Messenger RNA
JF-Expert Member
- Jul 24, 2022
- 1,102
- 3,022
Nawasalimu wote kwa jina la Jamhuri ya Muungano.
Vijana tunapitia mengi ya kukatisha tamaa, lakini leo niwape machache ya vituko vya sahili nilivyowahi kuviona kwa macho yangu.
1. Tuliitwa kwenye usahili mikoa ya nyanda za juu kusini, basi kwa furaha na kujiamini nikapaki vitu huyooo nikafika siku moja kabla nikaripoti na nikakuta watu wengine, siku ya pili yake tukawahi sana tu,basi wakati tunaendelea kusubili wasahili wakafika na gari aina ya cruiser wakashuka kama saba hivi, sisi tukajua wote ni wasahili, lahaula kumbe wengine ni wasahiliwa kama sisi na tuligundua baada ya kuona wanakuja kukaa kwa wasahiliwa. Baada ya usahili matokeo nakuachia utabiri mwenyewe.
2. Tuliitwa kwenye usahili wa serikali basi wakati tunaendelea kusahiliwa basi kuna kijana sijui wa mkubwa gani akawa ameondoka eneo lile, basi unaambiwa alitafutwa balaa na mwisho wa siku matokeo yumo.
3. Kuna siku tunasubiri usahili, kuna vijana wakawa wanasema wameagizwa kuja hapo kama utani vile, aisee haikuwa utani matokeo yalitujulisha.
4. Tumefanya usahili, matokeo watu ambao hawakuwepo kwenye usahili ndio waajiliwa.
5.Umetoka umejiandaa na kile ulichosomea mfano mechanical engineering na vile vitu vinavyoendana na umejiandaa haswaa,unaingia wanaanza kukuzodoa,mara huyu aulize mambo ya demokrasi yaani ni ujinga tuu maadamu wakukere tu maana hawana mpango na wewe ni vile umekuja acha wapoteze tu muda, inakera acha tu.
Dah mambo ni mengi sana, ushauri wangu vijana msio na connection mkaze sana na kumuomba Mungu, lakini naamini kila kitu kinawezekana.
Kama una kisa ni ruhusa kuweka.
Vijana tunapitia mengi ya kukatisha tamaa, lakini leo niwape machache ya vituko vya sahili nilivyowahi kuviona kwa macho yangu.
1. Tuliitwa kwenye usahili mikoa ya nyanda za juu kusini, basi kwa furaha na kujiamini nikapaki vitu huyooo nikafika siku moja kabla nikaripoti na nikakuta watu wengine, siku ya pili yake tukawahi sana tu,basi wakati tunaendelea kusubili wasahili wakafika na gari aina ya cruiser wakashuka kama saba hivi, sisi tukajua wote ni wasahili, lahaula kumbe wengine ni wasahiliwa kama sisi na tuligundua baada ya kuona wanakuja kukaa kwa wasahiliwa. Baada ya usahili matokeo nakuachia utabiri mwenyewe.
2. Tuliitwa kwenye usahili wa serikali basi wakati tunaendelea kusahiliwa basi kuna kijana sijui wa mkubwa gani akawa ameondoka eneo lile, basi unaambiwa alitafutwa balaa na mwisho wa siku matokeo yumo.
3. Kuna siku tunasubiri usahili, kuna vijana wakawa wanasema wameagizwa kuja hapo kama utani vile, aisee haikuwa utani matokeo yalitujulisha.
4. Tumefanya usahili, matokeo watu ambao hawakuwepo kwenye usahili ndio waajiliwa.
5.Umetoka umejiandaa na kile ulichosomea mfano mechanical engineering na vile vitu vinavyoendana na umejiandaa haswaa,unaingia wanaanza kukuzodoa,mara huyu aulize mambo ya demokrasi yaani ni ujinga tuu maadamu wakukere tu maana hawana mpango na wewe ni vile umekuja acha wapoteze tu muda, inakera acha tu.
Dah mambo ni mengi sana, ushauri wangu vijana msio na connection mkaze sana na kumuomba Mungu, lakini naamini kila kitu kinawezekana.
Kama una kisa ni ruhusa kuweka.