Uongo ni shida..
Jumapili iliyopita baada ya ibada Kanisani, Mchungaji akamuona Petro akiperuzi simu aliyonunua kwa sh 650,000 hivi karibuni..
Mazungumzo yakawa hivi:
Mchungaji: mtumishi Petro, simu nzuri hii..
Petro: naam, asante Mchungaji
Mchungaji: uliinunua lini?
Petro: kama wiki 3 hivi zilizopita
Mchungaji: Kwa bei gani?
Petro: (kwa kuwa huwa hatoi sadaka wala ZAKA, akawaza kuwa akisema kweli italeta picha mbaya..,) ni sh elfu 50 tu Mchungaji..
Mchungaji: oohoo, vizuri sana. Ebu nisubiri hapa..
Petro: sawa
Mchungaji: chukuwa laki moja hii hapa, Kesho uniletee simu 2 kama hii yako Kwa ajili ya mimi na mama Mchungaji..
Petro: sawa..
Saivi Petro anahangaika kutafuta mkopo wa haraka wa riba nafuu akanunulie hizo simu🙄