Vituko mitandaoni. Tupia chako

Vituko mitandaoni. Tupia chako

1698010855608.png
 
Mwambie anipigie ni mimi mama yake!!mwambie sina simu ila nimeona picha zake kwenye simu ya kupalaza ya khamisi/mwambie amenenepa sana ..mwambie nimeona gari lake ni zuri sana !!ila mwambie mama yake bado naishi kwenye lile banda pamoja na kuku/mwambie nimeumwa sana ila nikapona bila hata kutumia dawa/mwambie mzee juma bado ananidai pesa zake nilizokopa ili nimlipie ada amechukua kile kishamba nilichokuwa nakitegemea kufidia deni lake/mwambie mimi mama yake nimebaki pekee yangu tangu baba yake afariki sina hata wa kunisogezea kuni motoni/mwambie leo nimetamani sana nyama zile mboga zilizoota zenyewe upenuni zimenichosha mpka mdomo umekuwa mchungu/mwambie wale vijana walitaka wanipige eti mimi mchawi eeh/mwambie mama yake nimekuwa mzee sana nahesabu siku tu aje hata nishike mikono yake nimuoneshe mipaka ya nyumba yetu/!!salio limeisha mwambie mama anampenda sana!ila huku kijijini nimebaki pekee yangu wenzangu wote wameenda mjini kusherekea kwa watoto wao...

Tuwapende mama zetu wale tulojaaliwa kuwa nao hadi leo waliotangulia mbele za haki tuwaombee kwa mola awaweke mahali pema peponi
View attachment 2789696
Tuwapende mama zetu wale tulojaaliwa kuwa nao hadi leo waliotangulia mbele za haki tuwaombee kwa mola awaweke mahali pema peponi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom