Vituko mitandaoni. Tupia chako

Vituko mitandaoni. Tupia chako

FB_IMG_1660815155127.jpg
 

Masai na Taxi​

Baada ya kupanda daladala aina ya DCM kutoka Mbagala mpaka Mbezi na kulipa sh 1000. Masai akachukua tax wakati wa kurudi, walipofika sasa shughuli ilikuwa hivi...

Masai: we dureva? Naulisa Ng’ombe na mbusi ipi ngali?
Dreva: Ni ng’ombe ghali Masai.
Masai: kwanini Ng’ombe ngali?
Dreva: kwa sababu ni mkubwa zaidi ya mbuzi
Masai: umepata.. na mbusi na kuku ipi ngali
Dreva: ni mbuzi kwa sababu nae ni mkubwa kuliko kuku.
Masai: Umepatia..
Masai: sasa mie nimekwenda kule Mbezi kwa gari kubwa nikatoa sh. 1000. Sasa hii yako ndogo unasema nikupe 40,000 wewe wacha uwisi..
Nitakupa 500 tu.. Wee wacha kuibia morani buana…!!!
 

Mamba ya saluni ni shida​

SUGAR MUMMY alienda Salon kusuka.. wakati anasukwa akaingia
MKAKA mtanashati.
SUGAR MUMMY akaona isiwe shida, akaamua kurusha ndoano.
SUGAR MUMMY: Mambo?
KAKA: Poa.
SUGAR MUMMY: Mimi na wewe tunaweza kuongea baadae?
KAKA: Kuhusu nini?
SUGAR MUMMY : Nimekupenda nataka nikutoe out.
KAKA: Sawa, ila nitamwambia nini MKE wangu?
SUGAR MUMMY: Aaah ilo sio tatizo, wee mpange tu, mwambie unakwenda kumtembelea rafiki yako hospitalini.
KAKA: Haya, mwambie mwenyewe, ni huyo hapo anayekusuka..

Mtanange uliojiri baadaye ulihitimishwa Kwa Sugar Mummy kusachiwa pochi na msusi kuchukua malipo yake kamili, na Sugar Mummy kuondoka huku akiwa amesukwa nusu kichwa tuu 😊
 
Back
Top Bottom