Vituko mitandaoni. Tupia chako

Vituko mitandaoni. Tupia chako

Mke na mumewe..​

MKE: Mbona unanukia pafyumu ya kike?
MUME: Yaa kuna mwanamke tulikuwa tumeminyana ndani ya daladala
MKE: Na lipstiki kwenye shati?
MUME: Tulikumbatiana na wageni toka Zambia walitembelea ofisi yetu
MKE: Na ile kondom iliyotumika kwenye mfuko wa suruali?
MUME: Bwana eeeeh... wacha maswali ya kijinga mi nalala nina usingizi
MKE: Lazima niulize, maana mie huwa nahakikisha nimeacha kila kitu hukohuko ndio narudi nyumbani..
MUME: Umesema nini wewe?
MKE: Bwana eeeeh, wacha maswali ya kijinga mi nalala nina usingizi🙄
 

Nyama..​

Jamaa kaenda kumtembelea rafiki yake Levi, kule sehemu za kwetu, akakaribishwa bonge ya ugali na nyama nyingi tu..
Wakati anakula akagundua kuwa shemeji yake, mke wa rafiki yake hali nyama;

JAMAA: Halloo, hili ni bonge ya lanchi aise, lakini Levi mbona sisi tu tunakula nyama shemeji Gulo hagusi kabisa anaishia mlenda tu? Tabia gani hii?
LEVI: Hapana, sijamkataza, ila shemeji yako Mngoni halagi nyama ya FISI kama sisi😁
JAMAA: Duuuuh! Mbona kama naanza kusikia kizunguzungu humu tumboni mwangu aise🤔
 

Babu​

Babu: Mjukuu wangu ngoja nikusimulie hadithi ya mimi babu yako kwenye vita ya kagera
Mjukuu: Niambie babu
Babu: Kwenye vita ya kagera tulienda sehemu, askari wote tukakamatwa na maadui, wakatuambia chagueni kuuliwa au kubakwa.
Mjukuu: Sasa babu wewe ulichagua nn?
Babu: Niliuliwa!!!
 

Tofauti ya mwanamke wa Kizaramo, Kitanga, Kihaya, na wa Kichaga..​

Mwanamke wakizaramo: Unampa hela ana nunua dela anaenda ana msutia jirani, analivaa dela bila nguo ya ndani mbele yako, unazidiwa anakupa kitu fresh unatoka unatabasamu.

Mwanamke wa kitanga:
Unampa hela anapika vitu mtaa mzima unasikia harufu ya chakula, chenji inayo baki ananunua kinga ukirudi unakula afu unakula..

Mwanamke wa kihaya:
Unampa hela, ukirudi unakuta majirani wote wanataarifa kuwa wewe uliacha hela, anakupkia vitu vzuri, usiku anakuhudumia... ukimsifia anakuhudumia tena hata mara sita kwa usiku mmoja... wee mle, sifa tu..

Mwanamke wa kichaga:
Unampa hela, anaenda ananunua dagaa anapika na michuzi mingi mpaka dagaa wanafufuka unakula kwa shida, dagaa wanakula utumbo wako unazimia...
Madaktari wanajitahidi wanakutibu unafufuka. Ukiwa hujapata akili vizuri anakuletea bili ya umeme, anakukumbusha deni la kwa Massawe, anakukumbusha kodi ya nyumba.. unashikwa na presha unaaga mazima🙄
 

Jamaa aokota wallet yenye pesa..​

Jamaa aliokota wallet, alipofika nyumbani akafungua radio akatafuta station iliyokuwa na kipindi cha wasikilizaji kupiga simu..

“Naitwa John nimepiga simu kutangaza kuwa nimeokota wallet ndani ina laki 9, ATM Card na kikaratasi chenye PIN ya ATM Card na kijimkufu cha dhahabu kinene hivi…”

Mtangazaji:- Akhasante sana John, kwa hiyo ungependa kumrudishia mwenyewe... kama ana kusikiliza akutafute kwa namba Gani!?

John: Hapana, asinitafute tafadhali.. mi nilikuwa namshukuru tu maana amenitoa kwenye matatizo na ninapenda kumuombea Dedication wimbo wa Snura “MAJANGA” umfikie popote pale alipo…!!!
 

Ajira buana..​

Jamaa mmoja alienda kuomba kazi Mbuga ya Wanyama, akaambiwa nafasi ya Kazi ipo ila hakuna Sokwe, “hivyo utajifanya Sokwe na tutakupa ngozi utavaa”

Jamaa siku ya kwanza akavaa, walipokuja watalii mambo yalienda vizuri..

Siku iliyofuata Banda lake liliwekwa juu ya Banda la Simba, Jamaa ktk kuongeza mbwembwe akawa anarukaruka, kwa bahati mbaya si akaangukia ndani ya Banda la Simba, akawa anapiga kelele “Mama nakufwaaa!”

Mara yule Simba akamwambia “Acha Ufala ww kelele za nini sasa, mimi mwenyewe Binadamu!

Rudi kwenye Banda lako kabla watalii hawajaja watatushtukia!"

Chezea ajira wewe!!!

 

Huyu mke ni shida!​

MUME: “Unajua mi unanishangaza sana, kila siku nakusikia mara useme TV yangu, gari yangu, chumbani kwangu, mara hoo watoto wangu. Sisi ni mke na mume, kila kitu ni chetu. Jirekebishe bwana"

MKE: Yuko kimya anaendelea na shughuli zake za kupekua kabatini kama hasikii, na hakumjibu kitu mumewe

MUME: (akamuuliza kwa hamaki),”Sasa hapo unatafuta nini?”

MKE: “Sidiria yetu.."🙄

MUME: (kamfungia kabatini alafu kamwambia). “nipo chumbani"
 
JamiiForums809586372.jpg
JamiiForums-345636871.jpg
 
Back
Top Bottom