Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,146
- 829,063
- Thread starter
- #84,121
#SIMULIZIEndelea aisee wengine hatuijui...........
MWEKA NADHIRI NASHETANI (Sehemu ya pili)
Basi mke akamwambia mumewe mwendee mtabiri wa malimwengu huenda akakupa. msaada wa kuitoa NADHIRI hii. Siku iliofata mume akafunga safari hadi kwa mtabiri wa malimwengu, alimkuta, baada ya kukaribishwa vyema akapewa kigoda akaketi, yule mtabiri wa malimwengu akamuuliza akisema bwana #IMEJIDAWA asubuhi na mapema unashida gani..? Mweka NADHIRI akamjibu akisema, Mimi niliweka NADHIRI kwamba ng'ombe wangu mara yakwanza akizaa ndama dume nitatoa pesa nimpe shetani sasa kwabahati juzi ng'ombe wakazaa ndama dume napesa nilizo ahidi kumpa shetani ninazo, lakini shetani mwenyewe simjui je nifanyeje..?
Matabiri akamwambia nitakufundisha #AYA nawe utaisoma hadi uikariri moyoni kesho asubuhi nenda kwenye ule msitu mkubwa, ukifika katikati ya msitu panda juu ya mti mrefu kuzidi yote kusha mwite shetani kwasauti ya #KUPAZA akiitika mweleze shida yako nae atakukidhia.
Basi mweka NADHIRI akahifunza ile Aya hadi ikamkaa moyoni, siku ilofata akajilawa asubuhi sana akaenda hadi msitu, akauona mti mrefu akaukwea hadi juu, kisha amaanza kuisoma ile Aya kwautulivu sana, kisha akaita "SHETANIIII SHETANIII" akasikia sauti kwambali ikimwitika "UUUUU, UUUU!!!" Mweka NADHIRI akaiambia ile sauti "Niliweka NADHIRI kwamba ng'ombe wangu akizaa ndama dume nitatoa pesa kukupa wewe bahati ng'ombe wangu kazaa dume kwahiyo njoo uchukue pesa zako nilizo kuahidi. Ile sauti ikamjibu ikisema "NENDA KAMPE MKE WANGU MIMI SITUMII PESA" mweka NADHIRI akaiuliza ile sauti "MKEO ANAITWAJE NA ANAKAA WAPI.."? Lakini ile sauti haikujibu japo mweka NADHIRI aliuliza tenanatena,, basi mweka NADHIRI alirudi nyumbani akiwa kachoka kabisa asijue la kufanya.
Je mweka NADHIRI atampata wapi mke wa shetani..? Fatilia simulizi hii hadi ujue kilicho tokea.


