhuda wako ni kama vile umejibu hoja zangu na za waathirika wengine..

Kuhusu tabia za watu humu JF,ni kweli kuna watu wana matatizo hadi unashindwa kuelewa kama huko kuchangia nyuzi wamelazimishwa ama la...

Tuko pamoja mkuu!

Airtel wanatakiwa kuchukua hatua za haraka kwa hili.
 
hata mimi nimepata tatizo kama hilo.ukweli ni kwamba vocha za 1000 za airtel zina matatizo,me nimepata hasara ya 2000
 
hata mimi nimepata tatizo kama hilo.ukweli ni kwamba vocha za 1000 za airtel zina matatizo,me nimepata hasara ya 2000

Pole sana Sweet G... Ndiyo maana tunashirikishana mambo kama haya...
 
Pole sana, ila kwa kuwa sasa umeshalijua tatizo, chukuwa tahadhari au mwachie anayekuuzia aikwangue kisha akusomee namba tu.
niligundua kabla ya kukwangua kuwa imechubuka ! Nikaitema !
 
niligundua kabla ya kukwangua kuwa imechubuka ! Nikaitema !

Kutokana na maelezo ya mkuu Mnyamahodzo....
Airtel hawana mpango wowote wa kurekebisha tatizo lililopo,au walau kutusaidia kwa ile huduma ya customer care ili kuitambua na kumrudishia salio mteja kwa njia yeyote mbali na kwenda kwenye "ofisi zilizo karibu nasi"
 
Scratchly gently jamani hamuoni hiyo.Hasara zingine za kujitakia.
 
Miezi miwili iliyopita nilikuwa jijini Dar...
Nilinunua vocha tajwa nikaikwangua(scratch),bahati mbaya ikakwanguka vibaya... Nilipowapigia kitengo cha huduma kwa wateja na kueleza tatizo langu,walisema niende kwenye ofisi za Airtel zilizo karibu na mimi.

Nilipouliza kama nikiwatajia "serial number" ya vocha hiyo hawawezi kunisaidia,walinijibu hawawezi zaidi ya ushauri wa kwenda kwenye ofisi za Airtel.
Ingawa nikiwa Dar,naishi Kinondoni,Block 41,sikuona ulazima wa kufunga safari ya kwenda kuomba kubadilishiwa vocha hiyo. Niliona ni usumbufu kwa mteja.
Nilikuja kuigawa kwa watoto wiki mbili zilizopita. Wao walifanikisha kuingiza tarakimu zilizoharibika,wakafaidika nayo.

Jana nilinunua tena ya thamani hiyohiyo,ikaharibika vibaya mno! Nikaitunza na nikaamua kununua nyingine na kumwambia muuzaji anikwangulie.. Jirani yangu naye alifika na kuagiza vocha ya aina hiyohiyo akakwangua vibaya naye pia. Naye akalazimika kununua nyingine.

Nikatoka hapo nikaenda kwenye duka lingine lenye kutoa huduma ya tigo pesa,airtel money,na m-pesa. Nilipohadithia kisa changu,dada mmoja alidakia na kusema alipata kuona mtu akipata hasara ya sh 2,000 kwa vocha aina hizo. Na bwana mmoja naye alisema yeye amepata balaa kama hilo mara sita!

Je wenzangu mmepata masahibu kama yetu?

Mie pia iliwahi nipata hapa Nzega ati nikaambiwa niende ofisi yao iliyoko Mwanza. Ebu piga nauli kutoka Nzega hadi Mwanza! Naona hawa wako kibiashara zaidi wala si kutoa huduma. Poleee....!
 
imewahi nitokea pia nilikuwa naenda nchi jirani nikanunua vocha pale Namanga na ikawa hivo hivo kama vile imeloweshwa kwenye maji nikaitupa lakini vile vile ikajanitokea tena hapa hapa dar
 
hiyo ni kamali ya lazima, bila ridhaa ya kuingia, na ina wizi ndani.
 
Mie pia iliwahi nipata hapa Nzega ati nikaambiwa niende ofisi yao iliyoko Mwanza. Ebu piga nauli kutoka Nzega hadi Mwanza! Naona hawa wako kibiashara zaidi wala si kutoa huduma. Poleee....!

Yaani wanazingua sana wateja wao...
 
imewahi nitokea pia nilikuwa naenda nchi jirani nikanunua vocha pale Namanga na ikawa hivo hivo kama vile imeloweshwa kwenye maji nikaitupa lakini vile vile ikajanitokea tena hapa hapa dar

Tuko wengi yaani inabidi kama hii thread wanaisoma,wachukue hatua..
 
hiyo ni kamali ya lazima, bila ridhaa ya kuingia, na ina wizi ndani.

Nadhani Airtel tunao humu ndani kama wadhamini mojawapo wa JF..
Watakuwa wanasoma maoni yako..

Kiukweli ni kilio cha wengi...
 
hili nph tatizo.ninavocha ya airteltoka mwaka jana mwishoni.imeharibika nambana bado sijapata msaada
 
hili nph tatizo.ninavocha ya airteltoka mwaka jana mwishoni.imeharibika nambana bado sijapata msaada

Kuna mkuu hapo Mnyamahodzo..
Yeye ana majibu ya maswali yako.. Ila kwa ufupi,hawa jamaa hawajali wateja wao in terms ya unnecessary cash utilization to their customers..
 
Vocha za airtel za 1000 ni nyepesi kuharibika, mi mwenyewe hapo majuzi nlikwangua ikaharibika, nikapiga huduma kwa wateja wakanambia niende kwa mawakala ndo wanisaidie. Wakati swala ni kutaja serial number mchezo unaisha. Sidhani kama hawa jamaa wanatujali wateja!
 
Back
Top Bottom