Vituko mitandaoni. Tupia chako

Vituko mitandaoni. Tupia chako

1685719001694.jpg
 
Habari za asubuhi.
Updates za uwepo wa Simba tangu Tarehe 30.05.2023.
- Simba hao waliingia muheza kutokea Masaika.
Siku ya Tarehe 28 na 29 Kwa upande wa Masaika unaopakana na muheza walikula Punda mmoja na Mbuzi mmoja, siku ya Tarehe 30 walibainika kuwepo upande wa muheza baada ya kuonekana Kwa nyayo zake, usiku WA Tarehe 30 kuamkia Tarehe 31 katika kijiji cha Mpapayu aliliwa Punda mmoja, Jana Tarehe 01.06.2023 nyayo zake majira ya asubuhi zilionekana katika kijiji cha Tanganyika kata ya Lusanga, ambapo baadaye jioni tulipokea taarifa za uwepo wao kitongoji cha kizota kijiji cha Mlingano. Usk WA kuamkia Leo Tarehe 02 kitongoji cha Mshukuruni kijiji cha kwalubuye mwenyekiti ameripoti kuwa usk ng'ombe mmoja ameliwa. Hivyo, Hali bado si salama kwakuwa bado hatujafanikiwa kukutana nao, pia mashambulizi Yao yamekuwa ya wakati wa usk.
Mhe. Mkuu wa Wilaya anasisitiza tuendelee kuchukua tahadhari katika kipindi hiki.
Aidha, wataalam wa Wanyamapori kutoka TAWA wako muheza na tunategemea kupokea wengine kutoka TAWIRI.
Ahsanteni
OBADIA MSEMO
AFISA MALIASILI
MUHEZA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom