#HADITHI
MWEKANADHIRI NA SHETANI.
Hapokale paliondokea mtu namkewe waliokua na ng'ombe jike ambae walimpenda sana. Wakamtafutia #FAHARI mzuri ili baadae ng'ombe wao awe #MBUGUMA. Basi mke akamwambia mumewe, ng'ombe wetu mara yakwanza akizaa ndama jike nitafanya #KARAMU niwakaribishe mabibi wote wamtaa huu, mume nae akamwambia mkewe ng'ombe wetu mara yakwanza akizaa ndama dume nitatoa pesa kumpa #SHETANI. Basi baada ya mwaka mmoja ng'ombe wao akazaa ndama dume, mke akamwambia mumewe unakumbuka ahadi ukiotoa..? Mume akajibu naikumbuka, mke akamwambia basi ahadi ile #NINADHIRI yapaswa uitimize usipo itimiza ng'ombe wetu wote watapatwa na miosi.
Mume akamwambia mkewe sasa shetani mwenyewe nitamuona wapi..? Katika kijiji kile kulikuwepo na mzee mmoja aliefanya makao yake nje kidogo ya mji, akiitwa #MTABIRI_WA_MALIMWENGU. mke akamwambia mumewe, mwendee mtabiri wa malimwengu huenda atakushauri namna ya kuitoa nadhiri hii.
Mume akakubali, siku iliofuata alifunga safari kummwendea mtabiri wamalimwengu.
Wahenga wenzangu mnaikumbuka hii..? Je niendelee kuwasimulia au inatosha..?
View attachment 2010558